BREAKING

Thursday 7 January 2021

LAMECKY NYAMBAYA KIONGOZI MPOLE USONI! MWENYE HAIBA YA UANA MICHEZO...MUUMINI WA SOKA LA VIJANA.




Na Said makala

Nelson Mandela, rais wa kwanza wa Afrika Kusini kuchaguliwa kidemokrasia na Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, , alifariki Desemba 5, mwaka 2013 akiwa na umri wa miaka 95, Mandela aliwahi kutumikia kifungo kwa miaka 27 kwa sababu ya mapambano yake dhidi ya mfumo wa kibaguzi wa Afrika Kusini unaofahamika kama  Ukaburu, Aliachiwa huru kutoka gerezani mwaka 1990, na kuwa rais miaka minne baadae, na kuachia madaraka baada ya kutumikia kwa kipindi kimoja tu, kitendo adimu kufanywa na wenye madaraka barani Afrika.

Ni Mpambanaji aliyeonyesha uwezo wa kuongoza kwa vitendo, yes! alikuwa mtu mhimu sana katika Ulimwengu wa siasa , wacha nisiseme ya kisiasa hapa nataka kumzungumzia mtu mmoja anaitwa Lamecky Nyambaya Mwenyekiti Mpya wa Chama cha soka Mkoa wa Dar es Salaam, mtu jasiri hususani kuhamasisha soka nchini ambaye alianza kujiimarisha kwenye uongozi wa soka la Vijana 

Mwaka Jana Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) siku ya Jumapili,ya  Novemba 29,mwaka  2020 Ulifanyika uchaguzi na kupata viongozi wapya ambao wataongoza  chama hicho kwa miaka minne, nafasi hiyo ya Mwenyekiti iliyokuwa imeachwa wazi na Almasi Kasongo ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi (TPLB) tayari ina mtu sahihi mwenye haiba ya aina yake mtu mwenye moyo wa kusaidia soka popote anapokwenda, Huyoni Lamecky Nyambaya...


 Lameck Nyambaya aliyekuwa mgombea pekee na kupata kura 27 aliaminiwa zaidi na hiyo inatokana na utendaji wake wa kazi uliotukuka akiwa Mjumbe wa soka ndani ya Shirikisho la soka tanzania TFF,  akiwakilisha Mkoa wa Dar es salaam , hivi sasa bila shaka kupewa mikoba ya kuwa Mwenyekiti DRFA mengi mazuri yanakuja , katika mwaka wa 2021 Nyambaya anatakiwa kuzingatia mambo mengi lakini machache nitayataja na ni haya yafuatayo ili haiba yake iweze kutimia zaidi na kuendelea kupata sifa za kiongozi...

Kwanza.. .Nyambaya anapaswa kuendeleza pale Almas Kasongo alipoachia na kupiga mbizi ndefu kuleta maendeleo ya soka kwa kuwa tayari ana uzoezfu wa kuongoza, 

Pili.. .Azungumze na wadau kupata kilio cha wanamichezo kwani wapo wazazi ambao wanaaminiu kuwa vijana wao kudidimia katika soka ni kupoteza mwekeo sawa na wale wanaoingia katika shindano la Miss Tanzania wakiamini kule ni kujidhalilisha bila kujua kuwa huko kuna vipaji vinavyokufa kutokana na imani hizo potofu, hivyo anapaswa kuwa mshawishi zaidi kwa wazazi kupata vipaji.

Tatu...Nyambaya asijifungie Ofisni asiwe na Umangi Meza hayo yote akiepuka tunamuona Nyambaya mkubwa katika uendelezaji wa soka Tanzania kwa miaka ijayo

Hizo ni nguzo chache ambazo zinanishawishi kuamini Lamecky Nyambaya ni mtu mwenye malengo ya haki na maamuzi ya busara kila mara anapoamua kusaidia soka, naamini amekuwa karibu na familia ya soka amekuwa mwenye huruma na familia ya soka kama alivyo na huruma kwa familia yake hivyo wadau washikamane naye katika kuhakikisha soka linakuwa zaidi kwani yupo katika jiko bora la Dar es salaam, ambalo limejaa viungo vya kila aina , nikimanisha Mkoa wa Dar es salaam, ndio wenye vipaji vya kila aina....mimi nashawishika kumwita Lamecky Nyambaya ni Kiongozi wa mfano kwa kuwa hana Mbwembwe anatekeleza mambo yake kwa vitendo.


No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube