BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Wednesday, April 09, 2025

Tuesday, 6 February 2018

OKWI MAMBO YAKE SAFI, YUKO TAYARI KUIVAA AZAM FC...


Mshambuliaji Emmanuel Okwi ana nafasi ya kuwa katika kikosi cha Simba kitakachoivaa Azam FC katika mechi ya Ligi Kuu Bara, kesho.

Simba itakuwa mwenyeji wa Azam FC katika mechi hiyo huku ikiwa na matumaini ya kumtumia Okwi ambaye ni kinara wa mabao Ligi Kuu Bara kwa sasa akiwa na mabao 12.

Okwi aliumia baada ya kupigwa kwa makusudi na beki wa Ruvu Shooting katika mechi iliyopita na kulazimika kutolewa nje kwa ajili ya matibabu na hakurejea kwa kuwa alikuwa akipata shida.

Lakini Okwi ameonekana kupata nafuu haraka na aliungana na wenzake kambini tokea juzi na kuungana nao katika mazoezi.

Raia huyo wa Uganda aliikosa mechi ya kwanza kati ya Simba dhidi ya Azam FC kwenye Uwanja wa Azam Complex na kumalizika kwa sare ya bila bao.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube