BREAKING

Wednesday, 2 August 2023

KINANA: WAPINZANI JENGENI HOJA, ACHENI KEJELI KWA RAIS’.






MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahaman Kinanaa amewashauri na kuwakumbusha wanaiasa wa upinzani kuheshimu fursa ya maridhiano ya kisiasa iliyotolewa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.


Amesema lugha za matusi, kejeli na dharau dhidi kiongozi wa nchi zinapaswa kuepukwa ili kutoa fursa ya kuendeleza maridhiano na kuijenga Tanzania kwa pamoja.


Kinana ameyasema hayo jana mjini Tabora wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara alipokuwa akihitimisha ziara yake ya kikazi katika mikoa ya Dodoma, Manyara, Mara, Simiyu na Tabora kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 na uhai wa Chama.


"Niwasihi ndugu hatukatai mtoe hoja, hatukatai mseme yale mnayotaka kusema lakini semeni kwa uungwana, zungumzeni kwa busara, jengeni hoja.


"Kusema Rais ana akili za matope au kusema Rais ameuza bandari, wewe sema mkataba huu haujakaa  vizuri, utaeleweka, toa hoja kwa nini hauajakaa vizuri, upande wa pili watasema umekaa vizuri, lakini ukisema mkataba huu hata kichaa hawezi kuubali, maana nyingine unatuambia sisi sote ni vichaaa."


Kinana alitumia fursa hiyo kuelezea mchakato wa kupata maridhiano ambayo yametoa fursa ya wananchi wakiwamo wanasiasa kuwa na uhuru wa kutoa maoni.


"Kabla ya hapo mtakumbuka Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe alikuwa jela, Rais (Dk . Samia) kabla ya kesi haijamalizika akaamua kumwalika Ikulu...wakazungumza, wakakubaliana kwamba tujenge amani na umoja, hatimaye mazungumzo ya Chamwino yakazaliwa. Rais akaunda timu ya watu 10, watano CCM na watano Chadema. Leo nayasema haya  kwa sababu mimi ni Mwenyekiti kwa upande wa CCM katika mazungumzo hayo ya maridhiano. Mwenyekiti mwenzangu Freeman Mbowe yeye aliongoza upande wa pili na walikuja na hoja 15," amesema. 

 

Sunday, 23 July 2023

KINANA : MSHIKAMANO, MOJA NI SILAHA YA USHINDI KUELEKEA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA.








MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana, amewashauri viongozi wa Chama hicho katika ngazi zote kuendeleza umoja ili kwenda katika Uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 pamoja na Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 wakiwa wamoja na kuibuka washindi pamoja.

Kinana ameyasema hayo leo Julai 23, 2023 wakati akizungumza na viongozi wa CCM katika kikao cha ndani cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kondoa mkoabi Dodoma.

"Napongeza kazi kubwa inayofanywa na viongozi wa CCM hususan katika ngazi kitongoji, Kijiji, mtaa na Kata kwa kazi nzuri mnayoifanya. Mwakani ni mwaka wa Uchaguzi, hivyo naamini wana CCM tutakwenda kwenye uchaguzi wa Serikali za Mtaa mwaka 2024 tukiwa kitu kimoja, tukifanya kampeni wamoja na tutaibuka na ushindi tukiwa wamoja, hivyo hivyo katika uchaguzi mkuu mwaka 2025," amesema Kinana.

Ametumia nafasi hiyo kueleza kwamba Chama pia kinatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotelewa na viongozi wa CCM katika ngazi za kata, vitongoji, vijiji, wilaya na mkoa kwani wao ndio wanaokutana na wananchi na wakati wa uchaguzi ndio wanaokwenda kuomba kura.

Pia, amewapongeza madiwani wanaotokana na CCM ambao wamekuwa wakisimamia ngazi ya Kata na wamekuwa wakifanya hivyo bila ya kuwa na mshahara.

Saturday, 15 July 2023

KATIBU MKUU WA CCM DANIEL CHONGOLO AWASILI MBEYA...




 







Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) akisalimiana na wajumbe Mbeya mara baada ya kuwasili Mbeya ikiwa ni Ziara yake ya Siku moja yenye lengo la Kuzungumza na Wananchi pamoja na Wana CCM kutoka Baadhi ya Mikoa ikiwemo Songwe, Iringa, Rukwa pamoja na Njombe

Wednesday, 12 July 2023

WIZARA YA NISHATI YATENGA BILIONI TANO KUCHANGIA UTOAJI ELIMU YA UTUNZAJI MAZINGIRA KULINDA MABWAWA

 Wizara ya Nishati imetenga Sh bilioni tano katika bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya kuchangia utoaji elimu ya kutunza mazingira ili kulinda mabwawa yanayozalisha umeme nchini.

Waziri wa Nishati January Makamba amesema hayo katika ziara ya viongozi wa dini kutoka baraza Kuu la waislam Tanzania lililofanya ziara katika mradi ya kufua Umeme,wa Julius Nyerere .




Waziri wa Nishati January Makamba 




Wednesday, 21 June 2023

DC MOYO AONDOA SINTOFAHAMU KATIKA MLIMA CHILALO



Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo akiongea na wananchi wa Kijiji cha Mbute juu ya sintofahamu ya uchimbaji wa madini katika mlima Chilalo

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo akiwasikiliza wananchi wa Kijiji cha Mbute wakati wa kuondoa hofu kuwa Mlima Chilalo upo wilaya ya Ruangwa



Na Fredy Mgunda, Nachingwea

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo amefanikiwa kuondoka sintofahamu kwa wananchi wa Kijiji cha Mbute iliyokuwa imetanda juu ya uchimbaji wa madini ya Graphite  katika mlima Chilalo

Akizungumza wakati alipofanya ziara katika Kijiji hicho baada kusambaa Kwa video ikionyesha malalamiko ya wananchi juu mlima na msitu wa akiba wa Chilalo kuonekana upo katika wilaya ya Ruangwa na sio Nachingwea.

Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo aliwaeleza wananchi kuwa Mlima Chilalo upo wilaya ya Nachingwea na kila shughuli inayofanywa kwenye Mlima huo mapato yote yatakuwa ya wananchi wa wilaya ya Nachingwea.

Moyo aliwatoa hofu hiyo kwa kuwaambia suala la mipaka linashughulikiwa na serikali ya mkoa wa Lindi kwa ofisi ya wilaya ya Nachingwea ilifanya kazi mgogoro huo ila bado upande wa mkoa na kuhaidi hivi karibuni wataalam kutoka TAMISEMI na ofisi mkoa watafika eneo hilo kutatua mgogoro huo.

Kwa upande wake Afisa madini mkazi mkoa wa Lindi Eng Dickson Joram alisema kuwa leseni iliyotelewa katika eneo la Mlima Chilalo ni leseni ya utafiti na sio ya kuchimbwa kwa madini ya Graphite katika eneo hilo.

Eng Joram alisema kuwa wananchi wanatakiwa kuondoa hofu kuwa eneo hilo limeanza kuchimbwa madini wakati sio kweli.

Nao baadhi ya wananchi walisema kuwa wanampongeza mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo Kwa kuwapeleka wataalam na kutoa ufafanuzi juu ya uchimbaji wa madini ya Graphite katika mlima Chilalo

"Tumepata ufafanuzi wa mambo kadhaa ikiwemo mradi wa uchimbaji wa madini ya Graphite  Mlima Chilalo ambao umetulea hofu iliyokuwa imetanda Kwa wananchi"walisema

Tuesday, 20 June 2023

FOODPOINT WAPO MLANGONI KWAKO


 

Wednesday, 14 June 2023

ZIARA YA RAIS SAMIA -MWANZA YASHUSHA NEEMA AHAIDI KUKAMILISHA MIRADI YOTE YA KIMKAKATI




 

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube