BREAKING

Wednesday 6 June 2018

MAN U WAANZA FUJO ZA USAJILI, YAMSAJILI FREDY...WA BRAZIL


Klabu ya Manchester United imethibitisha kumsajili kiungo wa Brazil, Frederico Rodrigues de Paula Santos, kwa uhamisho wa paundi £52m kutoka Shakhtar Donetsk kutoka Ukraine.

Fred ambaye amejumuishwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil katika mashindano ya kombe la dunia mwaka huu huko Urusi, amesaini mkataba wa miaka mitano.

Usajili huo wa Fred kujiunga na Man United umekuwa wa kwanza kwa Kocha Jose Mourinho katika msimu huu wa majira ya joto tangu kumalizika kwa ligi kuu England.

Mshambuliaji huyo alihusika kwenye mtanange wa kirafiki kati ya Brazil dhidi ya Croatia ambapo timu yake iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Mchezaji huyo ameondoka Shakhtar baada ya kuitumikia kwa takribani miaka mitano tangu alipojiunga nayo mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube