BREAKING

Tuesday 2 April 2024

DSTV WAZINDUA KAMPENI YA MFALME WA BOMA YAWEKA KIHISTORIA ...





Afisa maendeleo bodi ya Filam nchini Simon Peter, amewaka watunzi wa Filam nchini kuwa wabunifu ili kuendelea kutengeneza soko kubwa la ajira kwa wasanii huku akiwakumbusha wasanii kuendelea kusajili kazi zao za sanaa katika Bodi ya filam

Hayo ameyasema wakati wa uzinduzi wa Tamthiliya ya Jiya mfalme wa Boma , ambayo imeshirikisha wasanii mbalimbali ikibeba maudhui ya kitanzania 

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo akizungumza katika uzinduzi huo amesema kwamba kwa mara ya kwanza DSTV imepokea kazi yenye viwango vikubwa ikiwemo mchanganyiko wa wasanii maarufu na wasio maarufu.

Katika hatua nyingine kuelekea marudiano ya michuano ya vilabu bingwa Afrika ambapo Simba na Yanga zinatarajia kucheza michezo yao ambapo Simba watawavaa Al Ahly Ijumaa wiki hii na Yanga wakiwakabilia Mamelod Sundowns siku hiyo hiyo amazitakia kheria huku akisema timu hizo zinauwezo mkubwa wa kutinga hatua ya nusu fainali.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube