BREAKING

Tuesday 29 March 2016

TAMASHA LA PASAKA LAHITIMISHWA MJINI KAHAMA MKOA WA SHINYANGA

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akimpokea Mkurugenzi wa Utawala Wizara ya Ujenzi na Mawasiliano Bi. Katolina Kipa Mgeni rasmi wa Tamasha la Pasaka ambaye alimwakilisha Waziri wa Ujenzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa katika tamasha hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Taifa mjini Kahama leo na kuhudhuriwa na Mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Vita Kawawa, Mbunge wa jimbo la Kahama Mh. Jumanne Kishimba na aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo Ndugu James Lembeli.
Waimbaji mbalimbali wametumbuiza katika tamasha hilo ambalo ndilo limehitimisha matamasha ya pasaka ya mwaka huu yaliyofanyika katika mikoa ya Geita , Mwanza na Shinyanga katika kanda ya ziwa, Waimbaji hao ni Upendo Nkone, Jennifer Mgendi, Boniface Mwaiteje, Martha Baraka, Goodluck Gozbert , Jesca BM, Christopher Mwahangila, Ephraim Sekereti na wengine wengi. (PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-KAHAMA)
4
Mkurugenzi wa Utawala Wizara ya Ujenzi na Mawasiliano Bi. Katolina Kipa Mgeni rasmi wa Tamasha la Pasaka ambaye alimwakilisha Waziri wa Ujenzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na Mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Vita Kawawa Kushoto ni Mbunge wa jimbo la Kahama Mh. Jumanne Kishimba.
5
Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama akisalimiana na Bw. James Lembeli wakati alipokuwa akipmokea kwenye uwanja wa Taifa mjini Kahama leo.
1
Mwimbaji Tumsifu Rufutu akiimba huku akiwa amevalia kama manabii wa zamani wakati alipotumbuiza katika tamasha la Pasaka mjini Kahama leo.
6
Mwimbaji Jesca BM akifanya vitu vyake jukwaani.
8
Mshabiki wa muziki wa injili wa mjini Kahama Grace Boyo na rafiki yake Sara Shija wakifuatilia burudani ya muziki wa injili iliyokuwa ikiporomoshwa na waimbaji katika tamasha hilo.
9
Mwimbaji Faustine Munishi akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Vita Kawawa na viongozi wengine mara baada ya kuimba nyimbo zake mbili katika tamsha hilo.
10
Msabiki wa muziki wa injili wa mjini Kahama Grace Boyo na rafiki yake Sara Shija wakifuatilia burudani ya muziki wa injili iliyokuwa ikiporomoshwa na waimbaji katika tamasha hilo.
11
Mashabiki mbalimbali wa muziki wa injili wakipiga picha za Selfie katika tamasha hilo.
12 13
Mwimbaji Martha Baraka na wacheza shoo wake wakifanya vitu vyao jukwaani.
14
Tamasha hilo pia limehudhuriwa na watu mbali mbali kama unavyoona katika picha hii.
15
Mwimbaji Ephraim Sekereti akiimba nyimbo za kusifu na kuabudu katika tamasha hilo.
16
Mkurugenzi wa Msama Promotion akipiga picha ya pamoja na waimbaji wa kwaya ya Grorius ya Kahama mkoani Shinyanga.
17
Mwimbaji Boniface Mwaiteje akifanya vitu vyake jukwaani huku mashabiki wakicheza kwa furaha.
18
Mashabiki wakicheza kwa furaha katika tamasha hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Taifa mjini Kahama.
19 20
Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama akicheza na wanakwaya wa Kwaya ya Grorius ya Kahama.
21
Mwimbaji Jeniffer Mgendi akiimba jukwaani.
22
Mwimbaji Goodluck Gozbert akipagawisha jukwaa katika tamasha hilo.
23
Mkurugenzi wa Utawala Wizara ya Ujenzi na Mawasiliano Bi. Katolina Kipa Mgeni rasmi wa Tamasha la Pasaka ambaye alimwakilisha Waziri wa Ujenzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisoma hotuba kwa niaba ya waziri Profesa Mbarawa katika tamasha hilo kushoto ni Alex Msama wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Vita Kawawa na Mbunge wa jimbo la Kahama Mh. Jumanne Kishimba.
24
Mwimbaji Upendo Nkone akiwaimbisha mashabiki wake wakati alipokuwa akitumbuiza jukwaani kwenye uwanja wa Taifa mjini Kahama.
25
Mwimbaji Boniface Mwaiteje na Faustine Munishi kutoka nchini Kenya wakifanya mambo makubwa jukwaani kama wanavyoonekana.
26
Mwimbaji Faustine Munishi akionekana kufurahiswa na mashabiki wakati alipokuwa akiimba jukwaani kwa kushirikiana na mwimbaji Boniface Mwaiteje.

Sunday 27 March 2016

RAIS Dkt JOHN MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA PASAKA AWASIHI WATANZANIA KUWA NA UMOJA

Na Mwandishi Maalum

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi watanzania kuendelea kuwa wamoja na kushirikiana kuijenga nchi yao, badala ya kubaguana.

Rais Magufuli ametoa wito huo leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya Pasaka pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Amesema Mwenyezi Mungu alimtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo kuja kuikomboa dunia bila kuwabagua wanadamu, vivyo hivyo nasi binadamu tunapaswa kutobaguana, iwe kwa dini zetu, makabila yetu, mitazamo ya kisiasa na hata rangi zetu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akilakiwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa alipowasili kwa Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Mkewe Mama Magufuli wakishiriki na waumini wengine Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam.
Kwaya wakati wa  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo.
.................................

Aidha, Rais Magufuli amewakumbusha watanzania kufanya kazi kama ambavyo vitabu vitakatifu vinasisitiza umuhimu wa kufanya kazi, na amebainisha kuwa Tanzania yenye neema inawezekana endapo kila mtu atazingatia kufanya kazi.

“Tukifanya kazi hatuhitaji hata misaada kutoka nje, nchi hii ina neema nyingi. Kwa kweli tukifanya kazi kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi nyingine na sio kuomba misaada kutoka nchi nyingine” Amesisitiza Dkt. Magufuli.

Rais Magufuli ambaye amesali kwenye kanisa hilo kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini ikiwa ni mara yake ya nne kusali katika kanisa hilo hata kabla ya kuwa Rais, amewaomba watanzania kuendelea kuliombea Taifa lao na pia kumuombea yeye ili afanikiwe kutekeleza jukumu kubwa na zito la kuiongoza nchi.

Pamoja na kuongoza maombi ya kumuombea Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli waliohudhuria ibada hiyo, Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa amempongeza Rais Magufuli kwa tabia yake ya kupenda kuhudhuria ibada na kuwasihi viongozi wengine kupenda ibada.

Askofu Malasusa ameuelezea ufufuo wa Yesu Kristo kuwa jambo la kuleta  matumaini, na hivyo amepongeza mwelekeo wa nchi kwa sasa, huku akisema Kanisa linaona matumaini kwa Taifa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini huku akisikilizwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa na Mchungaji Chalres Mzinga baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakisalimiana na waumini baada ya Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akisalimiana na mtoto Javiera Lyimo (9) anayesoma darasa la tano shule ya Genesis jijini  baada ya  Ibada ya Pasaka katika Kanisa la KKKT la Azania Front jijini Dar es salaam leo Machi 27, 2016.

KUMEKUCHA TAMASHA LA DINI LA UPENDO MUSIC FESTIVAL JUMAPILI YA PASAKA WASHIRIKI WAPO HAPA

Ikiwa zimebaki siku mbili yaani Jumapili ya Machi 27.2016 wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake wanatarajia kushuhudia tamasha la dini la Upendo Music Festival ambalo litaambatana na matukio mbalimbali ndani ya viwanja vya Leaders Club.
Tamasha hilo linaloandaliwa na kampuni ya Legendary Music Entertainment and Promotions Company Limited tayari imeweka wazi baadhi ya vikundi na wasanii washiriki wa tamasha hilo.
Baadhi ya Wasanii hao wenye kalama na upeo mkubwa katika kumuimbia Mungu wanaotamba ndani na nje ya Tanzania ni pamoja na: Angel Bernard, Emanuel Mbasha, Lynga George, Upendo Kihaile, Sarah Shilla, Faraja Ntaboba.
Pia wapo: Edson Mwasabwite, Angel Magoti, Abeid Ngosso, Ambwene Mwasongwe na Fridah Felix.
Aidha, washiriki wengine katika orodha hiyo ni pamoja na: Choir ya Kigogo KKKT, Gift and Beauty, Moses Saxer, Mise Ricprdias, The Joshua Generation, Glorious Worship Team, The Voice, Uinjilist Choir Kimara.
Wengine ni Doxers Praise Team, Calvary Band, The Jordan, The Next level, Chang’ombe Vijana Choir, Uinjilist Kijitonyaama, Tumaini Shangilieni Choir na wengine wengi.
Katika tamasha hilo hiyo siku ya Jumapili ya PASAKA, katika viwanja vya LEADERS CLUB, Kinondoni, linatarajia kuanza majira ya asubuhi ya nne ( 4:00) Hadi Saa 10:00 Usiku. Pia litajumuisha na Bonanza la Michezo, Michezo ya Watoto na Uuzaji wa Biashara mbali mbali
Kiingilio kawaida ni Tsh.5,000 na kwa viti maalum ni Tsh.10,000 huku kwa Watoto ni Tsh. 2,000.
“Music 100% Live, Njoo tumuimbie Mungu”.. Ulinzi na Usalama ni wa hali ya juu nyoote munakaribiswa.
abeddy_2
Abeid Ngosso
frida1
Fridah Felix
U36-620x399
Emanuel Mbasha Sarah Shilla
Sarah Shilla.
nightofhope17
Ambwene Mwasongwe.
Edson Mwasabwite
Edson Mwasabwite.
FB_IMG_1450057063985
Angel Bernard.
UPENDO MUSIC FESTIVALThe VoiceKundi la The Voice

MKUU WA WILAYA YA GEITA AWATAKA WANANCHI WA MKOA HUO KUMRUDIA MUNGU NA KUACHA MAUAJI YA ALBINO NA VIKONGWE

1
Mmoja wa Mashabiki wa Tamasha la Pasaka pamojana mashabiki wengine waliohudhuria katika Tamasha la Pasaka lililofanyika mjini Geita Mkoani Geita kwenye ukumbi wa Desire wakiimba kwa kuzinguka ukumbi huo wakati mwimbaji Upendo Nkone alipokuwa akifanya vitu vyake jukwaani na kuwafanya wavutiwe na tamasha hilo kiasi cha kushindwa kukaa kwenye viti wakizunguka huku na kule huku baadhi wakiwa wabebeba viti juu juu,
Katika Tamasha hilo mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangachie akizungumza na mashabiki wa muziki wa injili waliohudhuria katika tamasha hilo ameishukuru kampuni ya Msama Promotion na Mkurugenzi wake Bw. Alex Msama kwa kuandaa tamasha hilo kwani hiyo ni fursa pekee ya baadhi ya wananchi wa mkoa wa Geita kumrudia Mungu na kutubu ili kuacha tabia mbaya inayoupaka matope mkoa huo kwa mauaji ya walemavu wa ngozi Albino pamoja na Vikongwe
Waimbaji mbalimbali wameshiriki katika tamasha hilo ambao ni Upendo Nkone, Bonny Mwaiteje, Joshua Mlelwa, Martha Baraka, Jesca BM, Jennifer Mgendi, Mwimbaji kutoka Zambia Ephraim Sekereti, Waimbaji kutoka Nchini Kenya Solomon Mukubwa , na Mtanzania Faustine Munishi pamoja naye Christopher Muhangila.
Matamasha hayo yataendelea kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na keshokutwa litafanyika tamasha lingine kama hilo mjini Kahama mkoani Shinyanga.
Tamasha la Pasaka linaandaliwa na Kampuni ya Msama Promotion chini ya mkurugenzi wake Bw. Alex Msama kwa udhamini wa magazeti ya Dira, Dira TV na Dira FM na linafanyika kila mwaka katika kipindi cha sikukuu za Pasaka (PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-GEITA)
2 3
Mwimbaji Jesca BM akifanya vitu vyake jukwaani.
4
Mashabiki wake wakiitikia na kuimba kwa hisia wakati mmwibaji huo akiimba jukwaani.
5
Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama akirekebisha sauti katika mitambo wakati tamasha hilo likiendelea huku DJ akiangalia.
6
Mama akifurahia uimbaji na uponyaji kutoka kwa waimbaji katika tamasha hilo huku akiwa amemshikilia mtoto wake mchanga.
7
Maadhi ya mashabiki wa muziki wa injili wakifuatilia waimbaji kwa makini.
8
Mwimbaji Martha Baraka na kundi lake wakitumbuiza jukwaani huku baadhi yamashabiki wakipata picha kwa simu.
9
Mwimbaji Jennifer Mgendi naye akafanya mambo makubwa jukwaani kama anavyoonekana.
10
Mwimbaji Ephraim Sekereti akisalimiana na mdau mkubwa wa Msama Promotion Bw. Silas huku akitaniana na Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangachie wa tatu kutoka kushoto waliosimama mara baada ya kumaliza kuimba.
12
Mwimbaji Solomon Mukubwa kutoka nchini Kenya akiimba jukwaani huku mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangachie akicheza pamoja na Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama na mashabiki wengine.
13
Mwimbaji Solomon Mukubwa kutoka nchini Kenya akiimba kwa hisia mbele ya mashabiki wake walioonekana kuhamasika na nyimbo zake.
14 15 16
Mwimbaji Bonny Mwaiteje naye akafanya mambo makubwa jukwaani huku akipewa sapoti na mashabiki wake.
17 18 19
Mwimbaji Bonny Mwaiteje akiwa amewabeba wacheza shoo wake mara baada ya kumaliza kuimba jukwaani hii ilikuwa ni staili ya aina yake.
20
mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangachie akitoa salamu zake za shukurani kwa kampuni ya Msama Promotion kwa kuandaa tamasha la pasaka katika mkoa wa Geita wilaya ya Geita kwa ni jambo jema kuwahubiria amani wananchi wa Geita ili wamrudie Mungu na kuacha mauaji ya Albino na Vikongwe.
21
Waimbaji Solomon Mukubwa kulia , Bonny Mwaiteje kushoto wakimpiga tafu Mwimbaji mwenzao Christopher Muhangila katikati wakati alipokuwa akitumbuiza jukwaani.
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube