BREAKING

Saturday 23 June 2018

USWIZI INA JAMBO LAKE,YATOA KICHAPO SERBIA DAKIKA ZA LALA KWA BURIANI XHAKA AVUNJA REKODI YA 1996


Switzerland imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Serbia katika mchezo wa kundi E

Mabao ya mchezo huo yamefungwa na Mitrovic mnamo dakika ya 5 tu ya mchezo kwa upande wa Serbia huku la Switzerland likiwekwa kimiani na Granit Xhaka mnamo dakika ya 52 kabla ya Xherdan Shaqiri kuongeza msumari wa mwisho dakika ya 90 ya mchezo

Xhaka ambaye hivi karibuni amesaini mkataba wa muda mrefu kuitumikia Arsenal ameweka rekodi ya kupiga jumla ya pasi 71 ambazo hazijapigwa na mchezaji yoyote wa Urusi katika michuano hiyo tangu 1996.

Matokeo hayo yanaifanya Uswizi kuwa pointi sawa na Brazil katika kundi E lakini ikishika namba 2 kutokana na idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube