BREAKING

Saturday 20 July 2024

MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping katika ukumbi wa The Great Hall of the People kabla ya kuanza mazungumzo jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na ujumbe wake wakiwa kwenye kikao cha pamoja na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping na ujumbe wake katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing, tarehe 4 Septemba, 2024.






Friday 19 July 2024

MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akutana na Watanzania wanaoishi nchini China (Diaspora) wakiwemo wafanyakazi, wanafunzi na wafanyabiashara,  Jijini Beijing tarehe 06 Septemba, 2024.







Monday 29 April 2024

RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Kenya Mhe. Dkt. William Ruto mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mawaziri wa Kenya Musalia Mudavadi mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA.

RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Viongozi mbalimbali kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuainisha vipaumbele vya Nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya tarehe 29 Aprili, 2024. IDA ni Mfuko Maalum wa Benki ya Dunia ambao unatoa mikopo nafuu na misaada kwa nchi zinazoendelea.

Sunday 7 April 2024

RAIS DK.MWINYI AONGOZA DUA KUMBUKUMBU YA KARUME







RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameongoza kisomo cha Dua na Hitma ya kumuombea Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, iliyofanyika Afisi Kuu CCM Kisiwandui  Zanzibar tarehe 07 Aprili 2024.


Viongozi mbalimbali wameshiriki wakiwemo wa Serikali, Dini , Vyombo vya ulinzi na usalama na Vyama vya siasa.

Thursday 4 April 2024

RAIS SAMIA AWAAGIZA VIONGOZI WATEULE KUHESHIMIANA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wateule kuwa nguzo kubwa katika kutatua migogoro iliyopo kwenye jamii na sio kuisababisha migogoro.

Mhe. Rais Dkt. Samia amesema hayo kwenye uapisho wa viongozi wateule, Ikulu jijini Dar es Salaam, ambapo amesema mabadiliko ya viongozi ni mambo ya kawaida, ili kuimarisha ufanisi katika utendaji kazi kwa jamii na niwajibu wa viongozi kwenda kuwatumikia wananchi pindi wanapoteuliwa .

Aidha Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka  aliyekuwa Naibu Waziri wa Tamisemi, Deogratusi Ndejembi ambaye sasa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu akimsihi kwenda kufanya kazi kwa ukaribu na ushirikianio na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Patrobas Katambi, huku akitoa maagizo ya kuhakikisha vijana wanapata ajira na kuajiriwa.

Katika hatua nyingine amekemea migongano ya kimadaraka katika taasisi walizopo kwani watakapofanya hivyo hatosita kuwaondoa wote wawili…


RAIS SAMIA: MAKONDA UMENIKOSHA UMETUCHANGAMSHA WANACCM


IKULU-Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemuapisha aliyekuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Paul Makonda leo Aprili 4, 2024 Ikulu, Dar es Salaam kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Makonda anachukua nafasi ya John Mongella Hafla ya uapisho huo inahusisha viongozi mbalimbali 

Wednesday 3 April 2024

HAPI AULA U-KATIBU MKUU JUMUIYA YA WAZAZI CCM


Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) chini ya uenyekiti wa Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano, Aprili 3, 2024 imemteua aliyewahi kuwa mkuu wa mikoa ya Iringa na Mara, Ally Hapi kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa chama hicho.

Hapi anachukua nafasi ya Gilbert Kalima ambaye ameteuliwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga.

NI JOKATE TENA UVCCM VIJANA..


Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imemteua Jokate Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) akichukua nafasi ya Fakii Lulandala ambaye ameteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.

MAKALA AMRITHI MAKONDA NEC , JOKET,HAPI MAMBO SAFI



 

MWENYEKITI SAMIA AONGOZA KIKAO KAMATI KUU CCM









Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Dk. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM, kilichokutana leo Jumatano, Aprili 2024, jijini Dar Es Salaam.

RAIS SAMIA AZINDUA TUME YA ULINZI TAARIFA BINAFSI NA MIFUMO YA USAJILI...


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na wageni mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na Mifumo ya Usajili na Malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Aprili, 2024.









Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akigusa screen ya iPad kuashiria uzinduzi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na Mifumo ya Usajili na Malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Aprili, 2024.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya picha iliyotengenezwa na kufumwa kwa nyuzi kutoka kwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye mara baada ya kuzindua Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na Mifumo ya Usajili na Malalamiko ya ukiukwaji wa misingi ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 03 Aprili, 2024.

Tuesday 2 April 2024

DSTV WAZINDUA KAMPENI YA MFALME WA BOMA YAWEKA KIHISTORIA ...





Afisa maendeleo bodi ya Filam nchini Simon Peter, amewaka watunzi wa Filam nchini kuwa wabunifu ili kuendelea kutengeneza soko kubwa la ajira kwa wasanii huku akiwakumbusha wasanii kuendelea kusajili kazi zao za sanaa katika Bodi ya filam

Hayo ameyasema wakati wa uzinduzi wa Tamthiliya ya Jiya mfalme wa Boma , ambayo imeshirikisha wasanii mbalimbali ikibeba maudhui ya kitanzania 

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo akizungumza katika uzinduzi huo amesema kwamba kwa mara ya kwanza DSTV imepokea kazi yenye viwango vikubwa ikiwemo mchanganyiko wa wasanii maarufu na wasio maarufu.

Katika hatua nyingine kuelekea marudiano ya michuano ya vilabu bingwa Afrika ambapo Simba na Yanga zinatarajia kucheza michezo yao ambapo Simba watawavaa Al Ahly Ijumaa wiki hii na Yanga wakiwakabilia Mamelod Sundowns siku hiyo hiyo amazitakia kheria huku akisema timu hizo zinauwezo mkubwa wa kutinga hatua ya nusu fainali.

ROTARY CLUB WATOA MAFUNZO KWA WALIMU 80 YA KIDIGITAL

Jacline Woiso-Mwanachama wa Rotary Club 

Moses Fransis Mkuu wa Shule ya Msingi Kunduchi


Baadhi ya wanachama wa Rotary Club na walimu wakifurahia jambo wakati wa Uzinduzi wa Mafunzo ya Kidigital


Hamza kasongo Mwanachama Rotary Club akizungumza na walimu washiriki wa Mafunzo ya Kidigital 



Ili kuendana na kasi ya kidigital ya ukuajia wa teknolojia duniani Taasisi ya Rotary Klabu imetoa mafunzu ya Teknohama kwa walimu wa Shule tano za msingi  katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam,.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Mwananchama wa Rotary Klabu  Jackline Woiso amesema mafunzo hayo ni faida kubwa kwa walimu hao husuani kipindi hiki ambacho matumizi ya digital yanazidi kukua ambapo kuptia mafunzo hayo yatakapomalizika watakuwa wamepata faida.

Ameongeza  mafunzo hayo kwa walimu zaidi ya 80  itawajengea uwezo wa kutumia teknolojia hiyo  kwa upande wa uongozi na kuwajengea wanafunzi uwezo pindi wakiwa wakubwa kuendana na kasi ya Dunia  

Kwa upande wake Dkt. Gaudensia Tesha  Mhadhiri idara ya Kompyuta  Chuo cha DIT amesema kuwa mafunzo hayo ya walimu kutumia vishikwambi  itawasaidia kwa urahisi kuandaa matokeo ya mitihani yaweze kuchakatwa kwa urahisi, huku baadhi ya washiriki  wa mafunzo hayo Moses Fransis ambaye ni Mkuu wa Shule ya msingi Kunduchi akisema  kuna changamoto kubwa baadhi ya walimu wengi  hawana uelewa na mambo ya tehama hivyo itawasaidia kupunguza changamoto hiyo


 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube