BREAKING

Monday 4 December 2017

WANACHAMA WA SIMBA WAMPA TIMU MO KIULAINIIII...AHAIDI MAKUBWA KATIKA KLABU HIYO


  
Baada ya Mfanyabiashara bilionea kijana zaidi Afrika, Mohammed 
Dewji kushinda zabuni ya kuchukua hisa hadi 50 asilimia katika klabu ya Simba, Mohammed Dewji aliingia ukumbini akiwa anasubiriwa kwa hamu na wanachama wa Simba.

Wanachama hao ndiyo waliopitisha uamuzi huo na kusubiri tume iliyokuwa inasimamia kupitia jaji mstaafu Mohayo kupitia mchakato na baadaye kutangaza.

Baada ya kutangazwa walishangilia kwa nguvu na baadaye Mo Dewji aliingia huku akishangiliwa kwa nguvu na baadaye akapewa nafasi ya kuzungumza na wanachama hao aliowashukuru na baadaye kuwaeleza nia yake na mipango yake ya uwekezaji.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube