BREAKING

Wednesday 28 March 2018

MBWANA SAMATTA ASEMA TANZANIA ITAVUMA KIMATAIFA ZAIDI KUTOKANA NA WACHEZAJI VIJANA KUWA WENGI KWA SASA


Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania ambaye pia anasakata kandanda la kulipwa Ubelgiji Mbwana Ally Samatta, amesema vipaji Tanzani vipo nabado muda mchache Tanzania itafanya vyema kimataifa.

Nyota huyo amesema hayo mara baada ya timu ya Tanzania kuonyesha kiwango kikubwa katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki baada ya kuifunga Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) mabao 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
  Pongezi kwa wafungaji wa mabao hayo, Nahodha Mbwana Ally Samatta wa KRC Genk ya Ubelgiji na Shiza Ramadhani Kichuya wa Simba.

Huo unakuwa ushindi wa kwanza Tanzania tangu Julai 7 mwaka jana ilipoichapa kwa matuta Lesotho baada ya sare ya 0-0 kwenye Kombe la COSAFA mjini Rusternburg, Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube