BREAKING

Thursday 12 October 2017

DONALD NDOMBO NGOMA AIKOSA KAGERA SUGAR, ATANGULIA SHINYANGA......


Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma ataifuata timu yake mjini Shinyanga.

Yanga inaondoka leo kwenda mjini Bukoba ikipitia Mwanza kwenda kuivaa Kagera Sugar.

Ngoma na Thabani Kamusoko wanaachwa Dar es Salaam ili kuendelea na matibabu kutokana na kuwa majeruhi.

Lakini Ngoma, atakwenda Shinyanga kwa kuwa atakuwa amerejea katika hali yake.

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten amesema baada ya mechi ya Jagera, watakwenda Shinyanga kuivaa Stand United ambako Ngoma ataungana nao.

"Wakati tukiwa Shinyanga tutaungana na Ngoma. Daktari amesema atakuwa amerejea katika hali nzuri," alisema.

Yanga inapaa na "pipa" kwenda mjini Mwanza baadaye Bukoba kwa ajili ya mechi dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, wikiendi hii. 

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube