BREAKING

Friday 16 February 2018

UEFA NDOGO ARSENAL WAPO MOTO, BATSHUAYI ........


 Michy Batshuayi ameendelea kufanya vema huku akiendelea kupachika mabao akiwa na kikosi chake kipya cha Borussia Dortmund.

Batshuay amefunga mabao mawili katika michuano ya Kombe la Europa wakati Dortmund iliposhinda kwa mabao 3-2 dhidi ya Atalanta ya Italia katika michuano ya Eurola League.

Mshambuliaji huyu amejiunga na Dortmund akitokea Chelsea ambayo ilimtoa ili kumpisha Olviere Giroud aliyekuwa anatokea Arsenal.






MSD YATUNUKIWA ITHIBATI YA JUU YA UBORA



BOHARI ya Dawa (MSD) imeendelea kukidhi viwango vya ubora vya kimataifa katika mfumo wa ununuzi, utunzaji na usambazaji dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara (Supply Chain Management) na kupata Ithibati ya Kimataifa ya ubora ya daraja la juu inayojulikana kama ISO 9001:2015 ambayo itadumu kwa miaka mitatu (2018 - 2020).

Hatua hiyo imekuja baada ya ukaguzi wa ubora wa huduma zinazotolewa na MSD uliofanywa na kampuni ya Kimataifa ya ACM LIMITED mweziAgosti 2017, na kudhihirisha kuwa huduma zake zinafuata miongozoya ya juu ya kimataifa katika utoaji wa huduma za mnyororo wa ugavi.

Akizungumzia hatua hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Bwana Laurean Rugambwa Bwanakunu amesema kuwa hatua hiyo ya kupata ithibati ya juu ya Ubora ya Kimataifa imethibitisha umahiri wa MSD na imeongeza chachu ya utendaji, ubunifu na kuboresha masuala yote yanayo husiana na mnyororo wa ugavi ilikuwapa wananchi huduma bora, zenye viwango, bei nafuu na kuwafikishia kwa wakati.

Bwanakunu ameongeza kuwa Ithibati hiyo inaonesha dhahiri ubora wa mfumo wa ugaviwa MSD  kwa wateja na wananchi kwa ujumla, na kueleza kuwa huduma za MSD zinaendelea kuboreshwa zaidi kwani taasisi hiyo iko katika kipindi cha maboresho ya kiutendaji kupitia mpango mkakati wake wamwaka 2017 - 2020. 

Mara ya kwanza MSD ilipataIthibatiya kimataifa mwaka 2013 (ISO 9001:2008) baada ya kukidhi matakwa ya ubora kwa huduma zake za Ununuzi, tunzaji na Usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara na iliweza kuishikilia  ithibati hiyo kwa miaka yote bila kunyanganywa, kutokana na kuonekana kuendelea kukidhi viwango vya ubora kila walipokaguliwa. 

MSD imekuwa  miongoni mwa taasisi za kwanza nchinikupataithibatiyauborayakiwango cha ISO 9001:2015 kutokakiwango cha ISO 9001:2008 na imethibitisha umahiri wa utendaji wake.

Wednesday 14 February 2018

RAIS MSTAAFU MKAPA AONGOZA HARAMBEE YA KUCHANGIA MFUKO WA UDHAMINI WA KUDHIBITI UKIMWI


Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akihutubia wakati akiongoza harambee ya kuchangia Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Serena Dar es Salaam jana usiku.
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama akihutubia katika harambee hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi,Bw.  Godfrey Simbeye akihutubia.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko akihutubia.
Wasanii wakitoa Burudani katika harambee hiyo
Wadau wakiwa kwenye harambee hiyo.
Makofi yakipigwa meza kuu. Kutoka kushoto ni Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi,  Bw. Godfrey Simbeye na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mgodi wa Geita Gold Mine (GGM), Bw. Tenga B. Tenga.
Wadau wakiwa kwenye harambee hiyo.
Harambee ikiendelea.
Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa akitoa zawadi ya picha iliyonunuliwa kwa sh. milioni moja katika harambee hiyo.
Rais Mkapa akimkabidhi picha  Salama Mussa kutoka Benki ya NBC baada ya kuinunua katika harambee hiyo. Kulia ni Waziri Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama na wa pili kushoto ni Mdau Teddy Mapunda mratibu wa harambee hiyo.
Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa akimkabidhi picha Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Alvaro Rodriguez baada ya kuinunua katika harambee hiyo.
Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa akimkabidhi picha ya simba Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Hoteli ya Serena, Bw. Seraphin Lusala baada ya kuinunua kwenye harambee hiyo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mgodi wa Geita Gold Mine (GGM),  Bw. Tenga B. Tenga akimkabidhi Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa mfano wa hundi yenye thamani ya sh.milioni 100 zilizo tolewa na mgodi huo kuchangia mfuko huo.


Na Dotto Mwaibale

RAIS Mstaafu Benjamin Mkapa amewataka wadau mbalimbali na wananchi kuendelea kuchangia Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo nchini ambapo zaidi ya sh.milioni 200 zilipatikana.

Mkapa alitoa ombi hilo wakati akiongoza harambee ya kuchangia mfuko huo iliyofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, wawakilishi wa mashirika ya nje na ndani pamoja na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.

"Ni wajibu kwa kila mwananchi na wadau mbalimbali kuendelea kuchangia mfuko huu ili kusaidia mapambano ya Ukimwi hapa nchini na kuwa mapmbano hayo si ya mtu mmoja" alisema Mkapa. 

Katika hatua nyingine Rais Mstaafu Mkapa ameiomba Serikali kuendelea kutenga fedha za Ukimwi katika bajeti zake.

Akizungumza katika harambee hiyo Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama alisema kwamba Serikali itaendelea kusimamia Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) katika matumizi ya  fedha hizo.

Mhagama alisema asilimia 60 ya fedha hizo zitatumika kununulia madawa, asilimia 25 itatumika katika kutoa huduma za kinga pamoja na kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi mapya ya Ukimwi na asilimia 15 zitatumika  kwa ajili ya uwezeshaji na ufuatiliaji wa programu za Ukimwi.

Mhagama aliongeza kuwa matumizi ya dawa za kufubaza VVU kwa wanawake ni asilimia 92.9 wakati wanaume ni 86.1 na kuwa katika tisini ya tatu kati ya watu wanaoishi na VVU wenye umri wa miaka 15-64 ambao wametoa taarifa kuwa wanatumia dawa za kufubaza VVU asilimia 87.7 ya watu hao inaonyesha kiasi cha VVU kimefubazwa wanawake ni asilimia 89.2 na wanaume ni asilimia 84.

Alisema utafiti huo pia umeonyesha kuwa maambukizo mapya ya VVU (HIV incidence) kwa mwaka kwa watu wenye umri wa miaka 15-64 Tanzania Bara ni asilimia 0.29 ambayo ni sawa na watu 81,000.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko huo, Bw. Godfrey Simbeye alisema sekta binafsi imeunga mkono kwa kiasi kikubwa katika kuchangia mfuko huo na kuwa hakutakuwa na matumizi mabaya ya fedha hizo na zitakwenda kutumika kwa kile kilichokusudiwa.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko alimshukuru Rais Mstaafu Mkapa kwa kukubali kushiriki kuongoza harambee hiyo na kueleza kuwa Tacaids imekuwa ikiendesha harambee mbalimbali pamoja na kuandaa mashindano ya michezo na viingilio vyake vimekuwa vikiingia katika mfuko huo.







TOTTENHAM WAIKOMALIA JUVENTUS, UGENINI KATIKA MICHUANO YA UEFA, YATOKA SARE YA BAO 2-2








UKWAA LA NISHATI TANZANIA KUTOA SEMINA KWA WABUNGE



Na Mwandishi Wetu

JUKWAA la Nishati Tanzania linatarajia kutoa semina kwa wabunge ili wapate uelewa wa nishati na changamoto zake, watakapokuwa wanajibu maswali ama kuuliza wafanye hivyo kwa manufaa ya taifa.

Mratibu wa Jukwaa hilo nchini ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Hudson Nkotagu alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu shughuli wanazozifanya.

Profesa Nkotagu alisema wanaamini wabunge wakipata uelewa kuhusu nishati pale watakapokuwa wakijadili masuala hayo bungeni watakuwa na uelewa mpana, na maamuzi yake yatakuwa kwa manufaa ya taifa.

Pia alisema semina hizo zitatolewa kwa viongozi wakuu, watendaji wa serikali kutoka sekta za viwanda, mazingira, serikali za mitaa, wawekezaji pamoja na wafanya biashara mbalimbali.

Alisisitiza kuwa wananchi wengi hawana uelewa wa nishati kwamba kuna za aina mbili, aina ya kwanza inatokana na vyanzo vya nishata ambavyo vikitumika vinapoisha havirudi tena mfano gesi, mafuta, mkaa wa mawe pamoja na urani.

Na aina nyingine ni ile inayotokana na vitu ambavyo vinajiendeleza vyenyewe kiasili kwa mfano nishati ya sola, upepo, maji, mawimbi ya bahari na kuni.

“Nishati hizi zinajiendeleza kiasili. Kwa bahati nzuri zote tunazo katika nchi yetu. Tanzania imejaliwa kuwa na vyanzo vyote vya nishati, vinahitajika tu kuendelezwa,” alisema.

Alisema jukwaa hilo linashirikisha UDSM, Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST), pamoja na vyuo vikuu vine kutoka nchini Uholanzi ambavyo ni Twente, Ultreacht, Hanze na Delft.

Thursday 8 February 2018

TANESCO SUMBAWANGA YAPOKEA JENERETA YA KUZALISHA UMEME MEGAWATI 10


  
KITUO cha kufua umeme mkoani Rukwa kimepata jenereta  ya kufua umeme yenye uwezo  wakuzalisha MegawatI 10 zitakazoimarisha uzalishaji wa umeme mkoani humo.
Akizungumzia ujio wa jenereta hiyo, Meneja wa TANESCO Mkoani Rukwa Bw.Herini Muhina, alisema, hali ya uzalishaji umeme itakuwa bora zaidi na hivyo kufanya upatikanaji wa umeme katika wilaya za Sumbawanga, Laila, Kalambo na Nkasi kuwa bora zaidi.
“Nimatumaini yetu kuwa ongezeko hilo la umeme, litasaidia kwenda sambamba na mipango ya serikali ya kujenga uchumi wa viwanda kwani umeme wa uhakika utakuwepo na hivyo kufanya Mkoa wa Rukwa kuwa sehemu nzuri ya kuwekeza kwenye sekta hiyo ya viwanda.” Alitoa hakikisho Bw. Muhidin.

  Kaimu Meneja Mkuu Rasilimali Watu wa TANESCO Makao Makuu, Bw. Nathan Daimon (watatu kushoto), akipta maelezo kutoka kwa mdhibiti na mwendeshaji mifumo ya umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kituo cha Sumbawanga Mkoani Rukwa Bw.Halfan R. Seba  kuhusu jenereta ujio wa jenereta yenye uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 10 kwenye kituo hicho.

Bw. Daimon akipewa maelezo zaidi ya uendeshaji shughuli za TANESCO mkoani Rukwa.
 

 

Tuesday 6 February 2018

POLEPOLE AMNADI MTULIA KWA KISHINDO KATIKA KATA YA MUZIMUNI, MAGOMENI JIJINI DAR ES SALAAM, LEO


 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akitema cheche wakati akimnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akimnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akiingia kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Wananchi na wana CCM wakitimua vumbi kumlaki Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole , alipowasili kwenye viwanja vya Mtambani, kumnadi mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM katika Jimbo la Kinondoni  Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akimsalimia Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni baada ya kuwasili kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia (wa pili kushoto) katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni katibu wa CCm mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akimsalimia mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Kamba baada ya kuwasili kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole na viongozi wengine wa meza kuu wakishangilia baada ya kuwasili, kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akisaini kitabu cha wageni baada ya kuketi
 Mwenyekiti wa zamani wa Wilaya ya Kinondoni Ndugu Londa akizungumza baada ya kukaribishwa jukwaani kusalimia
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Kate kamba akimkaribisha Ndugu Polepole jukwaani baada ya kuhutubia
 Ndugu Polepole akitamba jukwaani kabla ya kumwita jukwaani Ndugu Mtulia kumnadi
 Polepole akimnadi Mtulia kwa wananchi
 Mtulia na Polepole wakionyesha furaha jukwaani wakati wakishangiliwa na wananchi
 "Ukishachaguliwa hawa wananchi wasaidie sana kutatua matatizo yao, maana wanakuamini na wanaaiamini CCM ndiyo maana watakuchagua" akasema Polepole kumwambia Mtulia (kushoto)

 " Na utatutuzi wa matatizo ya wanancho kwako utakuwa rahisi ukitumia Ilani hii ya CCM, maana kila kitu kimo humu" akaongeza Ndugu Polepole kumwambia Ndugu Mtulia kabla ya kumkabidhi kitabu hicho cha Ilani ya CCM ya 2015-2020
 Wananchi na wana CCM wakilipuka kwa nderemo wakati Ndugu Polepole akimnadi Mtulia
 Ndugu Polepole akimpongeza Mtulia baada ya kumkabidhi Ilani hiyo
 Kisha akamuasa zaidi
 Wananchi wakizidi kushangilia kwa vifijo
 Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia akiomba kura katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube