BREAKING

Friday 27 November 2015

BREAKING NEWZZZZZZ,RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT JOHN POMBE MAGUFULIAMSIMAMISHA KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA TRA BWANA RISHED BADE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa tanzania Dkt.John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Bwana Rished Bade na kumteua Bwana Philip Mpango kukaimu nafasi hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya mawasiliano ya Rais Ikulu Jijini Dar es Salaam, jioni hii imesema Rais Magufuli amemtaka Bwana Rished Bade kumpa ushirikiano wote kaimu Kamishna Mpango katika Uchunguzi kuhusu makontena 349 yaliyotoka Bandarini  bila taarifa zake kuwepo katika mamlaka ya mapato Tanzania .

 

BREAKING NEWZZZZZ….WAZIRI MKUU MAJALIWA AVAMIA BANDARI LEO, AAMRISHA KUKAMATWA KWA MAAFISA KIBAO WA TRA



Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa  wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi  baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia.
Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri. Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
 Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa  akiagana na viongozi wa TRA na TPA.

 

Wednesday 25 November 2015

JUKWAA HURU LAKOLEZA KASI YA RAIS DK. MAGUFULI

Baada ya Rais Dk. John Magufuli kuonyesha dhamira yake ya thati kutaka kuliinua taifa la Tanzania kutoka katika lindi la umasikini katika nyanja mbalimbali, kwa kupunguza gharama zisizo za lazima ikiwemo fedha zinazoangamia katika posho, sherehe na safari za nje, Leo Jukwaa Huru la Wazalendo limejitokeza kumuunga mkono kwa kutoa tamko zito. Pichani, Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Ally Salum Hapi akizungumza na Waandishi wa habari leo katika hoteli ya Travertine, Magomeni jijini Dar es Salaam akiwa na Katibu wake, Mtela Mwampamba (kulia).

IFUATAYO NI TAMKO HILO KAMA LILIVYOSOMWA NA VIONGOZI HAO.


JUKWAA HURU LA WAZALENDO
TAMKO LA JUKWAA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ndugu Wanahabari,

Mbele yenu sisi tuliowaita hapa ni Jukwaa Huru la Wazalendo ambalo limeitisha mkutano huu ili kufikisha yale tuliyoyakusudia kuwaeleza umma wa watanzania.


Sote tunatambua kuwa nchi yetu imetoka katika uchaguzi mkuu ambao umetupatia viongozi wapya wa awamu ya tano ya uongozi wa taifa letu chini ya Dr. John Pombe Joseph Magufuli. Tunapenda kuwapongeza watanzania wote kwa uchaguzi wa amani na utulivu. Aidha kwakua ndio mara yetu ya kwanza kuzungumza nanyi tunapenda kuwapongeza wanahabari wote kwa kazi nzuri ambayo mmekua mkiifanya kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchini. Tunawashukuru sana.

Mkutano wetu huu umebeba madhumuni makubwa mawili.
Kwanza ni kumpongeza Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa  hotuba yake aliyoitoa Bungeni siku ya ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mnamo tarehe 19/11/2015. Tunaiunga mkono Hotuba yake ambayo kwa kweli ilikuwa imebeba Uzalendo, Ujasiri, dira ya kweli ya maendeleo ya taifa letu na muuelekeo mpya wa Serikali ya awamu ya tano. Mambo yote aliyozungumzia Mh. Rais yamebeba maslahi mapana ya nchi yetu na yanalenga kuijenga Tanzania mpya ambayo waasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Abeid Amani Karume walikusudia kuijenga.

Pili, pamoja na mambo mengi yaliyogusiwa na hotuba ya Mh. Rais, eneo la kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa Serikali ni  moja katika mambo ambayo Jukwaa hili limeamua kuyaunga mkono kwa vitendo. Mh. Rais alitoa mchanganuo wa eneo moja tu la safari za nje na jinsi lilivyo ligharimu Taifa mabilioni ya shilingi na kuahidi kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake itajikita katika kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.

Aidha Mh. Rais ameanza kutekeleza kwa vitendo ahadi yake hiyo ya kupunguza matumizi yote yasiyo ya lazima Serikalini, ikiwemo hafla, warsha, makongamano na safari za nje.

Jukwaa Huru la Wazalendo, linatambua kuwa kwa miaka kadhaa mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe amekuwa na msimamo wa kutokupokea posho za kitako tangu akiwa mbunge wa Kigoma Kaskazini katika Bunge la 10. Pamoja na mh. Zitto, Jukwaa pia limepokea taarifa za baadhi ya wabunge wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioamua kuungaa mkono juhudi za Mh. Rais za kupunguza matumizi yasiyo ya lazima serikalini kwa kukataa hadharani kupokea posho ya kitako ya mbunge (sitting allowance).

Mnamo tarehe 23/11/2015, mbunge wa Singida Magharibi (CCM) Mh. Elibariki Imanuel Kingu alimwandikia barua Katibu wa Bunge akieleza msimamo wake wa kukataa kulipwa posho ya kitako ya Bunge (sitting allowance) katika kipindi chote cha miaka mitano (2015 -  2020). Huyu anakuwa ni mbunge wa pili baada ya Mh. Zitto Kabwe kutoka hadharani na kukataa posho ambazo msingi wake ni unyonyaji wa wanyonge na ubadhirifu wa kodi za wananchi.


Jukwaa linapenda kumpongeza Mh. Kingu Mbunge kwa ujasiri wake na Uzalendo kwa Taifa lake, uliomfanya kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vitendo.
Jukwaa linatambua ya kwamba, mapambano ambayo Mh. Kingu Mbunge ameyaanzisha ni makubwa, magumu na yanahitaji kuungwa mkono na watanzania wote wanaoipenda nchi yao bila kujali itikadi za vyama. Tunafahamu, wapo baadhi ya wabunge wabinafsi na wasio na huruma na wanyonge wa Taifa letu ambao hawajafurahishwa na hatua hii ya wabunge kama Zitto na Kingu ya kukataa posho ya kitako. Baadhi ya wabunge wameanza kumpigia simu na kumtumia jumbe (sms) za vitisho mh. Elibariki Kingu (MB) na wengine wakibeza kuwa anatafuta cheo.

Jukwaa linalaani hatua za wabunge hao wanaopinga nia njema ya Mh. Elibariki Kingu na Mh. Zitto Kabwe kwa uamuzi wao wa kukataa posho za kinyonyaji na hivyo basi, Jukwaa linawaomba wananchi wote majimboni, kuwataka wabunge wao waliowachagua kueleza misimamo yao hadharani juu ya kuunga mkono hatua ya kukataa posho kama njia ya kupunguza matumizi ya Serikali yasiyo ya lazima.

Jukwaa linafahamu ya kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kuidhinisha masharti ya kazi za kibunge na stahiki wanazopaswa kulipwa katika kazi hiyo.


Kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, tunamuomba na kumshauri Mh. Rais John Pombe Magufuli atakapokuwa anaidhinisha masharti na stahiki hizo, atusaidie kuifuta kabisa posho ya kitako ya wabunge (sitting allowance).


Aidha, Jukwaa linamuomba mh. Rais kuzipitia na kutoa agizo la kufutwa kwa posho zote zisizo za lazima zinazolipwa kwa watumishi wa umma wa kada mbalimbali yakiwemo mashirika ya umma.

Jukwaa letu linatoa wito kwa wabunge wote bila kujali vyama vyao, kuungana na Mh. Kingu(MB) na Mh. Zitto(MB) katika kukataa malipo ya posho ya kitako ili kupunguza mzigo mkubwa ambao Serikali inaubeba kuhudumia wabunge. Fedha hizi ni vyema zielekezwe katika kutatua kero za wananchi vijijini kama vile ukosefu wa maji, madawati, vitanda vya Hospitali n.k.

Tunasisitiza kwamba, Ubunge ni Utumishi,na wala sio Utukufu. Kazi ya Mbunge ni kuwawakilisha wananchi wake na si kuwanyonya. Tufike mahali kama Taifa tuwe na nidhamu ya matumizi ya kodi za wananchi na mgawanyo sawa wa keki ya Taifa. Kuendelea kulipana posho hizo ni ishara ya unyonyaji, dhuluma na kuongeza pengo kati ya wenye nacho na wasionacho nchini. Jambo hili linakuza chuki na hasira miongoni mwa wananchi wa hali ya kawaida dhidi ya viongozi wao na serikali kwa ujumla.

Tunawaahidi kuwa Jukwaa litaendeleza harakati (movement) na vuguvugu hili kwa kuanzia na Bunge kwasababu ndio wawakilishi wa wananchi. Tutaendelea kupaza sauti zetu ili wabunge wengi zaidi Wazalendo wajitokeze na kukataaa posho hizi. Tunajua kuwa wapo miongoni mwao wabunge wazalendo ambao wataguswa na wito huu na kuuunga mkono hadharani.


Aidha tutaendelea kuwasemea kwa wananchi wabunge ambao bado hawataki kukataa posho hizi bila kujali vyama vyao. Tunawaomba wananchi kote nchini kutuunga mkono katika harakati hizi ili tuweze kuokoa mabilioni ya shilingi yanayopotea kila Bunge linapokaa Dodoma kupitia posho ya kitako (sitting allowance).
Ahsanteni sana.

ALLY SALUM HAPI  - MWENYEKITI (0714 193161
MTELA MWAMPAMBA  - KATIBU   (0755 178927)

Tuesday 24 November 2015

UTT-PID YASHIRIKI MKUTANO WA MWAKA WA WANAHISA WA UTT-AMIS JIJINI DAR ES SALAAM.

 1 (1)
Maafisa masoko wa UTT-PID, Laurence Nzuki (kushoto) na Martin Mchanjila (katikati) wakitoa maelezo kwa baadhi ya watu waliotembelea kwenye banda hilo la UTT-PID wakati wa mkutano huo wa mwaka wa Wanahisa wa UTT-AMIS uliofanyika mwishoni mwa wiki, Novemba 21-22.2015, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.

Na Andrew Chale,

Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyochini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID) inafanya miradi mbalimbali ikiwemo huduma za uuzwaji wa viwanja katika maeneo tofauti nchini ikiwemo vile vya mradi wa katika miji ya Chalinze na Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani. Pia mradi wa viwanja vya Bunju, Tundwi songani-Kigamboni ambayo ipo Jijini Dar es Salaam. Mingine ni Kingorwila, Madaganya, Mkoani Morogoro. Lindi, Bukoba, Sengerema na kwingine kwingi hapa nchini.

UTT -PID ni miongoni mwa taasisi zinazofanya vizuri na utendaji wa kasi katika utoaji huduma za ushahuri katika maeneo ya upembuzi yakinifu wa miradi mbalimbali, Uratibu wa fedha na huduma zinazohusiana katika maandalizi ya mapendekezo ya miradi kwa benki au taasisi za fedha, uteuzi wa watoa huduma kuhusiana na maandalizi ya zabuni na usimamizi wa majengo na mali ambao ni utoaji wa huduma fanisi za usimamizi wa majengo yaliyochini ya uangalizi thabiti wa taasisi.
 
AiAlRphYQ4ymV39Xi_bF6xKSDvBBPFilGkB-PlxHPShu
AsfOxbUQv7XGaXHM7H-QB4HDmtD0NoXc-5OrHiTpRdSO
Picha ya juu na chini Afisa masoko wa UTT-PID, Mary Lugusi akielimisha wananchi juu ya miradi inayoendeshwa na taasisi hiyo kwa wananchi hao waliotembelea banda hilo.
AuISTCaTvV-iYBU-Kfj_MXe9kHuIQPYgU4bZXhQo6OXa
Wananchi wakitembelea banda hilo la UTT-PID..
AmP8BMKF9VkuKPXrXzrxLFNdWA_ZhP3KDMoYW5wunYlG
Mkuu wa Mahusiano ya Umma UTT-PID, Eugenia Simon akiwa pamoja na Mshahuri wa masuala ya uwekezaji wa UTT-Micro finance wakati wa mkutano huo mkuu wa mwaka wa wanahisa wa UTT-AMIS, uliofanyika Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.
AnQqTlX1RpGgYJtjKG4oeWsJ-LyltzccztY6XmJx9t4j
Mmoja wa wananchi akipata maelezo kutoka kwa afisa masoko wa UTT-PID, Mary Lugusi.

Monday 23 November 2015

SHEREHE ZA MIAKA 54 YA UHURU RAIS AFUTA GWARIDE ASEMA SASA SIKU HIYO ITATUMIKA KUFANYA USAFI

              Rais John Pombe Magufuli

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Joseph Magufuli, amefuta sherehe za Uhuru za desemba tisa mwaka huu ambazo zilikuwa zikifanyika kila mwaka na badala yake ameagiza siku hiyo itumike kufanya usafi kwa kila mwananchi.

Rais amesema ni aibu kwa taifa kuadhimisha miaka 54 ya uhuru mwaka huu huku likikabiliwa na ugonjwa wa kipindupindu ambao kwa kiasi kikubwa unasababishwa na uchafu, na ameagiza watendaji wote wa halmashauri na manispaa nchini kuahikikisha wanatayarisha vifaa vya kufanyia usafi ili kila mwananchi aweze kushiriki.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam amesema fedha ambazo zingetumika kwenye maadhimsho ya sherehe za Uhuru mwaka huu zitaelekezwa kwenye maeneo ambayo rais ataona zina mahitaji sana.

Wakati huo huo Balozi Ombeni Sefue amewataka watumishi wote wa Umma kuanza kuvaa Beji zenye Majina yao kwenye nguo zao kutoa fursa kwa wananchi kujua nani anamhudumia.


Kuhusiana na safari za nje kwa watumishi wa umma, Balozi sefue ana fafanua

Thursday 19 November 2015

BREAKING NEWZ:HUYU NDIYE NAIBU SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

                                                
     Dkt.Tulia Ackson Mwansasu

Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, limempitisha Dkt .Tulia Mwansasu kuwa Naibu Spika wa Bunge la 11, kwa kura 250 sawa na asilimia 71.2% dhidi ya mpinzania wake Mh.Magdalaena Sakaya aliyepata kura 101, sawa na 28.8%. 

HUYU NDIYE WAZIRI MKUU WA JAMHURI WA MUUNGANO WA TANZANIA , NI KASSIM MAJALIWA

 Waziri wa Tamisemi Elimu Kassim Majaliwa akiteta Jambo na Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Zubeiry Kabwe.


Waziri wa Tamisemi Elimu Kassim Majaliwa ateuliwa kuwa waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania




Wednesday 18 November 2015

KAMPUNI YA LETSHEGO YAFAIDIKA YAPATA ASILIMIA 75 YA HISA KATIKA BENKI YA ADVANS TANZANIA




Kampuni ya LETSHEGO Holding Limited yenye makao yake makuu nchini Botswana ambayo kwa Tanzania ikijulikana kama taasisi ya Mikopo ya Faidika, imetangaz kupata asilimia 75 ya hisa kutoka katika benki ya Advans ya Tanzania kwa kununua hisa moya kwa shilingi Bilioni 15.5 ambazo ni sawa na dola za Kimarekani Milioni 7.

Wakizungumza mbele ya waandishi wa habari mapema jana jijini Dar es Salaam, viongozi wakuu wa Faidika na Advans Tanzania wamebainisha kuwa sasa huduma za kifedha nchini zimeongezeka maradufu hivyo ni fursa za kipekee kwa watanzania wakiwemo wajasiriamali kujitokeza kwa wingi kuchangamkia huduma katika benki hiyo ya Advans. 

"Kufanikiwa kwa Faidika, kunaongeza uwekaji wa akiba, malipo, mikopo ya biashara ambayo ni moja ya mikakati yetu kwa wateja wetu. Hii pia itaruhusu benki ya Advans kutoa mchango mkubwa kwa Serikali ya Tanzania" ameeleza Mkurugenzi Mkuu wa Letshego Group, Chris Low katika tukio hilo.

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa, Benki kuu ya Tanzania (BOT) imeipatia kibali taasisi hiyo ya Faidika kuwa wakala wa benki ya Advans wa kutoa huduma za kibenki kwa niaba ya benki hiyo, katika vituo takribani 105.

Hata hivyo Letshego inaamini kuwa mafanikio hayo ni ishara tosha ya kutoa huduma bora kwa watu wote ikiwemo wale wa kipato cha chini, kati katika jamii ambao kihistoria hawajaweza kupata huduma stahiki katika benki za biashara hivyo mfumo mzuri wa kuwezesha jamii kupata huduma za kifedha, Letshego imekuja wakati muafaka wa kusaidia Serikali kuinua uchumi.

Letshego/Faidika kwa Tanzania inatoa huduma zaidi ya Watanzania 44,000 kupitia taasisi yake hiyo ya mikopo ya Faidika huku bidhaa na huduma zake pia zikipatikana kupitia mitandao wenye matawi zaidi ya 105 na ofisi za Satelaiti huku ikiwa na timu ya maafisa mauzo wapatao 230.

DSC_1778
Mkurugenzi Mtendaji wa Advans Tanzania, Bwana Tanguy Gravot (wa kwanza kulia) akizungumza kwenye mkutano mkutano huo. Wengine ni maafisa kutoka kampuni ya Letshego ambao wamenunua hisa asilimia 75 kwa benki hiyo ya Advans Tanzania.
Kwa upande wao benki ya Advans Tanzania wamepongeza kampuni ya Letshego kuwa mbia mkuu wa benki hiyo kwa njia ya uuzwaji wa hisa. Kwa hatua hiyo Letshego atakuwa mwanahisa mkuu huku wale wanahisa waanzilishi wa benki hiyo wakiwemo Advans SA na FMO watabaki kuwa wanahisa wadogo wa kampuni.
"Umoja ulioundwa kati ya kampuni hizi mbili utaiwezesha benki ya Advans Tanzania kutoa huduma zilizo bora kwa wateja wote wakiwemo wale wadogo, wa kati na wakubwa kwa maeneo yote huku pia kuongeza wigo wa kijiografia za huduma." alieleza Mkurugenzi Mtendaji wa Advans SA, Bw. Claude Falgon.
Kwa hatua hiyo, Advans inaamini kuwa wajasiriamali waadogo na wa kati ni wakati wa kuchangamkia fursa zaidi katika benki hiyo.
Advans ya Afrika Kusini (Advans SA) ni kampuni iliyoundwa tokea mwaka 2005 na Developement Finance 9Horus) pamoja na Eid,KfW, FMO, CDC Group plc, AFD group na IFC huku shughuli yake kubwa ikiwa ni kutengeneza mtandao wa taasisi ndogo ndogo za kifedha (MFIs) katika nchi zinazoendelea na zinazoinukia ilikutoa huduma za kifedha kwa wajasiliamali wadogo na wa kati.
Mtandao wa Advans umesambaa karibu dunia nzima ambapo pia waweza kutembelea mtandao wa : www.advansgroup.com
DSC_1807
Mkurugenzi Mkuu wa Letshego Group, Chris Low (katikati) akifafanua jambo kwa wanahabari (hawapo pichani) wakati wa shughuli hiyo ya kutangaza kuingia ubia na benki ya Advans Tanzania.
DSC_1801
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia shughuli hiyo..
DSC_1826
Mmoja wa wajumbe wa Bodi wa Taasisi ya mikopo nchini ya Faidika, Dk.Ellen Otaru Okoedion akielezea fursa za mikopo inayotolewa na Faidika huku akitumia wasaha huo kuwaomba wajasiriamali kujitokeza kwa wingi kuchangamkia huduma za kibenki na mikopo zinazotolewa na Faidika pamoja na benki ya Advans Tanzania.

Friday 13 November 2015

MVUA ZAHAIRISHA MECHI KATI BRAZIL NA AGERNTINA




Mchezo wa kuwania kufuzu kwa kombe la dunia kati ya Brazil na Argentina umeahirishwa kufuatia mvua nyingi kunyesha, na kusababisha kujaa kwa maji .

Mchezo huo ulikuwa  usiku wa siku ya alhamisi katika uwanja wa Estadio Antonio Vespucio Libert, mjini Buenos Aires sasa utachezwa usiku wa siku ya ijumaa.

Sehemu ya kuchezea ya uwanja huo ulijaa maji na washabiki wa soka pamoja na maafisa wa timu ya Brazil walikwama njiani kwenye foleni sababu ya mvua kubwa iliyonyesha.

Kocha msaidizi wa Brazil Gilmar Rinaldi, alisema "tulikutana na maafisa wa soka wa Argentina tukazungumza na hakukua na namna ya mchezo kuchezwa.

Katika mchezo huu Argentina itamkosa Nahodha wake Lionel Messi anayesumbuliwa na maumivu wakati Brazil itakuwa nae tena Nahodha wao Neymar Jr ambae hakucheza Mechi 2 za mwanzo akutokana na kuwa adhabu ya kutocheza michezo minne.

KOCHA MKUU WA TAIFA STARS BONIFACE MKWASA TAMBA KUWAFUNGA WA ALGERIA KESHO UWANJA WA TAIFA,AJIVUNIA SAMATTA ,NGASSA,ULIMWENGU

 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali Nchini na wengine nje ya nchi wakimsikiliza kocha wa Stars Boniface Mkwasa,kuelekea michezo wa kesho na Algeria.
 Mkwasa akisistiza jambo


Thursday 12 November 2015

KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU TAIFA YA CCM,YAMTEUA NDUGU DEOGRATIUS NGALAWA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA LUDEWA.


TIKETI ZA STARS, ALGERIA KUUZWA KESHO



Tiketi za mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia chini Urusi mwaka 2018 kati ya Tanzania dhidi ya Algeria ziataanza kuuzwa kesho Ijumaa katika vituo 10 viliyopo jijini Dar es salaam.

Magari maalumu yenye stika yataanza kuuza tiketi hizo za mchezo kesho saa 2 kamili asubuhi mpaka saa 12 jioni, ambapo tiketi zinauzwa kwa shilingi elfu tano (5,000) kwa viti vya rangi ya bluu na kijani na rangi ya machungwa, na elfu kumi (10,000) kwa viti vya VIP B & C.

Vituo vitakavyotumika kuuza tiketi hizo ni ofisi za TFF – Karume, Buguruni – Oilcom, Mbagala – Darlive, Mnazi Mmoja, Luther House – Posta, Big Bone – Msimbazi, Ubungo – Oilcom, Makumbusho – Stand ya Daladala, Uwanja wa Uhuru.

TFF inawaomba wadau, washabiki na watanzania kujitokeza kwa wingi kununua tiketi za mchezo huo katika magari maalumu yatakayokuwepo kwenye vituo vilivyotajwa, ili kuondokana na tatizo la kuuziwa tiketi zisizokuwa halali.

Wakati huo huo Ubalozi wa Algeria nchini Tanzania, umewataka waandishi wa habari wanaotrajia kwenda kuripoti mchezo wa marudiano jijini Algiers siku ya jumanne, kuwasilisha maelezo ya chombo wanachofanyia kazi pamoja na vifaa watakavyovitumia kwenye mchezo huo (camera, vinasa sauti) kuwasilisha maelezo hayo leo Alhamsi kabla ya saa 9 mchana katika ofisi za Ubalozi huo kwa ajili ya kupatiwa Accreditation za kufanyia kazi.

Matokeo ya mchezo wa jana  Azam Sports Federtaion Cup (ASFC), ni Mshikamano 0 - 1 Cosmopolitan,

BILITY MARAFUKU KUWANIA URAIS FIFA

Raia wa Liberia Musa Bility ameondolewa kutoka kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa Fifa kwa sababu ya maadili.

Shirikisho hilo linalosimamia soka duniani limeidhinisha wagombea watano pekee. Mkuu wa Uefa Michel Platini pia hajajumuishwa kwenye orodha hiyo ya wagombea.

Mfaransa huyo hata hivyo huenda akaongezwa iwapo marufuku yake itamalizika kabla ya uchaguzi kuandaliwa Februari.

Mwanamfalme Ali bin al-Hussein, Jerome Champagne, Gianni Infantino, Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa na Tokyo Sexwale ndio pekee walioidhinishwa.

Fifa imesema haitazungumzia zaidi sababu za kutemwa kwa Bility, ambaye anaweza kupinga uamuzi huo katika mahakama ya kutatua mizozo ya michezo. Imesema imeamua kutofichua maelezo zaidi kuhusu sababu hizo kwa maslahi ya Bility.

Bility ndiye rais wa shirikisho la soka la FA.

Uchaguzi huo utachagua mrithi wa Sepp Blatter, ambaye amesimamishwa kazi na anachunguzwa kwa tuhuma za ufisadi.

Blatter, 79, alitangaza atajiuzulu mwezi Juni baada ya Fifa kukumbwa na kashfa ya ufisadi.

Wagombea waliosalia Fifa
  • Mwanamfalme Ali bin al-Hussein, 39, ndiye rais wa Shirikisho la Soka la Jordan.
  • Jerome Champagne, 57, ni afisa mkuu mtendaji wa zamani wa Fifa.
  • Gianni Infantino, 45, ndiye katibu mkuu wa Uefa
  • Michel Platini, 60, ndiye rais wa Uefa na naibu rais wa Fifa (Ugombea wake bado haujaidhinishwa.)
  • Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa, 49, ndiye rais wa Shirikisho la Soka la bara Asia
  • Tokyo Sexwale, 62, ni waziri wa zamani wa Afrika Kusini
 

RC MAHIZA AUTAKA MFUKO WA BIMA YA AFYA (NHIF) KUTOA ELIMU ZAIDI KWA WANANCHI JUU YA UMUHIMU WA KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII (CHF)

MKUU WA Mkoa wa Tanga,Mwantumu Mahiza ameutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani hapa kuendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)ili kuweza kuongeza wigo mpana wa wanachama ambao wataweza kunufaika na huduma zao.

  Alitoa wito huo jana wakati akipokea mashuka 150 yaliyotolewa na mfuko huo vyenye thamani ya shilingi milioni tatu yaliyotolewa na Mfuko huo kwa ajili ya vituo vitatu vya afya vya Mkinga, Maramba na Lanzoni vilivyopo wilayani Mkinga ambavyo zilikuwa zikikabiliwa na changamoto ya uhaba wa mashuka. 



Monday 9 November 2015

MSANII BOBO SERETSANE "BO" WA AFRIKA KUSINI AFAGILIA MUZIKI WA TANZANIA , APONGEZA TAMASHA KARIBU MUSIC

DSC_0896
Msanii nyota wa Afrika Kusini, Bo Denim "Bo" akitumbuiza jukwaani wakati wa tamasha la msimu wa pili la Karibu Music Festival..!

[BAGAMOYO-TANZANIA] Mwanamuziki nyota kutoka Afrika Kusini Bo Denim maarufu ‘Bo’ amewashukuru waandaji wa tamasha la Music Festival linalofanyika kila mwaka mjini hapa huku likihusisha vikundi na wanamuziki mbalimbali kutoka mataifaa tofauti ya Afrika nan je ya Afrikaa.
Bo ambaye usiku wa jana Novemba 7, aliweza kupiga shoo hiyo kwa kiwango cha Kimataifa, alipata shangwe kwa mashabiki waliofurika kushuhudia tamasha hilo mjini hapa.
Baada ya shoo hiyo Modewji ilipata kufanya naye mahojiano ambapo amepongeza muziki wa Tanzania wakiwemo wasanii wanaovuma nje ya mipaka ya Tanzania. “Wasanii wa Tanzania wanauwezo mkubwa. Nimeshuhudia kundi la Weusi wamefanya vizuri sana” ameeleza Bo.
Tamasha hilo ambalo leo Novemba 8.2015, linatarajiwa kufikia tamati, linaratibiwa na Karibu Cultural Promotions Organization (KCPO) na Legendary Music Entertainment and Promotions Co. Ltd, T kwa kushirikiana na kampuni ya kinywaji cha Jebel Coconut. Wadhaminiwa wengine ni pamoja na Swiss Embassy, Precision Air, Coca Cola, Mwananchi Communication, Kaya fm, Magic fm, Focus Outdoor, Jovago, Kaymu na Time tickets.
DSC_0882
DSC_0858
DSC_0848
DSC_0843
DSC_0835
Bo akipagawisha mashabiki ...
DSC_0852
DSC_0884
DSC_0890
Mambo yalikuwa hivi ..
DSC_0884
DSC_0910
Host wa Karibu Music Festival 2015, Jazzphaa Nassor na Lulu wakishoo love wakati wa shoo hiyo ya "Bo"..

PAPAA WEMBA AFANYA MAAJABU KWENYE TAMASHA LA KARIBU MUSIC FESTIVALS 2015

DSC_1032
Mwanamuziki nguli wa dansi kutoka DRC Congo, Papaa Wemba kushoto akiimba na kucheza sambamba na madansa wake jukwaani usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la muzuki la Karibu Music Festival msimu wa pili linaloendelea katika viwanja vya Mwanakalenge,mjini Bagamoyo. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[BAGAMOYO-TANZANIA] Mwanamuziki kutoka Congo mwenye makazi yake nchini Ufaransa, Papaa Wemba, ameweza kuonyesha ukomavu wake kwenye muziki wa dansi licha ya kuwa na uri wa miaka 66, kwa kupiga shoo ya aina yake usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Karibu Music Festival 2015 linaloendelea ndani ya viwanja vya Mwanakalenge, Bagamoyo-Tanzania.
Katika shoo hiyo, Papaa Wemba aliweza kupanda jukwaani akiwa na bendi yake na kupiga nyimbo zaidi ya tano zilizokonga nyoyo mashabiki lukuki waliofurika ndani ya viwanja hivyo vya Mwanakalenge mjini hapa.
Papaa Wemba ambaye anatamba kwa muda mrefu na wimbo wa “Show Me The Way” ameweza kuwa miongoni mwa wasanii wa muziki wa dansi kutoka DRC Congo kufika Tanzania kwa mara ya pili sasa kwa vipindi tofauti huku watanzania wengi wakionyesha kumkubali na kufuatilia muziki wake mara kwa mara.
Baada ya shoo hiyo Papaa Wemba aliwashukuru Watanzania kwa kujitokeza kwa wingi na kumuunga mkono katika muziki wake ambapo alieleza kuwa tamasha hilo la Karibu Music Festival licha ya kuwa change kwa kufanyika mwaka wa pili, huko linakoelekea litakuwa kubwa zaidi na kuwa maarufu.
Katika shoo hiyo, Papaa Wemba aliimba nyimbo zaidi ya nne huku akiimba pia vibao kadhaa vilivyowahi kutamba miaka ya nyuma pamoja na nyimbo mbalimbali zikiwemo mpya.
Tamasha hilo ambalo leo Novemba 8.2015, linatarajiwa kufikia tamati, linaratibiwa na Karibu Cultural Promotions Organization (KCPO) na Legendary Music Entertainment and Promotions Co. Ltd, T kwa kushirikiana na kampuni ya kinywaji cha Jebel Coconut. Wadhaminiwa wengine ni pamoja na Swiss Embassy, Precision Air, Coca Cola, Mwananchi Communication, Kaya fm, Magic fm, Focus Outdoor, Jovago, Kaymu na Time tickets.
DSC_1025
Papaa Wemba akiimba jukwaani kwenye tamasha la Karibu Music Festival 2015, usiku wa kuamkia leo kwenye viwanja vya Mwanakalenge, mjini Bagamoyo
DSC_1099
Papaa Wemba akiwaimbisha mashabiki wake (hawapo pichani ) kwenye tamasha la Karibu Music Festival 2015, usiku wa kuamkia leo kwenye viwanja vya Mwanakalenge, mjini Bagamoyo
DSC_1027
Wanenguaji wa Papaa Wemba wakishambulia jukwaa kwa style ya aina yake ambao walikuwa kivutio katika tamasha hilo..
Sebene likiendelea jukwaani..
DSC_1102
Host wa tamasha la Karibu Music Festival 2015, Mc Lulu akipata kuimbisha mashabiki waliofurika katika tamasha hilo kwa kuimba sambamba na Papaa Wemba (Hayupo pichani) kibao cha "Show Me the way"..
DSC_1087
Papaa Wemba katika ubora wake..
DSC_1130
DSC_1030
Dansa akifanya yake jukwaani..
DSC_1063
DSC_1080
Papaa Wemba..
DSC_1090
Mwenyekiti wa tamasha la Karibu Music Festival, Amarido Charles (kushoto) akiwa pamoja na mwanamuziki kutoka Afrika Kusini, Bodenim 'Bo' katika viunga vya tamasha hilo viwanja vya Mwanakalenge..
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube