BREAKING

Thursday, 7 January 2021

MAISHA MAGIC BONGO YAZIDISHA UHONDO WA BURUDANI TAMTHILIYA MPYA ZA JUA KALI NA PAZIA ZA BAMBA KINOMA

Mambo ni bandika - bandua, paukwa – pakawa ndani ya chaneli maarufu ya Maisha Magic Bongo (MMB) ambapo imetangaza rasmi kuanza kwa tamthilia mbili kabambe za Pazia na Jua Kali, zitakazoanza kurushwa kuanzia Januari 2021 kwenye Chaneli ya MMB DStv 160.

 

Kiu ya mashabiki wa tamthilia za kibongo imepata dawa kwani tamthilia mpya ya Pazia imepikwa ikapikika huku ikisimamiwa na mzalishaji maarufu na kijana mtanzania Samwel Isike, ambaye pia ndiye aliyezalisha tamthilia iliyojizolea umaarufu mkubwa hapa nchini ya Sarafu.

 

Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo akimtambulisha mzalishaji mkuu wa tamthilia mpya ya PAZIA Samwel Isike wakati wa uzinduzi rasmi wa tamthilia mpya za kitanzania za PAZIA na JUA KALI zinazorushwa katika chaneli ya Maisha Magic Bongo – DStv 160.

 

 

Tamthilia hii imeaanza kurushwa kuanzia January 4, 2021 na inaonekana Jumatatu hadi Jumatano saa 1:30 Jioni. Tamthilia hii imejaa mikasa, visa, vitimbi bila kusahau mafunzo yatokanayo na maudhui yake. Tamthilia hii imesheheni vinara wa uigizaji hapa nchini akiwemo Jacqueline Wolper anayeigiza kama Miriam Lewa bila kumsahau Hisani Muya anayeigiza kama Henry Lewa

 

Wasanii wanaoigiza katika tamthilia mpya ya PAZIA wakijitambulisha mbele ya waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa tamthilia mpya za kitanzania za PAZIA na JUA KALI zinazorushwa katika chaneli ya Maisha Magic Bongo – DStv 160. Miongoni mwa waigizaji hao ni (kutoka kulia) Tino Muya  (Henry), Welu Sengo (Eliza), Ben Pol (Ben) Nasma Hassan (Regina) na Akim Juma (Edu).

 

 

Uhondo hauishii hapo, kwani mzigo mwingine unaoshushwa ndani ya MMB ni tamthilia ya Jua Kali kutoka kwa mzalishaji maarufu mwanadada Leah Mwendamseke, ambaye mbali ya kuwa ni mzalishaji wa tamthilia maarufu ya Kapuni pia ni mshindi wa tuzo mbalimbali katika tasnia ya filamu.

 

Wasanii wanaoigiza katika tamthilia mpya ya JUA KALI wakijitambulisha mbele ya waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa tamthilia mpya za kitanzania za PAZIA na JUA KALI zinazorushwa katika chaneli ya Maisha Magic Bongo – DStv 160. Miongoni mwa waigizaji hao ni - kutoka kushoto - Romy Jones (Bill Junior) Abbot Charles (Frank) Leah Mwendamseke na  Wansukula Zacharia (Tuma).

 

Tamthilia hii ya Jua Kali itaanza kutingisha jiji mnamo Januari 6, 2021 na itakuwa ikirushwa saa 3.30 usiku Jumatano hadi Ijumaa. Huku nako kuna waigizaji nguli kama  Rainfredd Masako anayeigiza kama Professor Bili na kumejaa vituko na mikasa ya kila aina ambapo wapenzi wa tamthilia hawatapenda kuikosa au kusubiri kusimuliwa.

 

Mtangazaji maarufu nchini Rainfred Masako ambaye anaigiza kama Profesa Bill katika tamthilia mpya ya JUA KALI akiwasalimu washiriki wa hafla ya uzinduzi rasmi wa tamthilia mpya za kitanzania za PAZIA na JUA KALI zinazorushwa katika chaneli ya Maisha Magic Bongo – DStv 160. Hafla hiyo iliyofanyika katika ofisi za DStv Tanzania ilihudhuriwa pia na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo. 

 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamthilia hizo, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo, amesema kuwa serikali inathamini na kutambua mchango mkubwa wa MultiChoice katika kukuza na kuendeleza tasnia ya filamu hapa nchini. Amesema kitendo cha chaneli ya Maisha Magic Bongo kuwa na maudhui mengi ya ndani kimekuwa ni chachu ya ajira nyingi katika tasnia lakini pia kimeongeza ushindani na ubora wa kazi za wazalishaji wetu.

 

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo akizungumza wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa tamthilia mpya za kitanzania za PAZIA na JUA KALI zinazorushwa katika chaneli ya Maisha Magic Bongo – DStv 160. Hafla hiyo iliyofanyika katika ofisi za DStv Tanzania ilihudhuriwa pia nawasanii na waigizaji wa tamthilia hizo na waandishi wa habari.

 

Dr. Kiagho amesema kuwa yeye binafsi amekuwa akiwatemebelea wasanii na kujionea uzalishaji wa filamu mbalimbali hapa nchini na ameridhishwa na kuongezeka kwa ubora na weledi katika uzalishaji wa filamu na maudhui mengine. Amewataka wasanii kutumia fursa hii vizuri na kuhakikisha kuwa wanaongeza ubora wa kazi zao ili ziweze kushindana katika soko la ndani na nje na hivyo tasnia ya filamu kuongeza mchango wake katika uchumi wa wasanii na taifa kwa ujumla

 

 

 

Naye Mkuu Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo, amesema mbali na kutumia wasanii na waigizaji wakongwe, wamehakikisha kuwa kuna mchanganyiko na waigizaji wapya na vijana ambao wanaleta vionjo vipya na vya kisasa katika tamthilia hizo na hivyo kuzifanya kuwa kivutio kikubwa kwa watazamaji wa rika zote.

“Kila mara tunaleta maudhui kulingana na matakwa ya wateja wetu, tunhakikisha kuwa tunawapatia maudhui yaliyoboreshwa na yenye vionjo vipya kila uchao bila kusahau uhalisia wa kitanzania kwenye maudhui yetu” alisema Ronald na kuongeza kuwa wanafurahi sana kufanya kazi na wazalishaji na waigizaji wa Tanzania na hivyo kuzidi kukuza vipaji vya wasainii wetu na kuwapa ulingo wa kuonyesha umahiri wao katika fani.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (wa pili kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo wakati wa uzinduzi rasmi wa tamthilia mpya za kitanzania za PAZIA na JUA KALI zinazorushwa katika chaneli ya Maisha Magic Bongo – DStv 160. Hafla hiyo iliyofanyika katika ofisi za DStv Tanzania ilihudhuriwa pia nawasanii na waigizaji wa tamthilia hizo.

 

Amesema kuwa katika miaka 5 tangu chaneli hiyo ianzishwe, mamia ya wazalishaji na wasanii wa Tanzania wamepata fursa ya kuuza kazi zao na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza soko la maudhui hususan filamu hapa nchini.

Saturday, 19 December 2020

AZAM FC YA MSEMAJI ZAKA ZA KAZI NA ILE YA LWANDAMINA INAVYOSHANGAZA....

 


Nelson Mandela, rais wa kwanza wa Afrika Kusini alikuwa wakwanza kuchaguliwa kidemokrasia na hatimaye akaja kuwa Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, ,alifariki 
Desemba 5,mwaka  2013 akiwa na umri wa miaka 95, alikuwa shujaa kila wakati alizungumza kwa staha , alisema maneno kwa adabu na hekima , mafano aliwahi kusema  "I am not a saint, unless you think of a saint as a sinner who keeps on trying.”  akiwa na maana kuwa " Msinihukumu kwa mafanikio yangu, nihukumuni kwa mara ngapi nilianguka na kuinuka tena"Mwisho wa kunukuu, sina maana ya kuzungumza siasa hapa ninachotaka kukizungumza ni kimoja katika soka husuani Msemaji wa Azam FC Zaka za Kazi Vs Lwandamina.... Zaka ni Msemaji hodari, lakini Lwandamina ni Kocha Mahiri wa Azam FC vitendo vya Lwandamina na Zaka ni Mbingu na Ardhi wakati Zaka akituaminisha msimu huu ubingwa unatua ndani ya klabu hiyo kocha wao Mzambia akili yake wala haimsikilizi kwani hadi sasa Azam FC sare zao ni mfanano wa Maua jana Azam FC ilikubali sare ya kufungana mabao 2-2 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Desemba 18, Uwanja wa Azam Complex, ukiwa ni mwendelezo wa matokeo mabovu kwa Lambalamba hao

Katika mchezo wa jana nyota njema ilianzia kwa Nyota wa Azam FC Ayub  Lyanga alikuwa wa kwanza kucheka na nyavu dakika ya 34, bao hilo lilidumu mpaka muda wa mapumziko na kuwafanya vijana wa Charles Mkwasa kwenda vyumba vya kubadilishia nguo wakiwa nyuma kwa bao moja.

 Kipindi cha pili Iliwachukua dakika 7 Ruvu kuweka mzani sawa kupitia kwa Emmanuel Martin baada ya kipindi kuanza kwa kufunga bao dakika ya 53 ambalo lilidumu kwa muda wa dakika 7 likapinduliwa na Mudahthiri Yahya dakika ya 60.


Ruvu walitumia dakika 10 kusawazisha bao hilo ambapo dakika ya 70 Fully Zully Maganga aliweka mzani sawa na kufanya ubao usome 2-2.

Ni Idd Seleman kwa Azam FC alionyeshwa kadi ya njano huku wajeda wanne walionyeshwa kadi za njano kutokana na nguvu na spidi ndani ya Uwanja wa Azam Complex.


Hii inakuwa ni sare ya pili mfululizo kwa Azam FC ndani ya Uwanja wa Azam Complex baada ya mchezo wao uliopita kufanya hivyo mbele ya Namungo FC na iligawana pointi mojamoja kwa kufungana mabao 2-2.

Matokeo hayo yanaifanya Azam FC ibaki nafasi ya pili ikiwa imecheza mechi 16 kibindoni ina pointi 29 huku Ruvu ikiwa nafasi ya nne na pointi 25 nayo pia imecheza michezo 16.


DORTUMUND YAOKOTWA JALALANI TENA,MOUKOKO AWEKA REKODI YAKE

Mshambuliaji kinda wa Klabu ya Borussia Dortmund, Youssoufa Muokoko  usiku wa kuamkia leo amefunga bao la kwanza ndani ya Ligi ya Uingereza maarufu kama Bundesliga na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo kufunga kwenye ligi hiyo.

Nyota huyo mwenye miaka 16 amevunja rekodi ya nyota wa Bayer Leverkusen, Florian Wirtz ambaye alifunga akiwa na miaka 17 ilikuwa dhidi ya Bayern Munich akiwa  Mei 2020.

Dortmund ambayo ilimchimbisha kocha wao Lucien Favre wiki iliyopita baada ya kupokea kichapo cha mabao 5-1 dhidi ya VfB Stuttgard nafasi iliyochukuliwa na Edin Terzic ilifungwa mabao 2-1 dhidi ya Union Berlin na Moukoko alifunga bao lake la kwanza.

Nyota huyo mzaliwa wa Cameroon amesema kuwa ni furaha kubwa kwake kufunga kwenye mchezo huo ilikuwa dakika ya 60 licha ya timu yake kupoteza jambo ambalo litawafanya wapambane kwa ajili ya mechi zao zijazo.

Mabao ya wapinzani wao yalipachikwa na Taiwo Awonyi dakika ya 57 na lile la ushindi lilipachikwa dakika ya 78 na Marvin Friedrich alipachika bao la ushindi na kuifanya Union Berlin kusepa na pointi tatu mazima Uwanja wa Alle Forsterel.

Matokeo hayo yanaifanya Dortmund iwe nafasi ya nne na pointi 22 baada ya kucheza mechi 13 Bayer Leverkusen  ni vinara wakiwa na pointi 28.



JUMLA YA VIJANA 2000 KUTOKA MKOA WA IRINGA KUFIKIWA NA MRADI WA LYRA IN AFRCA

 

Msimamizi wa mradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA Gift Mafue akitoa elimu kwa baadhi ya vijana waliopo kwenye mradi huo
Msimamizi wa maradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA Gift Mafue akitoa elimu kwa baadhi ya vijana waliopo kwenye mradi huo
Baadhi ya vijana washiriki wa mafunzo yanayotolewa na
maradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA.

 

 Na Fredy Mgunda,Iringa

JUMLA ya vijana 2000 kutoka kwenye wilaya tatu za mkoa wa Iringa kufikiwa na mradi wa imarika kijana wa LYRA IN AFRCA  wenye lengo la kufungua fikra na mitazamo chanya kwa vijana katika Maisha yao.

 

Akizungumza wakati wa kutoa mafunzo kwa baadhi ya vijana ambao wapo kwenye mradi huo, msimamizi wa mradi imarika kijana wa LYRA IN AFRICA Gift Mafue alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuwawezesha vijana kutambua fursa zilizopo na kuzifanyika kazi kwa kupata matokeo chanya.

Alisema kuwa mradi huo unafadhiliwa na watu wa uingereza kwa kuwezesha kutoa mafunzo mbalimbali kwa vijana ambao watakuwa wanatoa elimu kwa vijana na watu wengine kutoka kwenye jamiii ambayo wanaishi huko vijijini kwao.

Mafue alisema kuwa wameshafanikiwa kufanya mafunzo kwa vijana wa vijiji kumi na moja kutoka katika wilaya ya Iringa na Kilolo ambopo hadi sasa takribani vijana 401 wameshafikiwa katika awamu ya kwanza wakitegemea kuanza awamu ya pili mwaka 2021 mwezi wa pili kwa lengo la kufikia vijana wote waliolengwa na mradi.

Alisema kuwa lengo kuu mradi huo ni kuwawezesha vijana kuzitambua fursa zilizopo katika maeneo wanaishi na kuzigeuza kuwa fursa kiuchumi na kukuza maendeleo na kusaidia vijana wasikimbilie mijini na kuzitelekeza fursa zilizopo vijijini.

Mafue alisema kuwa mradi huo unahusisha vijana wenye umri wa miaka kumi na tano hadi ishirini na nane ikiwajumisha vijana walemavu na mzazi mmoja ambao hawana fursa yoyote na kuwasaidia kisaikolojia kuanza kuzichangamkia furs ana kujikombo kimaisha.

“Tunawasaidia pia mzazi mmoja ambaye alipata mimba akiwa shuleni au akiwa na umri mdogo kuzitambua furs ana kuzitumia ili kujikomboa kiuchumi na matumaini kwa vijana wanaoishi vijijini yameongezeka kwa vijana hao kuanza kufanya biashara za kiuchumi” alisema Mafue

 

Alisema kuwa mafunzo ya imarika vijana yamesaidia uundwaji wa vikundi vya kiuchumi ambapo hadi sasa jumla ya vikundi 21 tayari vimeundwa na vinafanya vizuri katika kukopa na kukopesha kwa lengo la kuinua kiuchumi.

Shuhudia Chang’a anatokea Kijiji cha Imalutwa alisema kuwa mafunzo hayo yamekuwa na faida ya kusaidia kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine ya kiuchumi tofauti na ilivyokuwa hapo awali kabla ya kupata mafunzo kutoka LYRA IN AFRICA.

Naye Yasinta Migodela alisema kuwa mafunzo hayo yamemsaidia kuboresha ufanisi wa kibiasha kwa kuwa hapo awali alikuwa anafanya biasha bila ya kuwa na mafunzo na kumpelekea kupata hasara lakini baada ya kupata mafunzo yamsaidia jinsi ya utunzaji wa fedha na mpangilio mzima wa biashara.

Kwa upande wao Stanslaus Mtweve,Nestory Simagunga,Cassian Kihongosi na Rebeka Mbwilo walisema kuwa mafunzo waliyopata kutoka katika shirika la LYRA IN AFRICA yamewasidia kuwakomboa kiuchumi na kifikra kutokana na elimu waliyopewa.

 

“Mara baada ya kupewa mafunzo hayo na shirika la LYRA IN AFRCA yalitusaidia kuridi katika vijiji vyetu na kuendelea kutoa elimu kwa jamii yetu ambao kwa asilimia furani tumesaidia vijana wengi kuacha tabia ya ulevi na matumizi ya madawa ya kulevya na wameanza kujikita katika shughuli za kiuchumi ambazo kwa sasa zinachochea uchumi kukua” walisema

 

 

 

MADIWANI HALMASHAURI MJI MAFINGA WAAHIDI NEEMA YA MAENDELEO KWA WANANCHI WAO

Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Mafinga Reginant Kivinge akiongea madiwani,watendaji na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa baraza hilo.

Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini na mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rose Tweve wakiwa kwenye uzinduzi wa baraza hilo la madiwani



MADIWANI wa Halmashauri ya mji wa Mafinga mkoani Iringa wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ili kureta maendeleo kwa wananchi waliwachagua na kuwapa dhamana ya kuwepo madarakani mara baada ya uchaguzi mkuu

Akizungumza mara baada ya kuzinduliwa kwa baraza jipya la madiwani wa Halmashauri ya mji wa Mafinga,mwenyekiti wa halmashauri hiyo Reginant Kivinge alisema kuwa wananchi wanamatumaini makubwa ya kimaendeleo kutoka kwa madiwani hao hivyo wanapaswa kwenda kuchapa kazi kwa nguvu zao zote.

Kivinge alimuomba mkurugenzi wa halmashauri hiyo Saada Mwaruka  pamoja na watendaji wote kuhakikisha wanashirikiana kwa ukaribu ili kuhakikisha wanatatua na kumaliza kero zote zinazowakabili wananchi.

 

Alisema kuwa halmashauri hiyo bado inakabiriwa na changamoto nyingi ambazo zimekuwa zikikwamisha juhudi za kureta maendeleo kwa wananchi wa jimbo la Mafinga Mjini hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa umoja wao ili kuleta maendeleo kwa wananchi yanayotarajiwa.

  "Natambua uchaguzi huu ulioisha tulipitia mambo mengi sana,lakini sasa uchaguzi umekwisha  ni mwendo wa kuchapa kazi sasa twende kuchapa kazi ili turudishe ile heshima muliyopewa na wananchi wetu kwa kutuchagua " alisema

 

 

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wa (CCM) wilaya ya Mufindi mkoa wa Iringa Daudi Yasini amewataka madiwani wa halimashauri ya Mji Mafinga kwenda kushungulika na kutatua kero za wananchi kwani chama hicho hakitasita kumchukulia hatua diwani yoyote asiyetimiza majukumu yake ipasavyo .

Kauli hiyo imetolewa wakati wa kikao cha kwanza cha madiwani wa halmashauri hiyo baada ya kula kiapo cha utii wa kuwatumikia wananchi kwa kufuata kanuni za maadili ya utumishi wa umma

Daudi alisema kuwa wananchi wamekuwa na imani kubwa na chama cha mapinduzi hivyo hivyo wanapaswa kuheshimu na kuthamini nafasi waliyopewa kwa kufanya kazi kwa weredi na ushirikiano kuhakikisha wanatatua kero za wananchi wa halamshauri hiyo.

"Tumekuwa na uchaguzi nyingi ila uchaguzi wa mwaka huu tumeweka historia kwa wilaya ya Mufindi kwa baraza letu lote ni CCM na hii ni kwa sababu ya kazi kubwa iliyofanywa na mh Rais Magufuli hivyo naamini hamtatuangusha mkatumikie nafasi muliyopewa kwa weredi uliotukuka" 

 

Daudi alitoa onyo kali kwa madiwani wote wanaodhani wamepewa nafasi hiyo kwa ajili ya kujinufaisha wao au kujipatia mali katika Halmashauri hiyo,chama cha mapinduzi kitapita kata kwa kata kuhakikisha kuwa viongozi waliochaguliwa wanatatua kero za wananchi la sivyo hatua kali zitachukuliwa kwa Diwani husika.

“Niwaonye wale wote ambao mnadhani mmepata nafasi ya kwenda kupiga dili halimashauri hapa ni kazi tu na endapo tutakuja kwenye kata yako na kukuta wananchi wanalalamika kero nyingi hazitatatuliwa basi hawatasita kuwachukulia hatua” alisema Daudi

Hata hivyo Daudi alimtaka mkurugenzi pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kushirikiana vyema na madiwani hao ili kutatua kero za wananchi zinazowakabili na sio kupishana kwenye maamuzi ya vikao ambavyo lengo ni kupunguza mzigo wa kero kwa wananchi

Naye katibu wa CCM wilaya ya Mufindi James Mgego aliwashukuru madiwani hao kwa uvumilivu na ushindi waliopata kwenye uchaguzi uliopita kwani walipita kwenye viunzi na vikwanzo Vingi mpaka kufika hapo walipo

Mgego alisema kuwa wananchi wamemaliza kazi yao na wajibu wao hivyo sasa ni wakati wa madiwani hao kurudisha dhamana na heshima waliyopewa kwa kwenda kuwatumikia na kutatua kero za wananchi

Alisema chama hicho kinatambua dhamana kubwa waliyopewa na wananchi hao kwa kuonyesha imani kwa chama hicho hivyo wanadeni kubwa la kurudisha maendeleo ya kweli kwa watanzania wote bila kujali itikadi ya vyama kwani uchaguzi umekwisha na sasa ni muda wa kuchapa kazi

Lakini pia Mbunge wa jimbo la Mafinga Cosato Chumi alissema kuwa anataka kupeleka mapendekezo bungeni ili kuweza kupata kibali na kubadili sheria ili kufanya biashara kwa mji wa Mafinga masaa 24 kwani wilaya hiyo inapitiwa na barabara kuu hivyo itakuwa ni fursa ya kukuza uchumi kwa wakazi wa Mafinga na kuongeza pato la halimashauri hiyo endapo watu watafanya biashara masaa 24 

Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Mafinga Saada Mwaruka alisema kuwa watendaji wote wa halmashauri hiyo wapo tayari kujitolea na kuonyesha ushirikiano kwa madiwani wote ili kuhakikisha wanatatua kero za wananchi na kuleta maendeleo katika Jimbo la Mafinga Mjini.

 

 

Wednesday, 17 June 2020

BABA WA SAMATTA ANENA JAMBO....WAKATI SAMATTA AKIWA UWANJANI LEO EPL

MSHAMBULIAJI wa timu ya Aston Villa inayoshiriki Premier League, Mtanzania, Mbwana Samatta amemhakikishia baba yake mzazi, mzee Ally Samatta kuwa atapambana kuhakikisha anainusuru timu yake isishuke daraja msimu huu.

Samatta ambaye amejiunga na timu hiyo katika usajili wa dirisha dogo msimu huu kwa mkataba wa miaka minne na nusu, ana kazi kubwa ya kuibakisha timu hiyo kutokana na kuwa kwenye nafasi mbaya ya 19 ikiwa na pointi 25 ikifuatiwa na Norwich City ambayo inaburuza mkia ikiwa na pointi 21.

Mzee Samatta alisema kuwa, kutokana na ligi kutarajiwa kurejea tena leo Juni 17, 2020, mtoto wake amemwambia atapambana kuinusuru timu hiyo kushuka daraja.

“Suala la ligi kurejea lipo wazi na kila mmoja amekuwa akilijua vizuri isipokuwa kijana amenieleza nia yake ni kutaka kuinusuru timu isishuke hivyo amepanga kucheza kwa kujituma zaidi ili kufikia malengo.

“Unajua wapo ambao walitaka ligi ifutwe kama zilizofanya nchi nyingine lakini England wao wameona ni bora kumalizia hivyo kila mmoja anatakiwa apambane na yeye ndiye amenieleza kwamba hatamani kuona wakishuka hivyo lazima ajitoe ili kuinusuru timu na msimu ujao waanze pamoja,” alisema mzee Samatta.

WADAU WATAKIWA KUENDELEA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KUINUA MICHEZO







WADAU WAMETAKIWA KUENDELEA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KUINUA MICHEZO  KUWEKA UDHAMINI KWENYE TIMU ZA MTAANI ILI KUIBUA VIPAJI AMBAVYO VITAKUA NA MANUFAA KWA TAIFA 
Kuali hiyo imetolewa katika Mchezo wa Kusisimua uliozikutanisha  timu mbili kati ya Soccer City ya Mabwepande ya Mtaa wa Mji Mpya  dhidi ya timu ya New Kibamba FC Mchezo ambao umedhaminiwa na kampuni ya Msukuma One inayodhalisha na kusambaza Nafaka huku lengo ikiwa kuunga Mkono Serikali ya awamu ya tank kuunga mkono juhudi za kuinua sekta ya Michezo.

Mkurugenzi Mkuu wa Msukuma One Aman Manengero amesema kuwa wataendelea kusaidia jitihada hizo ili kuleta meandeleo zaidi.
Ktika mchezo huo mkali ilishuhudiwa timu ya kibamba FC kukubali kipigo baada ya kuzidiwa kwa mikwaju ya penati dhidi ya timu ya soka city baada ya timu hizo kutoka sare ya 

goli mbili kwa mbili ndani ya dakika tisini huku timu ya soka city ikiibuka na zawadi ya jezi iliyotolewa na mdau huyo.






 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube