BREAKING

Tuesday 2 April 2024

ROTARY CLUB WATOA MAFUNZO KWA WALIMU 80 YA KIDIGITAL

Jacline Woiso-Mwanachama wa Rotary Club 

Moses Fransis Mkuu wa Shule ya Msingi Kunduchi


Baadhi ya wanachama wa Rotary Club na walimu wakifurahia jambo wakati wa Uzinduzi wa Mafunzo ya Kidigital


Hamza kasongo Mwanachama Rotary Club akizungumza na walimu washiriki wa Mafunzo ya Kidigital 



Ili kuendana na kasi ya kidigital ya ukuajia wa teknolojia duniani Taasisi ya Rotary Klabu imetoa mafunzu ya Teknohama kwa walimu wa Shule tano za msingi  katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam,.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Mwananchama wa Rotary Klabu  Jackline Woiso amesema mafunzo hayo ni faida kubwa kwa walimu hao husuani kipindi hiki ambacho matumizi ya digital yanazidi kukua ambapo kuptia mafunzo hayo yatakapomalizika watakuwa wamepata faida.

Ameongeza  mafunzo hayo kwa walimu zaidi ya 80  itawajengea uwezo wa kutumia teknolojia hiyo  kwa upande wa uongozi na kuwajengea wanafunzi uwezo pindi wakiwa wakubwa kuendana na kasi ya Dunia  

Kwa upande wake Dkt. Gaudensia Tesha  Mhadhiri idara ya Kompyuta  Chuo cha DIT amesema kuwa mafunzo hayo ya walimu kutumia vishikwambi  itawasaidia kwa urahisi kuandaa matokeo ya mitihani yaweze kuchakatwa kwa urahisi, huku baadhi ya washiriki  wa mafunzo hayo Moses Fransis ambaye ni Mkuu wa Shule ya msingi Kunduchi akisema  kuna changamoto kubwa baadhi ya walimu wengi  hawana uelewa na mambo ya tehama hivyo itawasaidia kupunguza changamoto hiyo


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube