BREAKING

Saturday 23 June 2018

'NIGERIA ILITUANGUSHA MWANZO SASA NI MOTO' RAIS WA NIGERIA ALIFUNGUKA HIVYO


Dakika 90 za mchezo wa kundi D umemalizika kwa Nigeria kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Iceland.

Mechi hiyo imekuwa ya pili kwa timu kutoka Afrika kupata ushindi baada ya Senegal kuitwanga Poland 2-1 katika mchezo wa kundi H.

Mabao yote ya Nigeria yamewekwa kimiani na Ahmed Mussa katika dakika za 49 na 75.

Matokeo hayo sasa yanakuwa yanaipa unafuu Argentina ambapo kibarua chao kijacho itakuwa dhidi ya Nigeria.


Argentina imekalia mkia kwenye kundi D kutokana na kipigo cha jana dhidi ya Croatia cha mabao 3-0.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube