BREAKING

Monday 12 March 2018

AZAM FC HAOOO NAFASI YA PILI, YAITANDIKA MBAO 2-1


Azam FC imerejea tena kwa muda kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi, baada ya kuifunga Mbao FC kwa mabao 2-1.

Ikiwa Uwanja wake wa nyumbani, Azam ilianza kupata bao la kwanza kupitia kwa Idd Kipagwile akifunga dakika ya 63.

Baada ya bao hilo, ilichuka dakika saba pekee ambapo Bernard Arthur alifunga bao la pili katika dakika ya 72 ya mchezo.

Bao pekee la Mbao lilifungwa na James Msuva, dakika ya 90 na Emmanuel Mvuyekure.

Matokeo hayo yanifanya Azam kuwa juu ya Yanga kwenye msimamo wa ligi kwa muda, ikifikisha alama 44 dhidi ya Yanga yenye 43.

Yanga itarudi kwenye nafasi endapo itashinda mchezo wake wa kesho dhidi ya Stand United utakaopigwa Uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube