BREAKING

Monday 28 May 2018

NAIBU WAZIRI MAVUNDE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA WCF KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI JIJINI MBEYA

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, akipeana mikono na mama mjane, Atulehemu Kiduko, ambaye analipwa fidia ya kila mwezi kufuatia kifo cha mumewe wakati akiwa kazini kwenye kiwanda cha karatasi Mgololo kilichoko Mufindi  mjini Iringa. mama huyo alitoa ushuhuda wa huduma anayopata kutoka WCF wakati wa kutano baina ya Serikali na wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini uliofanyika jijini Mbeya Mei 26, 2018 kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF Bw. Masha Mshomba.
  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, akifungua mkutano  baina ya Serikali na wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini uliofanyika jijinmi Mneya Mei 26, 2018 kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi.

SERIKALI ilianzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kwa lengo la kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanapata mafao bora na stahiki ya fidia tofauti na sheria ya zamani iliyotoa viwango vya chini vya fidia,  lakini pia kuwawezesha waajiri kupata muda zaidi kushughulikia masuala yao ya uzalishaji na uendeshaji.



Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, jijini Mbeya leo Mei 26, 2018 wakati akifungua mkutano baina ya Serikali na wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi.



Mhe. Mvunde alisema viwango vya juu vya malipo ya fidia kwa wafanyakazi walipokuwa wanaumia kazini kabla ya sheria ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, ilikuwa ni shilingi 108,000/=kwa mfanyakazi aliyepata ajali au kuumia kazini, lakini pia sheria inasema kulikuwa na malipo mengine ya shilingi 83,000/= kwa mfanyakzi aliyefariki kwa ajali au ugonjwa kutokana na kazi aliyokuwa akifanya na malipo hayo yalitegemea pia mkataba wa ajira yake unasemaje.

“Serikali ilikuja na sheria mpya baada ya kuona viwango hivi kwa ubinadamu na kwa hali halisi, vilikuwa vimepitwa sana na wakati na wafanyakazi walikuwa wanapata fidia hiyo kwa kadhia kubwa sana na viwango hivyo haviendani na ukuaji wa uchumi na kwa wakati tulionao.” Alifafanua Mhe. Naibu Waziri.

Aidha Mhe. Mavunde alisema, Mfuko unafaida kubwa sio tu kwa wafanyakazi bali pia kwa waajiri na taifa kwa ujumla ambapo  wafanyakazi sasa wanauhakika wa kupata kinga ya kipato kutoakana na majanga ambayo yatasababishwa na ajali, magonjwa ama vifo kutokana na kazi wanazofanya, lakini waajiri nao watapata muda zaidi wa kushughulikia masuala yao ya uzalishaji na uendelevu wa biashara na shughuli zao kwani Serikali kupitia Mfuko itabeba  mzigo wote wa gharama pindi mfanyakazi atakapofikwa na janga lolote awapo kazini.

“Pamoja na uchanga wake, Mfuko huu ambao umeanzishwa mwaka 2015 umeonyesha mafanikio makubwa katika kipindi kifupi kwani hadi sasa waajiri ambao wameshajisajili kwenye mfuko wetu ni 13,500 na wafanyakazi wao ambao wamepatwa na majanga wakiwa kazini wameshalipwa fidia na Mfuko fedha zisizopungua shilingi bilioni 2.52 kufikia Februari 2018.” Alibainisha.

Alisema Mfuko umekuja wakati muafaka kwani nchi inakwenda kwenye uchumi wa viwanda bila shaka kutakuwepo na ongezeko la ajali na magonjwa yanayotokana na uendeshaji wa shughuli katika viuwanda vyetu hivyo ni lazima kiwepo chombo kitakachosimamia majukumu haya ya fidia ili kuwapa nafasi pana waajiri kuendelea na shughuli zao za uzalishaji. 

“Rais wetu wa Jamhuri ya uungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli kila wakati tunapokutana kwenye baraza la Wafanyabiashara Tanzania amekuwa akituagiza sisi wasaidizi wake, kama kuna jambo lolote linajitokeza na sekta binafsi inafikiri kwamba jambo hili bado halijaeleweka na haliko sawasawa ni wajibu wetu sisi mawaziri kuchukua hatua haraka za kukutana na kujadiliana na wadau na kushauriana na wadau husika ili kufikia muafaka na kuelewana ili kwenda pamoja na ndio maana leo tuko hapa.” Alifafanua Mhe. Naibu Waziri Mavunde

Wakitoa ushuhuda mbele ya washiriki wa mkutano huo, Wafanyakazi waliopatwa na majanga ya kuumia au kufiwa na wenza wao, wameipongeza Serikali kwa kuanzisha Mfuko huo kwani umekuwa ni mkombozi kwa wafanyakazi.

“Mimi nilikatika vidole vya mkono wangu wa kushoto wakati nikitekeleza majukumu yangu ya kazi kwenye kiwanda cha Lake Cement kinachozalisha saruji ya nyati (Nyati cement) huko Kimbiji jijini Dar es Salaam na WCF imenilipa fidia ya mkupuo ya kiasi cha shilinhgi milioni 11, alisema Bw. Jimmy Samson Malumbo mbele ya Mkutano huo.



Mwingine aliyetoa ushuhuda wa faida ya Mfuko kwa wafanyakazi, ni mama mjane, Bi. Atulehemu Kiduko wa huko Mafinga Mkoani Iringa, alisema mumewe ambaye alikuwa mfanyakazi wa kiwanda cha karatasi Mgololo Mufindi Papers baada ya kuangukiwa na gogo wakati akitekeleza majukumu yake. Hivi sasa mama huyo mjane anapokea malipo ya fidia kila mwezi shilingi 110,000/= na watoto wake wawili kila mmoja analipwa shilingi 55,000/= kila mwezi.

“Kwakweli nimefarijika sana kwa malipo haya, ingawa nimeshampoteza mwenzangu, lakini fidia hii ninayolipwa imekuwa ikinisaidia sana katika kuhudumia familia yangu kijijini ikiwa ni pamoja na kumsomesha motto wangu  mmoja aliye darasa la tatu.” Alisema Bi. Atulehemu.

  Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba alisema Mfuko unaendeshwa kwa msingi wa utatu ambapo katika bodi ya wadhamini ambayo ina uwakishi wa serikali, wafanyakazi na uwakilishi wa waajiri kama ambavyo Shirika la Kazi Duniani linavyotaka katika masuala haya ya fidia kwa wafanyakazi.

Alisema, katika mfumo wa zamani, mfanyakazi anapotoka au kwenda kazini endapo atapatwa na tatizo njiani sheria ya zamani haikumtambua, tofauti na sheria ya sasa ambapo inaeleza mfanyaakzi akiumia au akifikwa na umauti wakati akitoka kazini au akielekea kazini sheria ya sasa inataka afidiwe.

“Alisema Mfuko umeweka utaratibu ili kuhakikisha mfumo wa usajili wa waajiri unakuwa wa haraka na rahisi lakini pia kushughulikia masuala ya ulipaji fidia katika kipindi kifupi.” Alisema.

Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga, kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi, akitoa hotuba
Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba akizungumza. 

 Sehemu ya waliohudhuria mkutano huo.
  Sehemu ya waliohudhuria mkutano huo.
  Sehemu ya waliohudhuria mkutano huo.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji, wa WCF, Bw. Anselkim Peter, akiwasilisha mada kuhusu shughuli za Mfuko.
 Mkurugenzi wa huduma za Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar, akitoa mada kuhusu namna tathmini inavyofanyika kwa Mfanyakazi aliyepatwa na madhara wakati akitelekeaza wajibu wake wa kazi.
 Mwakilishi kutoka chama cha waajiri Tanzania, (ATE), Bi. Patricia Chao, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mbeya, Dkt. Lwitiko Mwakalukwa, akizungumza kwenye mkutano huo.
 Washiriki wakipiatia taarifa mbalimbali za WCF.



 Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, (kushoto), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko huo, Bw. Anselim Peter, (wapili kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Bi. Laura Kunenge, na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalaam Omar, (aliyeipa mgongo camera), wakijadiliana jambo kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, WCF, Bi. Laura Kunenge
 Emiliana Gwagilo, Afisa Matekelezo wa WCF, akiandaa taarifa kwenye meza kuu

 Afisa Matekelezo wa WCF, Bw. George Faustin, akijibu baadhi ya hoja zilizojitokeza kutoka kwa washiriki wa mkutano.
 Mkurugenzi Mkuu wa WCF , akibadilkishana mawazo na Mkurugenzi wa Uendeshaji, Bw. Anselim Peter, (kulia), Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalaam Omar, (kushoto) na Afisa Matekelezo, Bi. Emiliana Gwagilo.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bw. Anselim Peter, (kushoto), na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, WCF, Bi. Laura Kunenge, wakiwajibika kwenye mkutano huo.
Naibu waziri Mavunde, akisindikizwa na Bw. Mshomba wakati akiondoka kwenye eneo la mkutano.

Wednesday 23 May 2018

NEYMAR AFANYIWA VIPIMO VYA AFYA, AUNGANA NA WENZAKE KWENYE MAZOEZI TAYARI KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA


Mshambuliaji nyota wa timu ya Taifa ya Brazil na PSG ya Ufaransa, Neymar Junior, amefanyiwa vipimo vya afya na tayari ameshaungana na wenzake mazoezini kujiandaa na michuano ya Kombe la Dunia huko Urusi.

Neymar alikuwa hayupo fiti tangu aumie katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya wakati PSG ilipokutana na Real Madrid kwenye hatua ya 16 bora.

Kuumia kwa Neymar kulizua hofu kama angekuwa na uwezekano wa kuwepo kwenye kikosi cha Brazil kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa mwaka huu Russia.

Tayari mchezaji huyo ameshaanza mazoezi baada ya vipimo vya afya kusoma kuwa yupo fiti kwa ajili ya michuano hiyo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa(kushoto), akifurahia jambo na Wazitri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, (wapili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Evod Mmanda, (watatu kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua, (wane kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TANESCO), Dkt. Alexander Kyaruzi, na Mkuriugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, wakati alipowasili kuzindua mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kufua umeme wa Gesi asilia (Mtwara Gas Plant), mkoani Mtwara Alasiri ya Mei 21, 2018. Kituo hizo sasa kitazalisha Megawati 22 kutoka za sasa Megawati 18.


 Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, akitoka eneo la mitambo mipya miwili ya kuzalisha umeme wa Megawati 4 kila mmoja baada ya kuizindua, kwenye Kituo cha Kufua umeme wa Gesi Mkoani Mtwara Mei 21, 2018.
Wabunge wa Mikoa ya Kusini, wakiwa na mwenyekiti wao, Mhe. Selemani Bungara(wapili kushoto)
 
NA MWANDISHI WETU, MTWARA-MEI 22, 2018

WABUNGE wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara, wameimwagia sifa Serikali hususan Wizara ya Nishati na Shirika la Umeme TANESCO kufuatia kumaliza adha ya umeme iliyodumu kwa takriban miaka 10 kwenye mikoa hiyo.

Pongezi hizo wamezitoa mbele ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, baada ya kuzindua Kituo cha Kuzalisha umeme wa gesi asilia (Mtwara Gas Plant), mkoani Mtwara Alasiri ya Mei 21, 2018.

Wa kwanza kutoa pongezi hizo alikuwa Mbunge wa Mtwara Mjini kupitia chama cha Wananchi CUF, Mhe Maftah Nachuma ambaye yeye alienda mbali zaidi na kufikia kusema atamuandalia Mhe. Waziri Mkuu mkutano mkubwa wa hadhara ili kuwaeleza wananchi wa jimbo lake, mafanikio yaliyoletwa na serikali.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu, leo ninayofuraha kubwa sana, kwani kilio cha muda mrefu cha wana Mtwara, cha kukosa umeme wa uhakika, hatimaye kimepatiwa ufumbuzi na kwetu sisi hii ni sherehe kubwa, ningetamani mkutano huu ungewaalika na viongozi wengine wa vyama vya siasa, na mimi binafsi nitakuandalia mkutano mkubwa wa hadhara ili uje uwaeleze wananchi maendeleo haya yaliyoletwa na serikali.” Alisema Mhe. Nachuma.

Naye Mwenyekiti wa wabunge kutoka Mkoa wa Lindi, ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kilwa Kusini, Mhe. Selemani Bungara, alisema maendeleo haya ambayo serikali inawafikishia wananchi ni kwa sababu bunge linaisimamia vema serikali.

“Siku zote tunasema Kusini kwanza mambo mengine baadaye, na mimi niwaambie, tutaendelea kupiga kelele hadi kero zote zitatuliwe, na niishukuru serikali kwa kumaliza hii kero ya umeme iliyudumu kwa muda mrefu.” Alisema Mhe. Bungara

Naye Mbunge wa Mtwara Vijijini, Mhe. Hawa Ghasia, yeye pia aliipongeza serikali kwa kumaliza kero ya umeme Mkoani Mtwara, kwani sasa Mkoa wa Mtwara umekamilika kwa kila eneo katika Nyanja ya uwekezaji.

“Mikoa yetu ya Kusini tuna kila kitu, Gesi iko hapa, Bandari tunayo, Ardhi ambayo wala haihitaji fidia nayo ipo, na sasa tunao umeme wa uhakika unaopatikana masaa 24, hii ni fursa nzuri kwetu sisi tunaotoka mikoa ya Kusini.” Alisema Mhe. Hawa Ghasia.

Akitoa taarifa fupi ya kituo hicho mbele ya Waziri Mkuu, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka alisema. Kituo cha kufua umeme kwa Gesi Asilia cha Mtwara kilianza rasmi kufanya kazi mwaka 2007, kwa sasa kituo hiki kinazaidi ya miaka kumi(10) na kina uwezo wa kuzalisha Megawati 18 za umeme na ndio chanzo pekee cha Nishati ya umeme kwa eneo lote la Mikoa ya Lindi na Mtwara, isipokuwa kwa baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Kilwa na Liwale ambayo yanapata umeme kutoka kwenye vituo vyao vidogo.

Mahitaji ya juu ya Nishati ya Umeme kwa eneo lote la Mikoa ya Lindi na Mtwara ni takribani Megawati 16.5” Alisema Dkt. Mwinuka.

Alisema, Katika kukabiliana na changamoto ya kukua kwa mahitaji ya umeme katika mikoa ya Lindi na Mtwara, serikali kupitia TANESCO ilifanya maamuzi ya upanuzi wa kituo hiki cha kuzalisha umeme ili kukiongezea uwezo wake. Hatua hii inahusisha usimikaji wa Mitambo miwili ya kufua umeme kila mmoja ukiwa na uwezo wa kuzalisha Megawati 2, na hivyo kufanya ongezeko la jumla la Megawati nne (4)

Hatua hii itaongeza uwezo wa kituo kuwa ni Megawati ishirini na mbili (22) ambao utatosheleza mahitaji ya sasa ya eneo hili na kuwa na ziada.

Akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani alisema, Hatua hii ni ya awali katika mpango endelevu unaolenga katika kuimarisha upatikanaji wa nishati ya umeme  katika mikoa ya Lindi na Mtwara ambapo kiasi cha Megawati nyingine nne (4) zitafuatia katika kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019, pia upo mpango mkubwa wa ujenzi wa mtambo wa Megawati 300 kwa msaada wa Shirika la Maendeleo la Watu wa Japani JICA, unaotarajiwa kukamilia ifikapo mwaka 2020.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, aliwapa changamoto wakazi wa Mkoa wa Mtwara kutumia umeme huo kikamilifu katika kujiletea maendeleo kwani sasa umeme ni bora na wa uhakika.

“Nitoe wito kwa vijana, sasa mnaweza kufanya shughuli za kunyoa(saloon), kuchomelea vyuma, kuranda mbao, kuuza juice, na hata wengine kuchaji simu na kuweka miziki kwenye simu kwa kutumia computer, mnayo fursa kubwa ya kufanya shughuli zenu ndogo ndogo za kiuchumi kupitia umeme huu ambao sasa unawaka masaa 24.” Alisema.

Waziri Mkuu aliipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara, kwa kuchangamkia haraka uwepo wa umeme wa kutosha kwa kuanza kuweka taa za barabarani na hivyo kuufanya mji wa Mtwara kung’aa majira ya usiku.

 Mbunge wa jimbo la Kilwa Kusini, Mhe. Selemani Bungara, akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa upanuzi wa Kituo cha Kufua umeme wa Gesi mkoani Mtwara Mei 21, 2018.
 Mbunge wa Mtwara Mjini Mhe.Maftah Nachuma, akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa upanuzi wa Kituo cha Kufua umeme wa Gesi mkoani Mtwara Mei 21, 2018.
 Mbunge wa Mtwara Vijijini, Mhe. Hawa Ghasia
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akihutubia
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akitoa hotuba yake.
 Waziri Mkuu akipitia hotuba yake kabla ya kuhutubia.
 Meneja wa Kituo cha Kufua Umeme wa Gesi Mkoani Mtwara, Mhandisi Mpulungwa Chilumba, (kushoto), akitoa maelezo ya kiutendaji ya Kituo hicho mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, (katikati), Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, (kulia) na viongozi wengine wa Mkoa wa Mtwara
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa Gesi cha Mtwara (Mtwara Gas Plant) Alasiri ya Mei 221, 2018. Kushoto ni Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani. . Kituo hizo sasa kitazalisha Megawati 22 kutoka za sasa Megawati 18.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akibonyeza kitufe ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi wa upanuzi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa Gesi cha Mtwara (Mtwara Gas Plant) Alasiri ya Mei 221, 2018. Kushoto ni Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani. . Kituo hizo sasa kitazalisha Megawati 22 kutoka za sasa Megawati 18.

 Waziri Mkuu, akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Dkt. Alexander Kyaruzi na viongozi wa juu wa Wizara ya Nishati na Shirika hilo, wakati alipowasili kwenye Kituo cha Kufua umeme wa Gesi cha Mtwara Mei 21, 2018.
 Wananchi wakishangilia
 Mama akiwa ma mwanaye huku akifurahi 
 Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, (wapili kushoto), akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Dkt. Alexander Kyaruzi, (kushoto), Naibu Mkurugenzi wa Shirika hilo anayeshughulikia uzalishaji umeme, Mhandisi Abdallah Ikwasa, (kulia) na Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme wa Gesi Mtwara, Mhandisi Mpulungwa Chilumba.
 Dkt. Kalemani akimnong'oneza kitu Meneja wa Kanda ya Kusini wa TANESCO, Mhandisi Aziz Salum.
 Wafanyakazi wa TANESCO Mtwara
 Waziri Mkuu Majaliwa na viongozi wengine wakifurahia burudani ya kwaya
 Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, wakiwa wenye furaha wakati vikundi vya burudani vikitoa burudani
 Picha ya pamoja

DAWA ZAVUSHWA KUPITIA MTO WENYE MAMBA MKOANI RUVUMA


 Wakazi wa vijiji vilivyopo kandokando ya mto Ruvuma wilayani Nyasa mkoani Ruvuma na wafanyakazi wa Bobari ya Dawa (MSD), wakisaidia kushusha maboksi yenye dawa na kuyaingiza kwenye mtumbwi baada ya kupelekewa na MSD Kanda ya Iringa leo na baadae kuyapeleka katika Zahanati ya Kijiji cha Mitomoni.
 Maboksi ya dawa yakiingizwa kwenye mtumbwi.
 Wakazi wa Kijiji cha Mitomoni wakisubiri mtumbwi ili kuwavusha upande wa pili wa mto Ruvuma.
 Dawa zikipelekwa Zahanati ya Mitomoni
 Maboksi ya dawa kutoka MSD yakishushwa
 Wananchi wakishusha maboksi hayo kutoka katika mtumbwi.
 Mkazi wa Kijiji cha Mitomoni Khadija Salum, akizungumzia upatikanaji wa dawa kutoka MSD.
 Mkazi wa kijiji hicho, Mbwana Koloma, akizungumzia changamoto ya miundombinu ya barabara na jinsi wanavyopokea dawa kutoka MSD.
 Mwenyekiti wa kamati ya Afya wa Kijiji cha Mitomoni Omar Hassan akizungumza wakati wa kupokea dawa hizo.
Mmoja wa viongozi wa Kijiji cha Nakawale, Ima Komba akisaini fomu maalumu ya kupokelea dawa kutoka MSD.

WANANCHI wanaoishi katika Vijiji vya Mkenda na Mitomoni vilivyopo kandokando ya mto Ruvuma wilayani Nyasa mkoani Ruvuma wamesema changamoto kubwa waliyonayo ni 
mazingira magumu ya miundo mbinu ambayo inasababisha ugumu wa ufikishaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kutoka  Bohari ya Dawa (MSD).

Wakazi hao wamesema kuwa, mazingira ya kufikisha dawa kwenye vijiji hivyo hutegemea zaidi usafiri wa kuvuka mto Ruvuma ambapo hulazimika kutumia boti,ambapo hata hivyo maisha yao yanakuwa na mashaka ndani ya mtumbwi hiyo ambayo iko wazi kutokana na mto huo kuwa na mamba wengi.

"Changamoto yetu kubwa ni usafishaji wa dawa kuja hapa kijijini kutokana na kutegemea zaidi mto huu ambao una mamba wengi, hata mwaka huu mwanzoni mtumbwi huu mnaouona ulipinduka na watu  wakiwapo wauza mitumba waliuawa na mamba; lakini tunashukuru  Bohari ya Dawa (MSD) kwani wao wanaweza kutuletea dawa  kwa wakati" alisema Mwenyekiti wa kamati ya Afya wa kijiji cha Mitomoni Omar Hassan.

Alisema ili kuondoa changamoto hiyo, wanaiomba serikali kuhakikisha inaboresha miundombinu ya barabara, ili dawa hizo zisafirishwe kwa njia ya barabara badala ya kutegemea mto huo. 

Alisema yeye na kamati yake wamekuwa wakipokea dawa mara nne kwa mwaka kutoka MSD na kuzihakiki kwa ajili ya matumizi.

"Pamoja na changamoto ya miundombinu lakini tumekuwa tukihakikisha dawa zinazoletwa na MSD zinafika kituoni na kutumika ipasavyo,"alisema.

Alisema kutoka Songea mjini hadi Kijiji cha Mitomoni, Songea vijijini, katika kituo hicho cha afya ni km 135 na MSD imekuwa ikihakikisha dawa hizo zinafika.

Alisema changamoto zinakuwa kubwa zaidi kipindi cha mvua kwa kuwa miundombinu ya barabara hadi kufika kivukoni ni tatizo na kuna wakati dawa zinafika usiku na zinatakiwa kuvushwa usiku huo huo.

Hassan alisema changamoto hiyo ya mamba katika mto huo anaijua vizuri kwani mtoto wake Sanifu Omar (27), alipoteza maisha kwa kuliwa na mamba wakati alipokuwa akisafirisha abiria kwa kutumia mtumbwi.

Mkazi wa Kijiji cha Mitomoni Khadija Salum alisema wamekuwa wakipata dawa zote muhimu katika kituoni hicho ikiwemo za mama mjamzito na mtoto bila ya ubaguzi na kwa wakati.

"Mimi nina watoto watano kuanzia ujauzito wa kwanza sijawahi kukosa dawa hapa pamoja na ugumu wa miundombinu lakini dawa zinafika hivyo serikali ione haja ya kuboresha barabara zetu," alisema.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mitomoni, Ivo Hekela, alisema kijiji hicho kinahudumia agonjwa 12,000 kutoka vijiji vitano ambavyo ni Mitomoni, Mipotopoto,Konganywita,Mkenda,Uhuru na Mozambique. 

Meneja wa MSD Kanda ya Iringa, John Sipendi, alisema wamekuwa katika changamoto ya kufikia vituo hivyo vya pembezoni ikiwa ni pamoja na kutumia muda mrefu kufikisha dawa na wakati wa mvua kukwama kwa magari njiani na gharama za usafirishaji kuogezeka.

Madereva wa MSD Kanda ya Iringa wamesema wamekuwa wakishindwa kushusha dawa wakati wa mvua za masika kutokana na mto huo kujaa maji hivyo hulazimika kulala kijijini hapo kwa siku mbili hadi tatu.

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube