BREAKING

Wednesday 1 November 2017

KUELEKEA MCHEZO WA LIGI KUU TANZANIA BARA MABINGWA WA SOKA TANZANIA BARA YANGA WAENDELEA KUJINOA UWANJA WA UHURU KABLA YA KUWAVAA SINGIDA UNITED NAMFUA , ULINZI WAIMARISHWA ZAIDI.


Wachezaji wa Yanga wakijifua katika Uwanja wa Uhuru

 wachezaji wa Yanga wakimsikiliza Kocha wao GeorgeLwandamina wakati wa mazoezi





Mabingwa wa Kandanda Tanzania Bara  Yanga wameendelea na mazoezi katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam ikiwa ni matayarisho ya mchezo wao dhidi ya Singida United utakaopigwa katika dimba la Namfua mjini Singida.  

Channel ten imeshuhudia wachezaji wa kikosi hicho wakijifua vilivyo chini ya kocha wao George Lwandamina huku baadhi ya wafanyakazi wa timu hiyo wakizuia waandishi wa habari kupiga picha mazoezi hayo.

Pamoja na changamoto hiyo Kamera ya Channel ten ilinasa baadhi ya matukio pamoja na mazoezi ambayo yaliuwa yakiendelea katika viwanja hivyo vya Uhuru Dar es Salaam.

Yanga wanaijiwinda na mchezo huo mgumu wa ugenini, dhidi ya timu ya Singida United ambayo imeleta mapinduzi makubwa tangu kupanda kwa daraja na kucheza Ligi Kuu.

Yanga itamenyana na singida ikitaka kupata pointi tatu ili kujitupa kileleni mwa Ligi kuu ambapo Simba ndio wanaongoza kwa sasa wakiwazidi wapinzani wao yanga kwa mabao ya kufunga, kwani kila timu ina pointi 16.

Mchezo huo pia utachangizwa kwa ushindani wa Singida United yenye alama 13 kutaka kuwakamata vinara wa Ligi simba kwa kushinda ili kufikisha pinti 16 na kuungana na vigogo wengine ambao ni Azam FC wenye pointi kama za Simba, Yanga pamoja na Azam FC




No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube