BREAKING

Tuesday 1 March 2016

SERIKALI YAWAPA MOTISHA WACHEZAJI WA TWIGA STARS


old map
Tanzania Tourist Board (TTB) has been following up the ongoing discussions on social media following a video clip being posted on YouTube (https://www.youtube.com/watch?v=iveX49WE7fw) which has been circulating through various media channels showing a person claiming that Oldupai Gorge, a site in Tanzania that holds evidence of the earliest existence of mankind is in Kenya.
This video clip has triggered a lot of discussions on the different social media among Tanzanians and other people who have good wishes for Tanzania tourism who know very well that Oldupai Gorge is in Tanzania and NOT in Kenya.
As a public institution, responsible for marketing and promotion of Tanzania tourist attractions, Tanzania Tourist Board is also dismayed by this misleading information which intends to distort the good work the Board has been doing in promoting Tanzania tourist attractions including the Oldupai Gorge.
The Board would like to take this opportunity to strongly refute this statement delivered by the said person from a neighboring country while addressing one of the sessions of the International Young Leaders Assembly (IYLA) in USA, August 2015.
We would like to inform the world that as it is the case for Mt. Kilimanjaro, Serengeti National Park, Zanzibar to mention just a few, Olduvai Gorge which is referred to as the Cradle of Mankind, where Dr. Louis and Mary Leakey discovered important hominid remains of the nutcracker ‘Australopithecus bosel’, who lived nearly two million years ago, is also in Tanzania and not elsewhere in the world. It is located in the eastern Serengeti Plains in the Arusha Region and about 45 km, from Laetoli, another important archaeological site of early human occupation. The paleoanthropologist-archeologist team Mary and Louis Leakey established and developed the excavation and research programs at Olduvai Gorge which achieved great advances of human knowledge and world-renown status. Olduvai Gorge is one of the key tourist attractions for Tanzania.
We call upon Tanzanians and those with good wishes for Tanzania wherever they are to continue supporting the effort’s undertaken by TTB in marketing Tanzania and her all tourism attractions. We believe that it is the role of every single Tanzanian to promote Tanzania as Africa’s best destination and ask them to join and support Tanzania Tourist Board in its efforts to promote destination Tanzania.
We would like to applaud the reaction made by Tanzanians and non-Tanzanian within and out of Tanzania, who through this incident were able to stand up as ‘one voice’ and tell the world that OLDUPAI GORGE is INDEED IN TANZANIA!
Issued by:
Public Relations Office
TANZANIA TOURIST BOARD
March 01, 2016

WATANZANIA WAHIMIZWA KUCHANGIA DAMU KWA HIYARI KUOKOA MAISHA

 Makamu
wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akifanyiwa vipimo na
mfanyakazi wa Maabara ya Muhimbili, Bi. Kibuna Mohammed (kulia) wakati wa zoezi
la kuchangia damu lilioratibiwa na Hospitali hiyo Kitengo cha Dharura. Zoezi
hilo la kuhamasisha wananchi kuchangia damu kwa hiyari lilifanyika eneo la
Karume jijini Dar es Salaam kwa siku mbili (Alhamisi na Ijumaa) mwishoni mwa
wiki.
 Makamu
wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akifanyiwa vipimo na
mfanyakazi wa Maabara ya Muhimbili, Bi. Kibuna Mohammed (kulia) wakati wa zoezi
la kuchangia damu lilioratibiwa na Hospitali hiyo Kitengo cha Dharura. Zoezi
hilo la kuhamasisha wananchi kuchangia damu kwa hiyari lilifanyika eneo la
Karume jijini Dar es Salaam kwa siku mbili (Alhamisi na Ijumaa) mwishoni mwa
wiki.
 Mfanyakazi
wa Maabara ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Bi. Kibuna Mohammed (kushoto)
akimfanyia vipimo mmoja ya wakazi wa Dar es Salaam waliojitokeza kwa hiyari
wakati wa zoezi la kuchangia damu lililoendeshwa na Kitengo cha Dharura
hospitalini hapo katika eneo la Karume, Ilala mwishoni mwa wiki.
 Makamu
wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto) akizungumza na Afisa
Uhisiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Bi. Neema Mwangomo baada ya
kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya zoezi la kuchangia damu kwa
hiari lililoendeshwa na Kitengo cha Dharura hospitalini hapo katika eneo la
Karume, Ilala mwishoni mwa wiki.
  Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi.
Zuhura Hanif (kushoto) akizungumza na Afisa Uhisiano wa Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili, Bi. Neema Mwangomo baada ya kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali kwa
ajili ya zoezi la kuchangia damu kwa hiari lililoendeshwa na Kitengo cha
Dharura hospitalini hapo katika eneo la Karume, Ilala mwishoni mwa wiki.
 Baadhi
ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani wakifanyiwa vipimo
katika zoezi la kuchangia damu lililoendeshwa na Kitengo cha Dharura cha
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili katika eneo la Karume, Ilala mwishoni mwa wiki.
Mmoja wa mkazi wa Dar es Salaam akipimwa presha kabla ya kushiriki zoezi la kujitolea damu kwa hiari wakati wa zoezi la kuchangia damu lililoendeshwa na Kitengo cha Dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili katika eneo la Karume, Ilala mwishoni mwa wiki. 
Mmoja wa mkazi wa Dar es Salaam akishiriki zoezi la kujitolea damu kwa hiari wakati wa zoezi la kuchangia damu lililoendeshwa na Kitengo cha Dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili katika eneo la Karume, Ilala mwishoni mwa wiki.
…………………………………………………………………………………………………….
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupitia kitengo cha dharura wametoa rai kwa watanzania kujitolea kwa hiyari kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaopokelewa hospitalini hapo.
Akizungumza wakati wa zoezi la uchangiaji damu lililofanyika kwa siku mbili mwishoni mwa wiki katika eneo la Karume jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru amebainisha kuwa zoezi hilo ni muhimu sana kwani litasaidia kuokoa maisha ya
wagonjwa wenye uhitaji huo wanaopokelewa hospitalini hapo kama vile
waliopata ajali, wakina mama wajawazito na watoto.
“Hospitali ya Taifa Muhimbili inahitaji wastani wa chupa za damu 100 lakini tunafanikiwa kupata wastani wa chupa 40 hivyo kuwepo na upungufu wa chupa 60 kila siku. Hali hii inapelekea kuhudumia
wagonjwa wenye uhitaji wa dharura tu huku wengine wakisubiri.” Alisema Profesa Maseru
“Wataalamu wananiambia kuwa kwa kawaida, damu inaweza kuhifadhiwa kwa muda wa takribani mwezi mzima kabla ya muda wake wa kutumika kwisha, na kutokana na uhifadhi wa damu kwa muda mfupi ndiyo maana tunasisitiza umuhimu wa watu kuchangia mara kwa mara.  Kitaalamu mwanamume anaweza kuchangia mara nne kwa mwaka na mwanamke mara tatu kwa mwaka.” Aliongezea Profesa Maseru
“Katika wakati wa kutoa huduma ya tiba ya dharura, haswa kwa wagonjwa wa ajali, watoto na wamama wajawazito, upatikanaji wa huduma ya  Ambulance na damu kwa wakati huongeza nafasi ya
kuishi kwa wahitaji kwa kiasi kikubwa mno na huduma hizi huokoa maisha ya mamilioni ya wagonjwa kila mwaka duniani kote,” alisema na kumalizia, 
“Natoa rai kwa wakazi wa Dar es slaaam na Watanzania wote kwa ujumla kujenga utamaduni wa kuchangia damu kwa hiari mara kwa mara ili nchi iwe na akiba ya damu ya kutosha, kwani asilimia moja ya Watanzania wakiamua kuwa wachangiaji damu wa kujirudia Mpango wa Taifa wa Damu Salama utaweza kukidhi mahitaji ya damu nchini.”
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif, kampuni inayojishughulisha na uuzaji na usambazaji wa ving’amuzi kwa ajili ya matangazo ya dijitali ambao walidhamini zoezi hilo amesema kuwa hii ni mara ya pili wao kudhamini zoezi hilo kutokana
na umuhimu wake katika kuokoa maisha ya watanzania wote kwa ujumla.
“Hakuna asiyefahamu katika maisha yetu yanayotuzunguka ajali zimekuwa nyingi zinazopelekea watu kupoteza maisha maelefu kubaki mejeruhi wenye uhitaji mkubwa wa damu ili kupata matibabu. Kama
tunafuatilia vyombo vya habari basi tutakuwa tunasikia ni mara ngapi kwa wiki ajali zinatokea barabarani na kuacha majeruhi wengi. Kwa upande wa akina mama wajawazito wanahitaji damu kwa kiasi kikubwa hasa baada ya kujifungua. 
Hatuwezi kukaa pembeni na kuwatizama wakikosa msaada wakati uwezo huo tunao.” Aliongezea Bi. Hanif “Tumejisikia faraja sana kuwa wamojawapo wa wadau walioshiriki kufanikisha zeozi hili na tunaahidi kuendelea kushirikiana na Muhimbili katika kuwahamasisha watanzania wajitokeze zaidi. 
Kwa mujibu wa wataalamu tunaweza kujitolea damu mpaka mara nne ndani ya mwaka, nina
uhakika kila mtanzania akifanya hivyo basi benki yetu ya damu itajaa na tutaweza hata kusaidia wengine wan chi za jirani wenye uhitaji.” Alimalizia Makamu wa Rais kutoka kampuni ya StarTimes Tanzania.

Shida ya maji jiji la Dar es salaam kuwa historia

 Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi Dawasa Mhandisi Romamus Mwang’ingo (Kushoto)  akitoa maelekezo kwa Mkuu wa msafara wa kamati ya Ushauri ya mkoa wa Dar es Salaam Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi (Kulia) juu ya ufanyaji kazi wa mitambo ya Ruvu chini.
 Mafundi wakiwa katika harakati za kulaza bomba litakalotumika kuleta maji kwenye tanki kubwa lililopo kibamba toka Ruvu chini na juu kwa ajili ya uhifadhi na usambazaji maji katika Jiji la Dar es salaam. 
Mafundi wakikarabati bomba kuu la kusambaza maji toka Ruvu juu katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Dar es Salaam na maeneo jirani.
 Mkuu wa msafara wa kamati ya Ushauri ya mkoa wa Dar es Salaam Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi (Katikati) akisikiliza maelezo juu ya ufanyaji wa kazi wa mitambo inayotumika kusambaza maji toka Ruvu juu kutoka kwa Meneja Mradi toka kampuni ya WABAG Mr. Pintu Dutta wakati wa kamati ya Ushauri ya mkoa wa Dar es Salaam ilipotembelea mitambo hiyo. 
 Mkuu wa msafara wa kamati ya Ushauri ya mkoa wa Dar es Salaam Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi (Kushoto) akisikiliza maelezo juu ya ramani inayoonesha usambazaji wa maji toka Ruvu Juu kwenda katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi Dawasa Romamus Mwang’ingo.
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
March 1 2016
Tatizo la ukosefu wa huduma ya maji katika baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam linatarajiwa kuwa historia mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa tanki kubwa lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita million 10 kwa siku lililopo Kibamba.
Hayo yamebainika mara baada ya wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Dar es Salaam walipotembela mradi huo unaofadhiliwa na nchi ya India ambapo mbali na kujionea ujenzi wa tanki hilo pia walitembelea na kujionea ulazaji wa bomba litakayokuwa linasafirisha maji toka vyanzo vya maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu na kwenda kuifadhiwa katika tanki hilo tayari kwa kusambazwa katika maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake.
Hata hivyo Disemba 31, 2015 Serikali ya Tanzania na India zilisaini mkataba wa ufadhili wa Dola Millioni 59.3 ili kutekeleza mradi wa ulazji wa bomba la maji kutoka Mlandizi mpaka Kimara na kuishia Kinyerezi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa tanki hilo la Kibamba.
Mradi huo unatarajiwa kukamilika Marchi 31 mwaka huu ambapo mpaka sasa umekamilika kwa asilimia 90 ili uanze kusambaza maji katika Mkoa wa Dar es Salaam na viunga vyake.
Mkuu wa msafara wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Dar es Salaam alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Said Meck Sadiq ambaye ndio mwenyekiti wa kamati hiyo amesema lengo la kamati hiyo ni kuona Jiji zima linakuwa na huduma ya maji safi na salama kwa matumizi mbalimbali na kuondokana na suala la maji ya mgao linalolikumba Jiji la Dar es salaam kwa miaka mingi.
“ Tatizo la maji litakuwa historia katika Jiji letu maana mradi huu ni mkubwa sana na utawezesha watu wengi kupata huduma ya maji safi na salama na tutaondokana na uhaba wa maji katika baadhi ya maeneo na yale ambayo yalikuwa hayana kabisa huduma ya maji kwa kipindi kirefu sana yatapatiwa huduma hiyo”
“ Nawaomba wananchi na wafanyakazi wa Dawasco kutunza miundombinu hii kwani ni hazina kubwa si kwetu tu hata kwa vizazi vijavyo, na ni marufuku kwa watu kujenga nyumba katika eneo lilipopita bombala maji, alama maalum ziwekwe ili kuonesha kuwa sehemu hii bomba limepita ili kuzuia uharibifu wa miundombinu” Alisema Mushi.
Mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa tanki la Kibamba litakuwa na uwezo wa kusambaza maji katika maeneo yafuatayo; Ruvu, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Kimara, ubungo, Segerea, hadi kinyerezi ambapo bomba linatakuwa limeishia hapo na maeneo yote ambayo yanapata maji kupitia mtambo wa Ruvu Juu na Chini na wale amabao bado hawajaunganishwa na huduma ya maji wataunganishwa ili waweze kupata huduma hiyo kwa urahisi zaidi.
Aidha, mmoja kati ya wajumbe wa kamati ya ushauri ya mkoa wa Dar es Salaam mbunge wa viti maalum Ilala (CHADEMA) Mhe. Anatropia Theonest amesema huduma ya maji ni suala muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yoyote, hivyo basi Serikali iliwekee uzito na kulitekeleza kwa nguvu zake zote na kuonya wale wanaohujumu miundombimu ya maji kuchukuliwa hatua za kisheria, iwe ni kwa wafanyakazi wa idara za maji au wananchi ili kuhakikisha huduma hiyo inawanufaisha wananchi.
Kamati ya ushauri ya mkoa wa Dar es Salaam inaundwa na wakuu wa Wilaya zote za mkoa wa Dar es salaam, Mameya wote, wabunge wa Mkoa wa kuchaguliwa, kuteuliwa au viti maalum na kamati hiyo inakuwa chini ya Uwenyekiti wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO AKABIDHI MICHANGO YA TWIGA STARS

wm1
Naibu Waziri wa  Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimkabidhi  Mhasibu wa wizara hiyo Godfrey Osmund shilingi milioni tatu zilizotolewa na mdau wa michezo ambaye hakutaka  jina lake litajwe kwaajili ya kuisaidia timu ya wanawake ya mpira wa miguu ya Twiga Stars. Fedha hizo zimewekwa  katika Benki ya NMB Bank House akaunti  namba “20110001677 inayojulikana kwa jina la Twiga Stars Special Fund”.
wm2
Naibu Waziri wa  Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimsikiliza Mhasibu wa wizara hiyo Godfrey Osmund mara baada ya kumkabidhi shilingi milioni tatu zilizotolewa na mdau wa michezo ambaye hakutaka  jina lake litajwe kwaajili ya kuisaidia timu ya wanawake ya mpira wa miguu ya Twiga Stars. Ijumaa ya wiki hii timu hiyo itacheza na   Zimbabwe  mashindano ya awali ya kufuzu kombe la Afrika kwa wanawake.
wm3
Naibu Waziri wa  Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akimweleza jambo   Mhasibu wa wizara hiyo Godfrey Osmund mara baada ya kumkabidhi shilingi milioni tatu zilizotolewa na mdau wa michezo ambaye hakutaka  jina lake litajwe kwaajili ya kuisaidia timu ya wanawake ya mpira wa miguu ya Twiga Stars. Mhasibu Osmund alizipeleka fedha hizo  katika Benki ya NMB Bank House akaunti namba “20110001677 inayojulikana kwa jina la Twiga Stars Special Fund”.
Picha na Anna Nkinda

Serikali yalitaka Dira ya Mtanzania kukanusha tuhuma dhidi ya Balozi Ombeni Sefue

mwb1
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw.Assah Mwambene (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  leo jijini Dar es Salaam kuhusu taarifa za upotoshaji zilizotolewa na Gazeti la Dira ya Mtanzania la tarehe 29/02/2016 kuhusu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Uratibu wa Vyombo Habari, Bw.Jamal Zuberi na Mkurugenzi Msaidizi Habari Bw.Vicent Tiganya wote kutoka Idara ya Habari (MAELEZO).
mwb2
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Bw.Assah Mwambane (ambaye hayupo katika picha) iliyokuwa ikiutaka uongozi wa Gazeti ya Dira Mtanzania kukanusha habari waliyoitoa hivi karibuni iliyokuwa na kichwa cha habari “Uchafu wa Ombeni Sefue Ikulu”.
Na Anitha Jonas – MAELEZO
…………………………………………………………………………………………………………………
Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw.Assah Mwambene ameutaka uongozi wa Gazeti la Dira ya Mtanzania kukanusha haraka na kuiomba radhi Serikali na   Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue kutokana na taarifa waliyoitoa katika toleo namba 404  la tarehe 29/02/2016 lenye  kichwa cha habari “Uchafu wa Ombeni Sefue Ikulu.
Hayo  yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi huyo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu taarifa kuwa hazikuwa na ukweli wowote kwani Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue hakuhusika katika uteuzi wa Mkurugenzi wa MSD wala kuhusika na kampuni ya CRJE katika utoaji wa tenda ya kujenga Chuo Kikuu cha Dodoma Oktoba 2007  kwani katika kipindi  hicho alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani.
“Serikali inautaka uongozi wa Gazeti la Dira ya Mtanzania ukanunushe taarifa hiyo kwa uzito ule uliyotumika kuchapisha habari hiyo na kama wanapinga wakidai wana ushahidi basi waupeleke mara moja kwenye vyombo vinavyohusika  ikiwemo Sekretarieti ya Maadili na TAKUKURU”,alisema Bw.Mwambene.
Aidha,  Bw.Mwambene amesema gazeti hilo liliandika kuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue alipigia chapuo Kampuni ya “UGG”  iliyowahi kuonyesha nia ya kujenga reli ya Kati nchini. Taaarifa hii pia siyo ya kweli na hakuna kampuni  yenye jina la “UGG” ilishawahi kuonyesha nia ya kujenga reli hiyo.
Mkurugenzi aliendelea kusema kuwa gazeti hilo lilimtuhumu pia Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue kuhusika na kumsafisha Bwana Eliakim Maswi wakati alichokifanya Balozi Sefue ilikuwa ni kusoma matokeo ya uchunguzi ambao hakuufanya yeye. Waliomsafisha ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Kamati ya Uchunguzi iliyoongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu kwani ndio waliiyofanya uchunguzi huo.
Hata hivyo serikali imewashauri wamiliki wa vyombo vya habari,wachapishaji,wahariri, na waandishi wa habari wajikite kwenye weledi na ukweli pia wafanye  utafiti wa kina  na kuandika mambo waliyo na uhakika nayo

Wataalamu TPRI wapelekwa Kilombero kufanya uchunguzi

dk rutNa Jacquiline Mrisho
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro imewapeleka wataalamu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Viuwatilifu ya Kitropiki (TPRI) wilayani Kilombero kufanya uchunguzi wa zao la mpunga linalosadikiwa kuharibiwa na dawa zilizomwagwa na Kampuni ya Kilombero Plantation (KPL) inayomiliki mashamba yanayopakana na mashamba ya wananchi.
Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Idara ya Uchumi na Uzalishaji Mali Mkoa wa Morogoro Bw. Ernest Mkongo kuhusu uchunguzi unaoendelea kufanyika katika mashamba ya wananchi ili kutathmini athari zinazotokana na dawa hizo.
“Wataalamu kutoka TPRI wameshafanya uchunguzi wa awali na mpunga huo umeonekana kuwa na rangi ya njano isivyo kawaida, hivyo wamechukua sampuli za mpunga huo na kuzipeleka maabara kwa ajili ya uchunguzi zaidi ili kujua kama umeharibiwa na dawa za kuondoa magugu zilizomwagwa na Kampuni ya KPL” alisema Mkongo
Aidha, Bw. Mkongo ameongeza kuwa, Taasisi ya TPRI ina wataalamu wa uhakika kwa hiyo anaamini watatoa majibu ya ukweli juu ya tatizo hilo.
TPRI ilianzishwa miaka ya 1940 ambapo kwa Tanzania ilirasimishwa rasmi katika Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Sheria Na. 18 ya mwaka 1979 kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa dawa zinazoathiri afya ya binadamu, wanyama na mazao.

Serikali yawapa motisha wachezaji wa Twiga Stars

TWI1
Baadhi ya wachezaji wa Timu ya Taifa ya mpira wa miguu wanawake “Twiga Stars” wakimsikiliza Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (hayupo pichani) alipowatembelea kambini kwao leo jijini Dar es Salaam.Twiga Stars inatarajiwa kucheza mechi na Timu ya Taifa wanawake ya Zimbabwe mchezo utakaochezwa tarehe 4 katika uwanjja wa Taifa.
Picha na WHUSM
TWI2
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura akizungumza na wachezaji wa Timu ya Taifa ya mpira wa Miguu wanawake “Twiga Stars” alipowatembelea kambini kwa leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Nkenyenge na Mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa BMT Bi. Jeniffer Mmasi Shang’a (kulia).
TWI3
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Selestine Mwesiga akitoa shukura kwa Serikali kutokana na jitihada zake za kuitafutia wadhamini Timu ya Taifa ya Mpira wa miguu wanawake (Twiga Stars) wakati Naibu Waziri wa Habari, Utamduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura(wapili kutoka kushoto) alipo watembelea wachezaji wa Timu hiyo leo jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa BMT Bi. Jeniffer Mmasi Shang’a (kulia). Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Nkenyenge.
TWI4
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura akisalimiana na Kocha wa Timu ya Taifa ya mpira wa Miguu wanawake “Twiga Stars” (Nasra Juma) alipowatembelea kambini kwao leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bi. Jeniffer Mmasi Shang’a.
TWI5
Mjumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bi. Jeniffer Mmasi Shang’a. akisalimiana na Kocha wa Timu ya Taifa ya mpira wa Miguu wanawake “Twiga Stars”  Bibi. Nasra Juma  wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (hayupo pichani) kambini kwao leo jijini Dar es Salaam.
……………………………………………………………………………………………………………………………..
Na: Frank Shijja,WHUSM
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imetoa motisha kwa wachezaji wa Timu ya Taifa ya mpira wa miguu wanawake(Twiga Stars) ikishinda katika mchezo wake dhidi ya Zimbabwe unatarajiwa kuchezwa siku ya Ijumaa tarehe 4 machi katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.
Haya yamebainishwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Annastazia James Wambula alipotembelea kambi ya Timu hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wachezaji wa Twiga Stars, Wambura amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa michezo wamekusanya shilingi milioni 15 ambazo zitatumika kama motisha kwa wachezaji hao.
Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa iwapo timu hiyo itaibuka na ushindi katika mechi yake dhidi ya Zimbabwe kila mchezaji atapata gawio la sh. Laki tatu kama mptisha na kuongeza kuwa itafanyika hivyo hivyo katika mchezo wa marudiano utakaochezwa nchini Zimbabwe.
Aidha alitumia fursa hiyo kuwaomba wadau wa michezo kuzidi kujitokeza na kuisaidi timu hiyo ikiwa ni pamoja na kuhudhuria kwa wingi katika mechi ya tarehe 4 machi dhidi ya Zimbabwe itakayochezwa katika uwanja wa Taifa.
Aliongeza kuwa msaada zaidi unahitajika ili kuiwezesha timu hiyo kukidhi mahitaji yake muhimu,hivyo alitoa wito kwa wadau mbalimbali kutoa michango yao kupitia Twiga Specila Fund, Akaunti na: 20110001677 iliyoko NMB tawi la Bank House jijjini Dar es Salaam.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesiga ameipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuhakikisha Twiga Stars inapata huduma muhimu ikiwemo motisha kwa wachezaji na benchi la ufundi.
Mwesiga pia amewapongeza wadau wote waliojitolea kusaidi timu hiyo ambapo amesema kujitokeza kwa wadau hao kunaongeza morali ya wachezaji.
Msaada huo wa shilingi milioni 15 umetolewa na wadau watatu ambapo mmoja aliyechangia sh. Milioni 3 aliomba jina lake lihifadhiwe, wengine ni Kampuni ya ASAS sh. Milioni 2 na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) sh. Milioni 10.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKAMILISHA ZIARA YA SIKU MBILI MKOANI TANGA

m1
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliangalia vijana wa kikundi cha sanaa cha Tanga kwanza alipowasili Ofisi  ya CCM Mkoa wa Tanga kwa ajili ya kuzungumza na Wanachama wa Chama hicho leo March 01, 2016. Makamu wa Rais amekamilisha ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Tanga.                
m2
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokua akizungumza nao katika Ofisi ya CCM Mkoa Tanga. Makamu wa Rais amekamilisha ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Tanga leo March 01.2016.
m3
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na vijana wa kikundi cha wasanii cha Tanga kwanza alipokua akiondoka katika Ofisi ya Chama cha  Mapinduzi CCM Mkoa Tanga baada ya kuzungumza na Wanachama wa Chama hicho leo March 01, 2016.  (Picha na OMR)        
m4
 Chipukizi wa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa Tanga Mwanakombo Mwakuru akimvisha Skafu Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipowasili Ofisi  ya CCM Mkoa wa Tanga kwa ajili ya kuzungumza na Wanachama wa Chama hicho leo March 01, 2016. Makamu wa Rais  amekamilisha ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Tanga. Kulia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Mhe.Henri Shikifu.
m6
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoani Tanga katika Ofisi ya CCM Nkoa Tanga. Makamu wa Rais amekamilisha ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Tanga leo March 01,2016.
m5
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokua akizungumza nao katika Ofisi ya CCM Mkoa Tanga. Makamu wa Rais amekamilisha ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Tanga leo March 01.2016.

Rais Magufuli atuma salamu za Rambirambi kwa Rais Mstaafu Kikwete




halRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kufuatia kifo cha Kaka yake Mzee Selemani Mrisho Kikwete, kilichotokea leo asubuhi nchini India.

Mzee Selemani Mrisho Kikwete alikuwa nchini India kwa matibabu.

Katika salamu zake Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshituko taarifa za kifo cha Mzee Selemani Mrisho Kikwete na amesema anaungana na familia ya Rais Mstaafu Kikwete kuombeleza kifo cha mtu muhimu kwa familia hiyo.

“Napenda kukupa pole nyingi wewe Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, familia yenu yote, ndugu jamaa na marafiki kwa kuondokewa na mtu muhimu katika familia, natambua uchungu mkubwa mlionao lakini nawaomba muwe  uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu” Alisema Rais Magufuli.

Dkt. Magufuli amemuombea Marehemu Mzee Selemani Mrisho Kikwete apumzishwe mahali pema peponi, Amina.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji’un.

Gerson Msigwa

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube