BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 14, 2025

Wednesday, 7 October 2015

MSANII WA FILAM TANZANIA RAY AWATAMBIA UPINZANI ASEMA WAO KUKAMATA NCHI BAADO SAANA


Na Mwandishi Wetu
Msanii Nguli wa filamu nchini, Ray Kigosi, amewaambia watanzania leokuwa makini na kusikiliza sera na kuachana na mihemko ya kisiasa itakayopelekea wao kufanya maamuzi watakayoyajutia baadae.
Kigosi ameyasema hayo alipokuwa katika moja ya mikutano inayoendeshwa na kundi la wasanii lenye kauli mbiu ya Nimestuka, katika jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kundi hilo inayopita kijiji kwa kijiji katika kuhakikisha kwamba wanawaelimisha vijana wenzao kuhusiana na usikilizwaji wa sera na mapokeo ya demokrasia kwa jamii.
Awali akiongea kabla ya kuwakaribisha wenzake 12 alioandamana nao, Kigosi amesema yeye alipokuwa Ukawa alikuwa akishuhudia vijana wakihamasishwa kupinga hata mambo yanayoonekana kuwa na tija yaliyofanywa na seriikali jambo ambalo yeye mwenyewe aliliona kuwa ni upotoshwaji wa wazi wazi.
"Naamini kuwa mpinzani, sio kupinga kila kitu, walipaswa pia kutufundisha jinsi ya kukabiliana na maisha kama vijana, lakini nikaja kugundua nimekosea sana kuacha kuungana mkono na Magufuli", alikiri Kigosi.
PICHANI JUU: Msanii wa filamu Ndende, akihamasisha wananchi wa Kishapu  kuhusiana na kumuunga mkono mgombea wa Chama cha Mapinduzi, Dk John Pombe Magufuli
Mchekeshaji Kitale, akiongea katika Mkutano wa Kampeni ya Nimes'tuka, inayoendeshwa na wasasnii wa filamu na muziki wa kizazi kipya, uliofanyika katika jimbo la Kishapu jioni hii
Inspekta Haroun, mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya akitoa burudani kwa wakazi wa jimbo la Kishapu baada ya mkutano wao wa kampeni ya Nimes'tuka, inayoendeshwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, wanaokiunga mkono Chama cha Mapinduzi
Muigiza filamu maarufu, Kajala Masanja, akiongea katika mkutano wa kampeni za Nimes'tuka, uliofanyika katika jimbo la Kishapu mchana wa leo, kulia ni Ray Kigosi
Mchekeshaji Mboto, naye ni mmoja kati ya wasanii wanaoendesha kampeni za Nimes'tuka, hapa akiongea na wananchi wa jimbo la Kishapu, mkoani Shinyanga
Muigizaji Skyner Ally naye akimwaga sera zake katika kampeni za Nimes'tuka
Miss Tanzania 2014, Lilian Kamanzima, akiongea na wananchi wa jimbo la Kishapu jioni ya leo katika mkutano wa kampeni za Nimes'tuka
Mikono juu...
Ray Kigosi akimwaga sera...
Msanii wa vichhekesho, StanBakora naye akiongea yake Kishapu leo

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube