BREAKING

Tuesday, 10 March 2020

BRAND KENYA YATUA JIJINI DAR ES SALAAM .....



The High Commissioner of the Republic of Kenya in the United Republic of Tanzania Amb. Dan Kazungu on Monday received a high- level trade mission from Kenya’s Export and Branding Agency, Brand.KE. The trade delegation was led by the Chief Executive Officer Mr. Peter Biwott. The trade mission is in Dar es salaam to hold consultations with key Tanzanian trade and investment promotion organisations in a bid to promote and enhance bilateral trade between Kenya and Tanzania. These include Tanzania Trade and Development Authority (TANTRADE), Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA) and Tanzania Private Sector Foundation (TPSF).
Kenya’s High Commissioner Amb. Dan Kazungu with Mr. Peter Biwott, CEO of Brand.KE holding discussions during the latter’s visit at the Kenya High Commission on Monday9th March 2020
While welcoming the delegation, Amb. Dan Kazungu mentioned that 48 percent of intra East African Community (EAC) trade occurs between Kenya and Tanzania which is an indication of the interdependence that exists between the two countries. He added that there is need for both Kenyans and Tanzanians to cooperate even more for shared prosperity.
On his part, Mr. Biwott said that it was a high time that Kenyans and Tanzanians focused more on cross border trade that would boost each other’s economies more as opposed to seeking foreign markets whose returns were much lower. Mr. Biwott also noted that Kenya and Tanzania are unique countries with vast opportunities ranging from agriculture, infrastructure, services, mining, logistics and the blue economy. In addition, there are opportunities for Kenyan companies in the financial service sector. These opportunities can be seized through partnerships with Tanzanian companies.
Brand.KE is a State Corporation established under the State Corporations Act Cap 446 through Legal Notice No.110 of August 9th, 2019 after the merger of the Export Promotion Council and Brand Kenya Board. The Brand.KE mandate is to implement export promotion and nation branding initiatives and policies to promote Kenya’s export of goods and services.
Brand.KE CEO Mr. Peter Biwott signing the visitor’s book at the Kenya High Commission. With him is Kenya’s High Commissioner Amb. Dan Kazungu
Kenyan companies, through Brand.KE, will participate in the 44th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF) slated for June and July 2020. Brand.KE has reserved a substantive number of booths for this years’ event that promises Kenyan high-level participation and a showcase of how trade and investment is undertaken in the East African region and beyond.
The DITF presents Kenyan companies to invest in Tanzania as well as export their goods and services while at the same time, offering opportunities to the Tanzanian private sector in so far as market and product diversification is concerned. Thus, participation in the Trade Fair will enhance trade, investment and tourism with a view to promote accelerated economic growth and development between the two countries and East Africa as well as the African continent.
Brand.KE in conjunction with the Kenya High Commission Dar es Salaam will organize a high-level business forum, an elaborate diaspora engagement and high-level participation at the Dar es Salaam International Trade Fair (DITF) between March and July 2020. The trade mission will focus its activities in four regions in its bid to boost the distribution channel of Kenyan goods in Tanzania. These include: - Mwanza (Mwanza region), Arusha and Moshi (Kilimanjaro region), Dar es Salaam (Dar es Salaam and Coast regions) and Mbeya (Southern region).
Brand.KE are also planning a second visit that will focus on developing an elaborate distribution channel for Kenyan goods in Dodoma (Central Tanzania) and Zanzibar in a carefully conceived and deliberate strategy to promote Kenyan exports in the United Republic of Tanzania.
Amb. Dan Kazungu receives a gift from Mr. Peter Biwott, CEO of Brand.KE at the Kenya High Commission on Monday 9th March 2020
The Kenya High Commission in Dar es Salaam is upbeat that these efforts will improve the trade performance that stands at Kshs 33.5 billion in January 2020, up from Kshs 28 billion in 2018.

ISUPILO HAKUNA ARDHI YA KUGAWAKWA WANANCHI,MIPAKA YA GEREZA ILINDWE.

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ikongosi wilaya ya Mufindi

NA FREDY MGUNDA,MUFINDI.
 
MKUU wa magereza la Isupilo Benjamin Kabisa wamejipanga kulinda ardhi ya magereza kwa kuwa  Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli amegiza kuwa magereza yote kuanza kujitegemea kwa kuzalisha chakula kupitia wafungwa.


Hoja hiyo imekuja mara baada ya wananchi wa kijiji cha Ikongosi wilaya ya Mufindi la kuomba ardhi ya kulima katika eneo la jeshi la magereza kwenye mkutano wa mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi wakati wa ziara ya Iringa mpya awamu ya pili.


Benjamin alisema kuwa eneo la gereza la Isupilo mipaka yake inajulikana na ipo kisheria nay eye hawezi kugawa eneo hilo hadi pale mamla za juu za serikali zitakavyo amua kwa kuwa kila kitu kipo kimaandishi.


Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi alikataa ombi hilo kwa wananchi wa kijiji cha Ikongosi  wakati wa mkutano wa kupokea kero za wananchi wa wilaya ya Mufindi.


Alisema kuwa ardhi ya magereza ni kwa ajili ya matumizi ya magereza kuzalisha chakula kwa ajili ya wafungwa.

hata hivyo Hapi alisema kuwa sio kila ombi la wananchi anatakiwa kuwatekelezea kwani kimsingi ardhi ya magereza ni maalum kwa ajili ya utaratibu wa serikali kuhifadhi ardhi yake kwa ajili ya matumizi yake ya baadae.

"Serikali ina kawaida ya kuwekeza benki ya Ardhi kwa ajili ya matumizi ya kijamii ikija kutokea wananchi wameongezeka na serikali inahitaji kujenga kituo cha afya ama shule benki yake ya ardhi ni kwenye ardhi hiyo iliyowekezwa kwenye taasisi zake kama magereza,jeshi la kujenga Taifa na maeneo mengine"

Aidha alisema iwapo wananchi wanahitaji eneo kwa ajili ya ujenzi wa shule wanaweza kukaa chini na Magereza ili kupewa eneo Ila sio kwa ajili ya kilimo .

Alisema kimsingi shule ni mali ya serikali na magereza ipo chini ya serikali hivyo wanaweza kupewa eneo la ujenzi na kuwekewa mipaka.

"Ila niwaeleze wazi wananchi kuwa sio kila ombi mnaloomba mnaweza kusikilizwa maombi mengine hayawezekani kama hili la kuomba ardhi ya magereza kwa ajili ya kulima  watu binafsi"


Hata hivyo Hapi aliagiza magereza kutumia wafungwa kuendeleza ardhi hiyo kwa kilimo Kama Rais Dkt John Magufuli alivyoagiza kwa magereza zote nchini kutumia wafungwa kuzalisha chakula Chao wenyewe.

TARURA SITISHENI UJENZI WA BARABARA ZA VUMBI HADI MVUA ZITAKAPO SIMAMA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akizungumza kwenye ziara ya Iringa mpya awamu ya pili alipokuwa anakagua ujenzi wa barabara yaKinyanambo, Pareto,Chumi,Lutherani na Mwamkoa Mbagala iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga akiwataka wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) kusitisha ujenzi wa barabara hizo kwa kuwa ujenzi huo hauna tija kwa wananchi
 Baadhi ya uharibifu unaondelea kwenye maeneo ambayo ujenzi wa barabara unaendelea hivi sasa kwenye maeneo ya Mji wa Mafinaga Mji.
 Baadhi ya uharibifu unaondelea kwenye maeneo ambayo ujenzi wa barabara unaendelea hivi sasa kwenye maeneo ya Mji wa Mafinaga Mji

NA FREDY MGUNDA,MUFINDI.

SERIKALI ya mkoa wa Iringa imewataka wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) kusitisha ujenzi wa barabara za vumbi zinazoendelea kujengwa na wakandarasi mbalimbali kutokana mvua kubwa zinazoendelea hivi sasa.

Akizungumza kwenye ziara ya Iringa mpya awamu ya pili alipokuwa anakagua ujenzi wa barabara yaKinyanambo, Pareto,Chumi,Lutherani na Mwamkoa Mbagala iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga,mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi aliwataka wakala wa barabara mjini na vijijini (TARURA) kusitisha ujenzi wa barabara hizo kwa kuwa ujenzi huo hauna tija kwa wananchi.

Kipindi hiki mvua zinanyesha kwa wingi kila kona na zimekuwa zikiharibu miundombinu katika maeneo mengi katika mkoa huu wa Iringa,hivyo kutokana na hali hiyo natangaza kusitisha ujenzi wa barabara hizo hadi pale mvua zitakapo isha.

Hapi aliwataka viongozi wa TARURA kuhakikisha wanawasimamia vilivyo wakandarasi wote wanajenga barabara hizo ili zijengwe katika ubora unatakiwa kulingana na thamani ya fedha iliyotolewa na serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

“Hakikisheni mnawasimamia vilivyo wakandarasi hao kwa kuwa fedha zinazotumika ni kodi za wananchi hao ambao mnawaona hapa,hivyo lazima thamani ya fedha hizo ionekane kwa wananchi hawa” alisema Hapi

Hapi aliwataka TARURA kuongeza kasi ya ujenzi wa mitandao ya barabara za lami katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga na ujenzi wa taa za barabarani ili Halmashauri ya Mji wa Mafinga kuwa Manispaa na hatimaye mkoa wa Iringa kuwa Jiji.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliamu aliwataka TARURA  kujenga mitaro yenye ubora unaotakiwa ikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa inamudu maji yote yanayopita na kuzilinda barabara zisiaharibike haraka na zidumu kwa muda mrefu.

“Barabara zetu nyingi za wilaya hii zinaharibika kutokana na kutokuwa na mitaro iliyobora inayohimili maji mengi na ndio maana barabara zinaharibika kila uchwao hizi ni bora kuweni wakali kwa wakandarasi wanaopewa tenda za mitaro kwenye barabara husika” alisema Wiliam

Akijibia hoja za mkuu wa mkoa,mwananchi Inocent Mahanga na mkuu wa wilaya ya Mufindi,meneja wa TARURA Mafinga Tc Injinia Simoni Ngagani alisema kuwa watahakikisha barabara zinajengwa kwenye ubora unatakiwa kulingana na thamani ya fedha za mradi husika.

Tutahakikisha ujenzi wa Mifereji na barabara zinajengwa kwa viwango stahili ili kutumia vilizuri kodi za wananchi


Thursday, 9 January 2020

MTIBWA SUGAR VS YANGA NI KUFA AMA KUPONA.....KOMBE LA MAPINDUZI ...



Leo ni Nusu fainali ya michuano ya Mapinduzi ambapo Yanga watawakabili Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Aman Zanzibar.

Mchezo huo utapigwa jioni ya leo ambapo watani wao wa jadi Simba watashuka Dimbani kumenyana na Mabingwa wa kombe hilo Azam FC na iwapo timu hizo zenye upinzani mkubwa zitakutana fainali basi kwa msimu huuu watakuwa wamekutana mara mbili na huenda wakakutana mara tatu ......

ALIYEMKANA MTANGAZAJI KUJIUNGA NA AZAM FC AJIUNGA AMWAGA WINO AZAM......


 KHLEFFIN Hamdoun, kiungo mshambuliaji aliyekuwa akiitumikia Mlandege ya Zanzibar amemalizana na Azam FC  kwa kusaini kandarasi ya miaka minne.
 
 Kocha Mkuu wa Azam FC, Aristica Cioaba alivutiwa na uwezo wa nyota huyo baada ya kumuona kwenye mchezo wa robo fainali wa Kombe la Mapinduzi ambapo Azam FC  ilishinda kwa bao 1-0.

Katika moja ya mchezo uliochezwa katika michuano ya mapinduzi kati ya Mlandege na Azam Mtangazaji wa Azam Sports Ahmed Ally alimhoji juu ya kuijunga na Azam Khleffin Hamdoun  alikana lakini sasa mambo hadharani.


Huu ni usajili wa kwanza kwa Azam FC msimu huu kwenye dirisha dogo lililofunguliwa mwezi, Desemba 15, 2019.

Tuesday, 31 December 2019

MKULO ASEMA HANA MPANGO WA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KILOSA, MOROGORO 2020



Na Mwandishi Wetu, Morogoro.

Aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Morogoro Mustafa Mkulo (pichani) ameshangazwa na baadhi ya watu kudai anataka kugombea ubunge katika jimbo la Kilosa huku akikanusha hana mpango wowote wa kugombea nafasi hiyo.

Akiongea na waandishi wa habari mjini Morogoro katika salamu za mwaka mpya wa 2020 ikiwa ni sehemu ya kawaida yake kufanya hivyo kila mwisho wa mwaka, Mkulo amesema ajabadilisha maamuzi yake ya kutogombea nafasi ya ubunge na kushangwazwa na baadhi ya watu kudai anataka kuombea tena nafasi hiyo.

“Kuna watu wamekuwa wakidai nataka kugombea tena ubunge Kilosa hizi ni habari za uongo sina mpango wa kugombea ubunge sehemu yoyote ile hapa nchini “ amesema Mkulo.

Mkulo amesema bado anajivunia katika miaka 10 ya ubunge jimbo la Kilosa kwa kutekeleza ilani ya chama kwa kipindi hicho na Wana-Kilosa kuridhika na utendaji wake.

Aidha Waziri waziri huyo mtaafu wa Fedha amesema ataendelea kuwa mwanachama na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hata hivyo amefafanua kuwa pamoja sio mbunge na wala hafikirii kugombea nafasi hiyo lakini ataendelea kutoa mawazo yake kwa CCM na hata kusaidia wasiojiweza kwa niaba ya CCM ili chama kiweze kutekeleza mipango yake ya kimaendeleo.

Katika salamu zake za mwaka 2020 Mkulo amesema anafurahishwa na utendaji kazi mzuri wa Rais wa awamu ya tano Dkt John Pombe Magufuli na anaunga na wanaCCM wengi kutomuingilia katika katika uchaguzi wa kipindi cha pili ya miaka mitano ijayo 2020 hadi 2025 ili aweze kutekeleza kwa ufasaha mipango ya kimaendeleo alioicha katika awamu ya kwanza.

“Huu ni utaratibu wangu wa kila mwaka kutoa salaumu za mwaka mpya tangu nikiwa mbunge na sasa ni wakati wa kusema ukweli Rais Magufuri kwa miaka minne amefanya mengi mazuri anahitaji pongezi kutoka kwa Watanzania hasa katika kupandisha uchumi na kuboresha miundombinu ya nchi hii” amesema Mkulo.

Mustafa Mkulo ni Mbunge Mstaafu ambaye aliongoza kwa miaka 10 katika jimbo la Kilosa ambapo pia katika kipindi hicho alishika nafasi ya Waziri wa Fedha na kuacha kugombea mwenyewe kwa hiari yake katika uchaguzi 2015 na nafasi yake ikachukuliwa na Mbunge wa sasa Mbaraka Bawaziri ambapo amesema maamuzi yake ya kuacha kugombea ni kutoa nafasi wa wanaCCM wengine kuchangia mawazo yao katika kuliletea maendeleo jimbo la Kilosa.

TCAA WAZINDUA MFUMO WA KIDIGITALI WA KUSAIDIA KUTUA NDEGE KATIKA KIWANJA CHA NDEGE CHA MPANDA - KATAVI

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe na Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania,Mizengo Pinda kwa pamoja wakikata utepe kuasharia kuuzindua mfumo wa kidigitali utakaowezesha ndege kutua salama katika Kiwanja cha Ndege Mpanda, Mkoani Katavi. Afisa Muongoza Ndege Mwandamizi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania TCAA Sunday Walinda akimpatia Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe maelezo ya kitaalamu kuhusu mfumo wa kidigitali utakaowezesha ndege kutua salama katika Kiwanja cha Ndege Mpanda, Mkoani Katavi. Rubani wa Shirika la ndege la Tanzania Rubani Hamza akielezea namna mfumo huo ulivyorahisisha hatua za utuaji ndege katika uwanja wa ndege wa Mpanda, Katavi. Viongozi walioketi meza kuu wakipungia ndege ya Shirika la ndege la Tanzania kama ishara ya kuitakia safari njema ilipokuwa ikipaa kutoka uwanja wa ndege wa Mpanda, Katavi. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania, Hamza Johari akielezea mchakato mzima ukinzia na tafiti na hatimaye kubuniwa kwa mfumo huu wa kidigitali wa kuziwezesha ndege kutua salama katika uwanja wa ndege wa Mpanda, Katavi. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe, akielezea kufurahishwa na jitihada zilizofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kufanikisha mfumo huu kukamilika sambamba na kuipongeza mamlaka hiyo kwa kutumia wataalamu wazawa waliobuni mfumo huu katika Kiwanja cha Ndege Mpanda, Mkoani Katavi. Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh Juma Zuberi Homera ameipongeza TCAA kwa kubuni mfumo huu na kusisitiza kuwa wananchi wa Mpanda watumie fursa hii ya ujio wa ndege mara tatu kwa wiki kujiimarisha katika kuwekeza kwani milango ya biashara na wageni zaidi kufika mpanda kwa usafiri wa anga sasa imerahisishwa. Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Mh. Mizengo Pinda akiwachagiza wanaMpanda kuitumia fursa hii ya ujio wa ndege katika wilaya hiyo kujinufaisha kiuchumi.
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube