BREAKING

Tuesday 22 January 2019

SPORTSPESA NA DSTV WALIVYODHAMIRIA KUWAPA FURAHA WATANZANIA KATIKA MASHINDANO YA SOKA YA SPORTPESA CUP...

Mkurugenzi wa udhibiti na Utawala Sportpesa ABASS TARIMBA akisisitiza jambo wakati alipozungumza na waandishi wa habari kutangaza rasmi kuanza kwa mashindano ya Sportpesa 2019 yanayoanza Januari 22 ...
 Afisa Masoko na Maudhui wa Multichoice Tanzania Shumbana Walwa 'Shuu" akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa maandalizi ya michuano ya Kombe la SportPesa inayoaanza Januari 22 mwaka huu, Michuano hiyo itaonekana moja kwa moja kupitia DSTV katika kifurushi cha Bomba....


RAJA CASABLANCA WAPANGIWA TIMU MBILI ZA MOROCCO KUNDI A KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA


MABINGWA watetezi, Raja Club Athletic, maarufu kama Raja Casablanca wamepangwa pamoja na wapinzani wao wa Morocco, RS Berkane na Hassania Agadir kwenye Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika droo iliyopangwa mjini Cairo, Misri leo ikiongozwa na mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Cameroon, Patrick Mboma pamoja na Katibu Msaidizi wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Anthony Baffoe timu nyingine katika kundi hilo ni mabingwa wa Kongo, AS Otoho. 
Kukutana kwa timu tatu za Morocco kwenye hilo, kunakumbushia michuano ya mwaka 2012, wakati timu tatu za Sudan; Al Merreikh, Al Hilal na Ahly Shendi zilipopangwa kundi moja pai, huku timu nyingine kwenye kundi lao ikiwa ni Interclube ya Angola.
Raja Casablanca imepangwa Kundi A pamoja na RS Berkane na Hassania Agadir Kombe la Shirikisho Afrika

Timu mbili za Tunisia, Etoile du Sahel na CS Sfaxien zimekutanishwa Kundi B pamoja na Enugu Rangers ya Nigeria na Salitas ya Burkina Faso. 
Timu nyingine mbili za Zambia, Zesco na Nkana FC zimepangwa pamoja katika Kundi C Kombe la Shirikisho Afrika baada ya droo iliyofanyika leo makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mjini Cairo, Misri.
Pamoja na Zesco na Nkana FC, klabu anayochezea beki Mtanzania, Hassan Ramadhani Kessy, timu nyingine katika kundi hilo ni Al Hilal ya Sudan na Asante Kotoko ya Ghana.
Mabingwa mara tano Afrika, Zamalek ya Misri wamepangwa Kundi D pamoja na mabingwa wa Kenya, Gor Mahia, Petro Atletico ya Angola na NA Hussein Dey ya Algeria.

MAKUNDI YOTE KOMBE LA SHIRIKISHO:
Kundi A – Hassania Agadir (Morocco), AS Otoho (Kongo), RS Berkane (Morocco), Raja (Morocco)
Kundi B – Etoile du Sahel (Tunisia), Rangers (Nigeria), Salitas (Burkina Faso), CS Sfaxien (Tunisia)
Kundi C – Zesco (Zambia), Al Hilal (Sudan), Asante Kotoko (Ghana), Nkana (Zambia)
Kundi D – Gor Mahia (Kenya), NA Hussein Dey (Algeria), Petro Atletico (Angola), Zamalek (Misri)

KESSY NA NKANA YAKE KUNDI MOJA NA ZESCO, AL HILAL NA ASANTE KOTOKO SHIRIKISHO


TIMU za Zambia, Zesco na Nkana FC zimepangwa pamoja katika Kundi C Kombe la Shirikisho Afrika baada ya droo iliyofanyika leo makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mjini Cairo, Misri.

Pamoja na Zesco na Nkana FC, klabu anayochezea beki Mtanzania, Hassan Ramadhani Kessy, timu nyingine katika kundi hilo ni Al Hilal ya Sudan na Asante Kotoko ya Ghana.

Mabingwa watetezi, Raja Club Athletic wamepangwa pamoja na wapinzani wao wa Morocco, RS Berkane na Hassania Agadir kwenye Kundi A, huku timu nyingine katika kundi hilo wakiwa ni mabingwa wa Kongo, AS Otoho. 

Kukutana kwa timu tatu za Morocco kwenye hilo, kunakumbushia michuano ya mwaka 2012, wakati timu tatu za Sudan; Al Merreikh, Al Hilal na Ahly Shendi zilipopangwa kundi moja pai, huku timu nyingine kwenye kundi lao ikiwa ni Interclube ya Angola.

Hassan Kessy, wa kwanza kushoto walioinama amepangwa kundi moja na Zesco, Al Hilal na Asante Kotoko

Katika droo hiyo ambayo mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Cameroon, Patrick Mboma alisaidiana na Katibu Msaidizi wa CAF, Anthony Baffoe kupanga makundi, timu mbili za Tunisia, Etoile du Sahel na CS Sfaxien zimekutanishwa Kundi B pamoja na Enugu Rangers ya Nigeria na Salitas ya Burkina Faso.
Mabingwa mara tano Afrika, Zamalek ya Misri wamepangwa Kundi D pamoja na mabingwa wa Kenya, Gor Mahia, Petro Atletico ya Angola na NA Hussein Dey ya Algeria.

MAKUNDI YOTE KOMBE LA SHIRIKISHO:
Kundi A – Hassania Agadir (Morocco), AS Otoho (Kongo), RS Berkane (Morocco), Raja (Morocco)
Kundi B – Etoile du Sahel (Tunisia), Rangers (Nigeria), Salitas (Burkina Faso), CS Sfaxien (Tunisia)
Kundi C – Zesco (Zambia), Al Hilal (Sudan), Asante Kotoko (Ghana), Nkana (Zambia)
Kundi D – Gor Mahia (Kenya), NA Hussein Dey (Algeria), Petro Atletico (Angola), Zamalek (Misri)


KWA MSAADA WA MTANDAO WA BIN ZUBEIRY....

BODI YA WAKUREGENZI DAWASA YAWATAKA WAFANYAKAZI DAWASA WAWE WAADILIFU

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakipewa maelezo juu ya mfumo wa usambazaji wa maji kutoka katika tanki la Makongo jijini Dar es Salaam. Bodi hiyo inafanya ziara ya siku tatu ili kuweza kujifunza na kujionea jinsi mifumo ya usambazaji wa maji kwa jiji la Dar es Salaam na Pwani. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
 Mashine zilizofungwa katika tanki la makongo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakionyeshwa mtambo wa kuendeshea maji. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Wakiangalia mfumo wa Tenki la SalaSala jijini Dar es Salaam ikiwa ni ziara yao ya kujifunza masual mbali mbali ya maji.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi  wakiwa wamewasili kituo cha mtambo wa Ruvu chini- eneo la Bagamoyo - Pwani. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakiongea na wafanyakazi wa DAWASA kituo cha mtambo wa Ruvu chini- eneo la Bagamoyo - Pwani. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakiongea wakiangalia zoezi la kutandika mabomba ili kuwagawia maji wakazi wa Goba -Kizudi jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASA, Injinia Aron Joseph akiwaonyesha Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange jinsi maji yanavyovunwa katika Mtambo wa Ruvu Chini - eneo la Bagamoyo - Pwani.
Wakikagua eneo la mto Ruvu chini...
Mkurugenzi wa uzalishaji na usambazaji maji wa DAWASA, Injinia Aron Joseph akiwaonyesha Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (kwanza kulia) pampu za kuvuta maji.
Meneja wa DAWASA ofisi ya Bagamoyo, Alexander Ng'wandu akitoa maelezo machache mbele ya Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange mara baada ya kutembelea ofisi hizo zilizopo mjini Bagamoyo - Pwani.
Meneja wa DAWASA ofisi ya Bagamoyo, Alexander Ng'wandu akitoa maelezo machache mbele ya Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA iliyoongozwa na Mwenyekiti wao Jenerali Mstaafu Davis mara baada ya kutembelea tenki  la maji la Bagamoyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange pamoja na wajumbe wa bodi wakiongea na wanahabari mara baada ya kumaliza kutembelea kituo cha mtambo wa Ruvu chini- eneo la Bagamoyo - Pwani.
JENERALI MWAMUNYANGE ATEMBELEA MTAMBO WA RUVU CHINI NaCathbert Kajuna - Kajunason/MMG. Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na majitaka Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA) imewataka wafanyakazi wa DAWASA kuendelea kuwa waadilifu katika kazi zao ili kuweza kuwapa huduma bora wananchi wa Dar es Salaam na Pwani. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi mara baada ya kutembelea mtambo wa uzalishaji maji wa Ruvu Chini na kuongea na wafanyakazi wa DAWASA wa kituo hicho. Jenerali Mstaafu Mwamunyange amefurahishwa na utunzaji wa mazingira katika eneo la mto Ruvu ikiwa ndio chanzo kikubwa kinachozalisha maji kwa asilimia 88 katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Akiwa katika ziara yake ya siku ya pili, Jenerali mstaafu Mwamunyange ametembelea mtambo huo ikiwa ni mara ya kwanza toka achaguliwe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo. "Nimejifunza mambo mengi hata wenzangu wamekili kuna mambo mengi tulikuwa hatuyafahamu hakika sasa tutakuwa watendaji wazuri kwa kutambua kile tunachokisimamia," Amesema Jenerali Mstaafu Mwamunyange. Amesema jitihada kubwa za serikali zinafanyika kuhakikisha wananchi wote wanapata maji hususani kwenye maeneo yaliyokuwa hayana maji kwa kipindi chote kikubwa wananchi wawe wavumilivu kwakuwa DAWASA wanafanya kazi kuwapelekea maji. Baada ya kuwasili katika mtambo huo walipata fursa ya kuzungumza na wafanyakazi wa mtambo huo na kuwataka wafanye kazi kwa juhudi kubwa ili kutimiza adhma ya serikali ya kufikia asilimia 95 ya wananchi wote ifikapo 2020. Amesema, anafahamu kuna changamoto mbalimbali za wafanyakazi ila amewaahidi atazifanyia kazi atakapokutana na Sekretarieti ya DAWASA. Mbali na kutembelea mtambo wa Ruvu Chini, Bodi hiyo ilitembelea Tenki la maji la Changanyikeni, Busta pampu zilizofungwa Makongo kwa ajili kusukuma maji na maunganisho mapya Salasala. Ziara ya Bodi ya Wakurugenzi itaendelea kwenye maeneo mengine tofauti kwa ajili ya kujifunza na kuona namna DAWASA wanavyotoa huduma ya maji kwa wananchi wa Dar esSalaam na Pwani.

Thursday 3 January 2019

JAMHURI YAIGOMBEA AZAM FC ,KOMBE LA MAPINDUZI


Michuano ya Mapinduzi imenza kutimua vumbi huku kigogo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bar azam FC akianza kwa sare na timu ya Zanzibar ya Jamhuri

Mechi hiyo iliyokuwa na upinzani kwa pande zote mbili, ilishuhudiwa Azam FC ikianza kuandika bao la uongozi dakika ya 28, lililofungwa na kiungo mshambuliaji, Tafadzwa Kutinyu, kwa mkwaju wa penalti uliotokana na Emmanuel Balele, kuunawa mpira wakati akiokoa shuti la mfungaji wa bao hilo.

Jamhuri iliyocheza kwa nidhamu kubwa kwenye eneo la ulinzi hadi kufanikiwa kuwabana washambuliaji wa Azam FC, ilipata bao la kusawazisha dakika ya 66 lililofungwa na Abdul Ramadhan, bao lililowafanya kuambulia pointi hiyo moja.

Matokeo hayo yanaifanya Azam FC kuhitaji matokeo mazuri kwenye mechi zake tatu zilizobakia za hatua ya makundi, ikianza na Yanga Jumamosi hii, mchezo unaofuatia utakaofanyika Uwanja wa Amaan saa 2.15 usiku.

LUKAKU AGUSA MPIRA WA KWANZA NA KUFUNGA MAN UNITED IKISHINDA KWA MABAO 2-0





 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube