BREAKING

Saturday 30 April 2016

CHAMA CHA WAKUNGA TANZANIA (TAMA) WATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI


DSC_2376Katibu Mkuu wa TAMA, Dkt Sebalda Reshabari (kushoto) akieleza jambo kwa wanahabari na watu mbalimbali (hawapo pichani) wakati wa mkutano huo kwa waandishi wa habari juu ya kufahamishwa shughuli za Wakunga. Kulia ni Bi. Felister Bwana kutoka UNPFA, Nchini Tanzania.
DSC_2381Mkutano huo ukiendelea...
DSC_2383 DSC_2389Baadhi ya maafisa kutoka taasisi za Wakunga na mambo ya Afya wakifuatilia mkutano huo.
DSC_2391Katibu Mkuu wa TAMA, Dkt Sebalda Reshabari akito mada katika mkutano huo..
DSC_2397DSC_2402Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mkutano huo
DSC_2408Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mkutano huoDSC_2409Katibu Mkuu wa TAMA, Dkt Sebalda Reshabari akitoa mada katika mkutano huo kwa wanahabari..
DSC_2436Mratibu wa TAMA, Bi. Martha Rimoy akitoa mada maalum kwa waandishi wa habari namna kazi na shughuli za Wakunga wanazofanya hapa nchini
DSC_2432
Afisa Mipango wa UNFPA, hapa nchini, Bi.Felista Bwana akitoa maelezo mafupi juu ya wakunga hapa nchini
DSC_2448Mratibu wa TAMA, Bi. Martha Rimoy akitoa mafunzo hayo katika mkutano huo kwa wanahabari
DSC_2464Baadhi ya wanahabari wakiwa katika mkutano huo
DSC_2479Bi. Felista Bwana akitoa mada katika mkutano huo
DSC_2467Katibu Mkuu wa TAMA, Dkt Sebalda Reshabari akifafanua maswali kwa wanahabari wakati mkutano huo..
DSC_2481
DSC_2426Picha ya pamoja baadhi ya wanahabari na wandaaji wa mkutano huo maaalum kwa wanahabari kuelekea siku ya Wakunga Duniani ambayo kilele chake ni hapo Mei 5 mwaka huu huku kwa Tanzania ikitarajiwa kufanyika kwenye viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam. 


Chama cha Wakunga Tanzania(TAMA) watoa mafunzo kwa wanahabari Nchini
Chama cha Wakunga Tanzania (Tanzania Midwives Association-TAMA) imefanya mkutano maalum wa kuhamasisha waandishi wa Habari kuhusu kazi za wakunga katika kuelekea siku ya Wakunga Dunia ifikapo hapo Mei 5 mwaka huu.
Katika mkutano huo uliofanyika jana Aprili 28, TAMA ilibainisha kuwa, wanahabari wengi wamekuwa wakichanganya habari za wakunga wataalam ambao wapo chini ya Chama hicho na wale wakunga wa jadi ambao hawana taalum pamoja na kiapo cha kufanya kazi hiyo kitu ambacho kinaleta usumbufu mkubwa kwa jamii.
Mratibu wa TAMA, Bi. Martha Rimoy katika mkutano huo, ameeleza kuwa, shughuli za Wakunga wataalam ni wale tu ambao wamesomea taaluma hiyo pamoja na kula kiapo katika kumsaidia Mama na Mtoto na na huyo ndiyo anaitwa Mkunga na si wale ambao hawajapata mafunzo wala kula kiapo.
Aidha, aliomba wanahabari na vyombo vya habari kuzipatia nafasi/Kipaumbele habari za Wakunga kwani zitaondoa woga kwa jamii iliyojenga Imani potofu kwa wakunga.
“Jamii imekuwa ikijenga Imani potofu namna ya Wakunga buka kujua mkunga huyo ni yupi. Tunaomba ifahamike Mkunga ni yule aliyepata mafunzo yake kitaalam na pia kula kiapo pamoja na kusajiliwa na taasisi husika kama ilivyo taratibu za Nchi.
Tuondoe Imani zingine kwa Wakunga pia tunawaomba wanahabari kuweza kutoa elumu ya kutosha kuhusiana na mambo ya Wakunga hasa wakunga wataalam ambao wamepatiwa mafunzo yote ya kuhakikisha wanamuokoa Mama na mtoto wakati wa uzazi” alieleza Bi. Martha Rimoy.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa TAMA, Dkt Sebalda Reshabari ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, ameeleza kuwa, Wakunga wataalam wanao wajibu
wa kumsaidia Mwanamke na mtoto katika kukabiliana na vifo vitokanavyo na Masuala ya Uzazi vinavyozidi kuwatesa akina mama wengi, hasa inapokuja wakati wa tendo la kujifungua.
Aidha, Dkt. Sebalda amebainisha kuwa, pamoja na Changamoto mbalimbali, vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka 5, imepungua kwa asilimia 81, huku akitaka muendelezo wa elimu utolewe kwa Jamii.
Kwa upande wake, Afisa Mipango wa Afya ya Mama na Uzazi wa Shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA)nchini, Bi. Felista Bwana ameelezea kuwa, upo umuhimu wa Mkunga mtalaam katika kuokoa Uhai wa Mama na mtoto kwani bila wao Dunia ingekuwa kwenye matatizo makubwa.
Siku ya Ukunga Duniani Inatarajiwa kuadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam, Mei 5 mwaka huu huku ikibeba ujumbe wa kauli mbinu ya “Wanawake na Watoto wachanga ni muhimili wa Ukunga”.
Aidha, mkutano huo ulieza changamoto wanazokabiliana nazo wakunga ni nyingi hivyo wameimba Serikali kuangalia namna ya kukabiliana nayo ili kila Mkunga kufanya kazi yake kwa uhuru na haki kwa dhama za sasa huku wakiomba jamii kuondoa dhana potofu dhidi yao pindi wawaonapo katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali zote.
Mkutano huo maalum wa TAMA, ulihusisha wanahabari mbalimbali kutoka katika vyombo vya Habari nchini ikiemo, Magazeti, Radio, Televisheni na magazeti ya mtandaoni.


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube