BREAKING

Thursday 8 June 2023

CHONGOLO :TUMIKIENI MATAIFA YENU AWAASA VIJANA WA AFRIKA


Katibu Mkuu wa Chama cha mapinduzi Daniel Chongolo akiwahutubia Viongozi Makada wa vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika  katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS) iliyopo Kibaha kwa Mfipa, mkoani Pwani.



Katibu
 wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema, akisikiliza kwa makini Mada katika ufunguzi a Mafunzo ya Viongozi Makada wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika ya Mwaka 2023







Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Daniel Chongolo akifuatilia baadhi ya mada katika mafunzo ya Viongozi vyama vya ukombozi 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  amewaasa  vijana kutoka bara la Afrika,ujitambua na kuwa tayari kuzitumikia nchi zao kwa weledi, uwezo na uzalendo mkubwa , hasa katika kuendeleza mambo mazuri yanyoambatana na kuongoza mapambano ya ukombozi wa kiuchumi kwa ajili ya wananchi 

Chongolo amesema hayo wakati akifungua Mafunzo ya Viongozi Makada wa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika ya Mwaka 2023 katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS) iliyopo Kibaha kwa Mfipa, mkoani Pwani.

Aidha  Chongolo amewataka vijana kutambua wajibu wa kuiandaa kwa wakati mwema wa uongozi kwa nyakati na mazingira ya sasa, ambapo wanatakiwa kujitambua na kubeba dhima ya uongozi unaolenga kuwatumikia watu kwa weledi na uzalendo mkubwa wa hali juu, kwa ajili ya kubadilisha na kuboresha hali za maisha ya watu.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kufanyika kwa takriban wiki mbili, ambapo yanawakutanisha vijana  viongozi na makada wa Vyama mbalimbali vikiwemo vya MPLA, SWAPO, FRELIMO, ANC na ZANU PF, CCM pamoja na CPC.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube