BREAKING

Wednesday 23 May 2018

NEYMAR AFANYIWA VIPIMO VYA AFYA, AUNGANA NA WENZAKE KWENYE MAZOEZI TAYARI KWA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA


Mshambuliaji nyota wa timu ya Taifa ya Brazil na PSG ya Ufaransa, Neymar Junior, amefanyiwa vipimo vya afya na tayari ameshaungana na wenzake mazoezini kujiandaa na michuano ya Kombe la Dunia huko Urusi.

Neymar alikuwa hayupo fiti tangu aumie katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya wakati PSG ilipokutana na Real Madrid kwenye hatua ya 16 bora.

Kuumia kwa Neymar kulizua hofu kama angekuwa na uwezekano wa kuwepo kwenye kikosi cha Brazil kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Dunia kwa mwaka huu Russia.

Tayari mchezaji huyo ameshaanza mazoezi baada ya vipimo vya afya kusoma kuwa yupo fiti kwa ajili ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube