BREAKING

Friday 19 January 2018

NAIBU WAZIRI WA MADINI MHE BITEKO AWATAKA WACHIMBAJI WADOGO KUTAMBUA UMUHIMU WA KULIPA KODI

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza jambo wakati wa mkutano na wachimbaji wa madini ya Jasi na Chumvi Mkoani Mtwara, Leo 19 Januari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Wachimbaji wa madini ya Jasi na Chumvi Mkoani Mtwara wakimsikiliza Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko wakati wa Mkutano wa pamoja na wachimbaji hao kwenye ofisi za Madini Kanda ya kusini, Leo 19 Januari 2018.
Mwenyekiti wa wachimbaji wadogo Kanda ya kusini Ndg Peter Ludovick akieleza kero za wachimbaji mbele ya Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko wakati wa mkutano na wachimbaji wadogo, Leo 19 Januyari 2018.

Na Mathias Canal, Mtwara

Wizara ya Madini imesisitiza wachimbaji wadogo na wakubwa nchini kutambua umuhimu wa ulipaji kodi kwa kila wanachozalisha kwani itasaidia kuongeza pato la Taifa kwa kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi ikiwemo ukarabati wa miundombinu, Ujenzi na uimarishaji Wa sekta ya afya, elimu, Sekta ya umeme na sekta ya maji.

Akizungumza Mkoani Mtwara wakati wa mkutano na wachimbaji wa madini ya Jasi na Chumvi Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amesema kuwa jamii bado haina elimu ya kutosha juu ya ulipaji kodi hivyo ofisi za madini nchini zinapaswa kuongeza msukumo Wa utoaji elimu juu ya ulipaji kodi na utunzaji wa kumbukumbuku za shughuli za uvunaji Madini kwa kila mahali kwenye leseni.

Mhe Biteko alisema kuwa wachimbaji wadogo kote nchini wanapaswa kutambua kuwa hawatakiwi kusalia kukwepa kodi badala yake wanapaswa kutoka kwenye uchuuzi na hatimaye kuhamia kwenye ufanyabiashara na kuhifadhi taarifa zote kwa mujibu wa kanuni kwa kipindi cha miaka 5.

Alisema kuwa mtu yeyote anapoitwa mfanyabiashara anatambulika katika jamii na serikali kwa ujumla wake hivyo kigezo kikubwa na muhimu kwa mfanyabiashara ni kulipa kodi kwa mujibu Wa kanuni, sheria na taratibu.

Akizungumza kwa msisitizo Mhe Biteko alisema kuwa watanzania wamempata Mhe Dkt John Pombe Magufuli kuongoza Taifa akiwa Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania katika kipindi cha miaka mitano hivyo wanapaswa kuunga mkono juhudi za utendaji wake kwa kulipa kodi kwa manufaa ya jamii nzima.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Wa Madini ameupongeza uongozi Wa Ofisi ya Madini Kanda ya Mtwara kwa ushirikiano mzuri na wachimbaji jambo ambalo limeimarisha utendaji wao pasina malalamiko dhidi ya serikali.

Kwa upande wake Mwenyekiti Wa Chama Cha wachimbaji Mkoa Wa Mtwara Ndg Festo Balegele akizungumza wakati Wa mkutano huo alimsihi Naibu Waziri wa Madini kutilia mkazo uongezaji thamani wa chumvi inayozalishwa nchini kwa kuikausha (Drying) na kuisaga (Grinding) sambamba na kuongeza Madini joto kwani itapelekea serikali kuokoa fedha nyingi za kigeni zinazotumiwa na serikali kuagiza chumvi nje ya nchi.

Alisema kuwa kila mwaka jumla ya tani 350 za chumvi huagizwa nje ya nchi ambapo ikiwasili nchini inauzwa kwa shilingi 500 kwa gramu 500 sawa na shilingi 50,000 kwa kilo 50 kiasi ambacho ni kikubwa Mara tano ya gharama za chumvi inayozalishwa nchini kwani inauzwa kwa shilingi 5000 kwa kilo 50.

Alisema kuwa chumvi inayoagizwa nje ya nchi ni kiasi cha Tani 350,000 kila mwaka huku akisisitiza kuwa serikali ingetilia mkazo na kuboresha miundombinu nchini ingerahisisha upatikanaji wa chumvi nyingi nchini ambayo inauzwa kwa kiasi kidogo chenye uwezo wa kukidhi mahitaji ya watanzania.

SHONZA:HATUTORUDI NYUMA KATIKA KUSIMAMIA MAADILI

  Naibu Wazir wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akizungumza viongozi wa taasisi ya Malezi Bora Foundation inayoundwa na wasanii wa filamu nchini (hawapo pichani) walipomtembelea ofisini kwake leo mjini Dododma. Kulia ni mtunza fedha wa taasisi hiyo Bi. Susan Natasha.

  Naibu Wazir wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wakwanza kushoto) akizungumza na viongozi wa taasisi ya Malezi Bora Foundation inayoundwa na wasanii wa filamu nchini walipomtembelea ofisini kwake leo mjini Dododma. Kutoka kushoto ni Bi. Susan Natasha, Bi. Shamsa Danga, Bi. Heriety Chumira na Bi. Farida Sabu.

  Naibu Wazir wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (waatatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa taasisi ya Malezi Bora Foundation inayoundwa na wasanii wa filamu nchini walipomtembelea ofisini kwake leo mjini Dodoma. Kutoka kushoto ni Bi. Heriety Chumira, Bi. Susan Natasha, Bi. Shamsa Danga, Bi. Farida Sabu na Bi. Pili Lwey.


Mtunza fedha wa taasisi ya Malezi Bora Foundation Bi. Susan Natasha Humba (kulia) akimfanunulia jambo Naibu Wazir wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza  kushoto) wakati viongozi wa taasisi hiyo walipomtembea Naibu Waziri huyo ofisini kwake leo mjini Dodoma.
(PICHA NA OCTAVIANA F. KIMARIO-WHUSM)
WHUSM

Wednesday 17 January 2018

MBUNGE RITTA KABATI ATOA MSAADA WA MAFUTA MAALUM YA KUPAKA KWA WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI MKOA WA IRINGA

Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi box la mafuta hayo katibu wa Tas mkoa wa Iringa bwana Leo Sambala katika ukumbi wa halmashauri ya manispaa ya Iringa  
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi boxi  la mafuta hayo katibu wa Mufindi bwana Andrea Kihwelo
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi  mafuta hayo moja ya walemavu wa ngozi
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akimkabidhi boxi la mafuta hayo mwenyekiti wa wilaya ya Kilolo ndugu Anna Masasi 

JAMII imetakiwa kuwalea, kuwatunza na kuwajali watu wenye ulemavu wa ngozi albino kwa kuhakikisha kwamba wanaishi katika mazingira mazuri, yenye usalama na sio kuwanyanyapaa pale wanapohitaji mahitaji yao ya msingi.

Aidha Chama cha walemavu wa ngozi (TAS) mkoa wa Iringa kimeshauriwa kuendelea kushirikiana na serikali, ili walemavu hao pia waweze kupata elimu juu ya afya ya usalama wa ngozi pamoja na kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili katika maisha yao.


Hayo yalisemwa na mbunge wa viti maalum Ritta Kabati wakati alipokuwa akitoa msaada wa mafuta maalum ya kupaka watu wenye ulemavu wa ngozi albino katika hafla fupi iliyohudhuriwa na walemavu hao ambayo ilifanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya manispaa ya Iringa


“Nampongeza Mwenyekiti wa TAS mkao wa Iringa kwa jitihada zake alizozifanya juu ya namna ya kupata mafuta haya, kama chama endeleeni kuwa wabunifu namna ya kulisaidia kundi hili tete la walemavu kwa kuwalea na kuwatunza katika mazingira mazuri”, alisisitiza mbunge Kabati 

Vilevile Kabati  aliongeza kwa kuwataka viongozi wa chama hicho kutumia fursa waliyopewa na wanachama wao, kuhakikisha kwamba wana ainisha matatizo waliyonayo walemavu wa mkoa wa Iringa na kuyafikisha katika ofisi za serikali ili yaweze kufanyiwa kazi.

Kabati alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inahakikisha kuwa inafakiwa kutatua matatizo ya wananchi wa ikisha maisha yao yanaboreshwa.

“Hata haya mafuta yamenunuliwa na serikali kupitia wizara ya afya ,maendeleo ya jamii ,jinsia ,wazee na watoto na yanasambazwa nchi nzima hivyo sisi viongozi kazi yetu ni kwasaidia usafiri walememavu hawa” alisema Kabati


Awali akitoa maelezo mafupi juu ya changamoto zinazowakabili albino katika mkoa wa Iringa huo, Mwenyekiti wao Hellen Machibya  alisema kuwa wanashindwa kuwafikia wanachama wake kwa urahisi kutokana na kukosa usafiri na rasilimali fedha, kwa ajili ya kuwatimizia mahitaji yao ya msingi. 

Machibya alifafanua kuwa kukosekana kwa fedha kunakwamisha utendaji kazi na uendeshaji wa shughuli husika, hivyo wanaiomba serikali kuwaangalia kwa jicho la huruma kwa kutatua kero zinazowakabili ili kundi hilo tete liweze kusonga mbele kimaendeleo.

Machibya alisema kuwa kazi aliyoifanya mbunge huyo ni kuokoa maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa kuwa watakuwa wanajikinga na mionzi ya jua.

Machibya alisema kuwa watu wenye ulemavu wa ngozi wamekuwaathirika wakubwa wa ugonjwa wa kasa kutokana na ngozi zao kushambuliwa na jua na kusababisha kuiathiri ngozi hivyo msaada uliotolewa na serikali umeokoa sana maisha.

“Jamani sisi watu wenye ulemavu tunapenda sana kufanya kazi tatizo mionzi ya jua inatuathiri sana na kusababisha kushindwa kufanya kazi zetu kwa uwezo wetu hivyo tunaomba serikali na wadau kama mbunge Ritta Kabati waendelee kutusaidia maana mafuta haya dukani ni gharama sana hivyo watu wenye ulemavu wa ngozi hatuzimudu” Machibya

Lakini Chama cha walemavu wa ngozi (TAS) mkoa wa Iringa wamemshukuru mbunge wa viti maalum Ritta Kabati kwa kuwasidia kuwafikishia mafuta ya kujipaka mwilini kwa ajili ya kujikinga na mionzi ya jua ambayo imekuwa ikiwasababishia kupata ugonjwa wa kansa.

MNEC SALIM ASAS AMWAGA MAMILIONI YA FEDHA KATA YA KIHESA KWA AJILI YA MAENDELEO

 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas,diwani halali wa kata ya kihesa  Jully Sawani na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) manispaa ya Iringa wakifurahia kukabidhiwa kwa hati kwa diwani wa chama hicho tukio hilo lilifanika katika ofisi ya kata ya kihesa likihudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na mamia ya wananchi na wanachama wa chama hicho.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas,diwani halali wa kata ya kihesa  Jully Sawani wakizungumza na wananchi waliohudhulia tukio hilo
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas,diwani halali wa kata ya kihesa  Jully Sawani wakiwapokea wanachama wapya kutoka chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wa kata ya kihesa 
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas akiongea na wananchi walijitokeza kushudia tukia na kupewa cheti diwani wa kata hiyo Jully Sawani

KATA ya kihesa manispaa ya Iringa imeanza kupata neema ya mamilioni ya fedha za kimaendeleo mara baada ya kumpata diwani mpya kupitia chama cha mapinduzi (CCM) baada ya kupita bila kupigwa kutoka na vyama vingine vya siasa kutoweka wagombea.

Akikabidhiwa hati ya utambulisho wa kuwa ndio diwani halali wa kata ya kihesa,Jully Sawani alielezea mikakati ya kimaendeleo ya kata hiyo ambayo ataanza nayo ni kukarabati miundombinu ya barabara kwenye baadhi ya mitaa ya kata hiyo.

“Ukipita kwenye mitaa yetu utagundua kuwa mtaa kama mtaa wa mafifi miundombinu ya barabara sio nzuri kabisho akahidi kuwa ndani ya wiki hii atapeleka kata pila lianze kazi ya kuzikarabati bara bara hizo ili kurahisisha usafiri kwa wananchi wake kwa kuwa wamemtuma kufanya kazi” alisema Sawani

Sawani aliongeza kwa kusema kuwa amejianda kuhakikisha anatatua kero za wananchi kwa kushirikiana na serikali ya manispaa ya Iringa ambayo inatekeleza sera za chama cha mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 huku ikiwa na kauli mbiu inayosema kuwa hapa kazi tu.

“Naomba niseme ukweli wananchi wangu wote wa kata ya Kihesa sasa ni wakati wa kufanya kazi na sio mchezo mchezo mliokuwa mnaufanya nimeomba kuwa diwani kwa lengo la kuhakikisha kila mwananchi wa kata hii anafanya kazi kwa kuhakikisha kuwa familia yake haiwi masikini,ninasema kuwa kila ukilala hakikisha unaukataa umasikini kwa kuutamka wakati unalala tena kwa zaidi ya mara tisa hapo ndio utafanya kazi” alisema Sawani

Aidha Sawani alitoa kilio chake cha kwa kuomba msaada wa kimaendeleo kwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) MNEC Salim Asas ambapo alimwambia kuwa wananshida ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari ya Kihesa na kusaidiwa kumalizia ujenzi wa jingo la kibiashara ambalo lipo jirani na ofisi za kata ya hiyo.

“Mheshimiwa MNEC Salim Asas nipo hapa naomba utusidie msaada wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari ya Kihesa na jingo hili ambalo lipo mbele yetu unaliona linahitaji kumaliziwa ili kuweza kuongeza ajira kwa wananchi wa kata yangu hivyo naomba sana msaada wako kukamilisha hivi vyote kwa awamu hii ya kwanza” alisema Sawani

Akihutubia mamia ya wananchi walijitokeza katika hafla hiyo ya kukadhiwa cheti cha kuwa diwani wa kata hiyo Jully Sawani, MNEC Salim Asas alisema kuwa atatoa mifuko miambili ya saruji kwa ajili ya kutatua kero hiyo ya ujenzi wa madarasa katika shule ya sekondari Kihesa na kuahidi kuwa ataitembelea shule hiyo kujua changamoto nyingine.

“Leo naanza kwa kutoa mifuko miambili ya saruji lakini nitakuja hapo shule kujionea changamoto nyingine za shule hiyo ili niweze kuzitatua kabisa na kuwaacha wananfunzi wakisoma kwa uhuru kwa lengo la kukuza kizazi chenye elimu bora na kuja kusaidia taifa katika kuleta maendeleo wote tunajua kuwa bila elimu huwezi kupata maendeleo hivyo nitasaidia sana kwenye elimu” alisema Asas

Asas aliwakata viongozi wa kata hiyo kuandaa bajeti ya kumalizia jingo hilo ambalo litaongeza ajira kwa wananchi wa kata hiyo ambao kwa sasa hali zao za kiuchumi zimedolola hivyoa atafanya linalowezekana kuhakikisha kuwa wananchi wa kata hiyo wanabadili na kuacha kuishi kimazoea.

“kata ya Kihesa anayoijua yeye ni ile yenye vijana wengi wasio na ajira ambao kwa bahati mbaya wamekuwa wakishughulishwa kwenye siasa badala ya kuhamasishwa kufanya shughuli za maendeleo” Alisema Asas


Asas alisema vijembe na malumbano ya kisiasa katika kata hiyo yanatosha na akawataka vijana hao kuunda vikundi vya ujasiriamali vitakavyowawezesha kufikiwa kirahisi na mipango mbalimbali ya maendeleo 

KOMBE LA FA LEICESTER YAICHAPA FLEETWOOD 2-0 MUWASHI KELECHI IHEANACHO ANAPIGA MABAO TU, JAMIE VARDY NAYE ATUPIA













MHE BITEKO AITAKA STAMICO KUITHIBITISHIA SERIKALI KWANINI IENDELEE KUWEPO

Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akikagua mtambo wa uchongaji mashimo kwa ajili ya utafiti wakati alipotembelea Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akisitiza wakati wa kikao cha pamoja na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akisitiza wakati wa kikao cha pamoja na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akiwa katika picha ya  pamoja na Uongozi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.

Uongozi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) umetakiwa kutoa maelezo kwa serikali katika kipindi cha muda mfupi kueleza sababu za kuendelea kusalia kuwepo kwa shirika hilo kutokana na kukosa umakini katika utendaji.

Kauli ya kuchukizwa na utendaji wa Shirika hilo imetolewa Leo 16 Januari 2018 na Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko Wakati akizungumza na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika hilo Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam.

Mhe Biteko alisema kuwa serikali ilikuwa na makusudi mazuri kufuatia mabadiliko ya Sera za kiuchumi katika miaka ya 1980 kwa STAMICO kuwekwa kwenye orodha ya mashirika yanayotakiwa kubinafsishwa na hatimaye kubinafsishwa rasmi mwaka 1996 lakini katika kipindi chote cha utendaji hakuna msaada wowote ambao Shirika hilo limeipatia serikali zaidi ya kuingiza hasara maradufu.

Alisema kuwa pamoja na STAMICO kuwa na jukumu la kuendeleza migodi ya Madini na kufanya biashara za Madini ikiwemo mradi wa dhahabu wa STAMIGOLD uliopo Biharamlo Mkoani Kagera na Mgodi wa Makaa ya Mawe KABULO uliopo Mkoani Ruvuma lakini Taasisi hiyo imeshindwa kuendeleza migodi kwa ufanisi huku wachimbaji wadogo wakisalia kuwa katika uduni wa mbinu rafiki na tija katika utendaji kazi wao.

Alisema kuwa Shirika hilo linapaswa kutafakari kwa umakini utendaji wake kwani limeongeza hasara kwa serikali ya deni la shilingi Bilioni 1.77 hivyo serikali haiwezi kuendelea kusalia kuwa na Shirika linalozalisha madeni kuliko matokeo makubwa na faida.

Aliongeza kuwa wataalamu wote katika sekta ya Madini wanapaswa kutambua kuwa biashara ya Madini ni zaidi ya kutoa leseni hivyo watambue kuwa kuna kila sababu ya kuwa na matumizi bora ya mapato na kutazama namna bora ya kuifanya sekta ya Madini kuchangia asilimia 10% ya pato la Taifa.

Mhe Biteko alisema kuwa imani bila matendo ni uduni wa fikra hivyo kuwa na cheo kikubwa serikalini halafu uzalishaji ni mdogo ni kipimo halisi cha utendaji wa mazoea walionao watumishi wengi ambao wamekosa uzalendo na bidii katika utendaji kazi.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli imekusudia kusimamia vyema rasilimali za wananchi hivyo watendaji katika sekta mbalimbali wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kumsaidia Rais Magufuli katika kuteleleza adhma ya serikali.

Monday 15 January 2018

LIVERPOOL NI 'Unbelievable': WENYEWE WANACHEEKA....WAICHAPA MAN CITY 4-3





DC ALI HAPI AZIPONGEZA DAWASA NA DAWASCO KWA USIMAMIZI MZURI UTEKELEZAJI WA UJENZI WA MIRADI YA UBORESHAJI MAJI


 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Mhe., Ali Hapi, (katikati), akiteremka kutoka juu ya tenki kubwa la kuhifadhia maji linalojengwa huko Mabwepande nje kidogo ya jiji, wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya maji wilayani kwake Januari 13, 2018.
MKUU wa wilaya ya Kinondoni Mhe. Ali Hapi, amewataka wakandarasi wanaotekeleza ujenzi wa mradi wa uboreshaji wa huduma za ugawaji na usambazaji maji wilayani kwake kuongeza kasi ya kukamilisha mradi huo kama ambavyo mkataba unaelekeza.

Mhe. Hapi aliyasema hayo leo Januari 13, 2018 mwishoni mwa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundomnbinu hiyo inayohusisha matenki makubwa manne na vituo vinne vya kusukuma maji (Booster Stations) ikiwa ni pamoja na utandikaji  wa mabomba ya kusafirisha maji.

Mradi huo ambao unatekelezwa na Wizara ya Maji na Umwagiliaji kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka jijini Dar es Salaam, (DAWASA), ni sehemu ya mradi mkubwa wa uboreshaji wa huduma za ugawaji na usambazaji maji katika baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Pwani,  Dar es Salaam, sehemu ya mikoa ya Morogoro na Tanga na ulianza kutekelezwa mwezi Machi 2016.

“Mradi huu ulipaswa kuwa umekamilika Novemba mwaka jana, lakini hatua waliyofikia baadhi ya maeneo wako asilimia 80, mengine asilimia 75 na mengine asilimia 50, ahadi yao ni kwamba ndani ya kipindi kifupi kijacho wataweza kukamilisha mradi huu.” Alisema

Hata hivyo Mheshimiwa Hapi amepongeza usimamizi na ufuatiliaji wa karibu unaofanywa na mamlaka husika zinzosim amia mradi huo. “Niwapongeze DAWASA na DAWASCO kwa kazi nzuri ya kuhakikisha wanasimamia na kufuatilia utekelezaji wa mradi huu.” Alisema Mhe. Hapi.

Alitaja maeneo yatakayofaidika na mradi huu kuwa ni pamoja na wakazi wa Makongo, Changanyikeni, Salasala, Bunju, Mabwepande na Wazo.

“Mradi ukikamilika utaondoa kero ya maji katika wilaya yetu  kwa asilimia 95, kwa hivyo, hii nifaraja kubwa kwa wananchi wa Kinondonbi hususan katika maeneo nilkiyoyataja.” Alifafanua.

 Mhe. Hapi, akimsikiliza Mkandarasi,   Mhandisi P.G. Rajani wa kampuni ya WAPCOS limited ya India, alipotembelea sehemu ya ujenzi wa mtambo wa kusukuma maji huko Salasala jijini Dar es Salaam.

 Mhe. Hapi, akimsikiliza Mkandarasi,   Mhandisi P.G. Rajani(kulia) wa kampuni ya WAPCOS limited ya India, alipotembelea sehemu ya ujenzi wa tenki kubwa la kuhifadhia maji huko Salasala jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Modester Mushi kaimu mkurugenzi wa ufundi DAWASA.
 Mhe. Hapi na msafara wake wakipanda juu ya tanki linalojengwa.
 Mafundi wakiwa kazini huko Salasala.
 Mhe. Hapi akipokelewa na Meneja Uhusiano wa Jamii, DAWASA, Bi. NMelly Msuya, wakati akiwasili huko Makongo Juu, kuanza ziara ya kukagua miradi hiyo.
 Meneja Uhusiano wa Jamii, Bi. Nelly Msuya, (wapilia kushoto) na Afisa Uhusiano wa Jamii wa DAWASA, Bi. Mecky Mdakju, wakimsubiri Mkuu wa wilaya Mhe. Hapi, alipozuru eneo la Makongo Juu kukagua ujenzi wa kituo cha kusukuma maji.
 Mhe. Hapi, (kulia), akifurahia jambo na afisa kutoka DAWASCO, Bi.Judith Singinika(katikati), baada ya kutembelea eneo la ujenzi Bunju.
 Tenki kubwa likifunikwa huko Salasala.
 Mhe. Hapi, (kushoto), akiwa na Bi.Modester Mushi kaimu mkurugenzi wa ufundi DAWASA, (kulia) na Bi. Nelly Msuya, Meneja Uhusiano wa Jamii, DAWASA, walipotembelea ujenzi wa kituo cha kusukuma maji Bunju.
 Mkuu wa wilaya akizungumza na vibarua.

 Mkuu wa Wilaya Mhe. Hapi, akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa ziara hiyo, huko Mabwepande.
Bi.Mecky Mdaku, Afisa Uhusiano wa Jamii, DAWASA, akipanda juu ya tenki la Makongo Juu lililofikia asilimia 80 kukamilika

Wednesday 10 January 2018

AIBU SPIKA ATEMBELEA BOHARI YA DAWA (MSD)

 Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Bwana Laurean Bwanakunu, akizungumza na Naibu Spika, Tulia Akson alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja kutembelea MSD kuona shughuli mbalimbali za uhifadhi dawa na Vifaa tiba jijini Dar es Salaam jana.
 Hapa Naibu Spika, Tulia Akson akitembelea ghara la kuhifadhi dawa na vifaa tiba.
Naibu Spika akipata maelezo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Bwana Laurean Bwanakunu, akiagana na Naibu Spika, Tulia Akson baada ya kumaliza ziara hiyo ya kikazi.

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube