BREAKING

Thursday 14 March 2019

SIMBA HAITANII!! YAAPA JUMAMOSI ITAKUWA VITA YA KISASI....


Timu ya Simba itakuwa uwanjani kuvaana na AS Vita kwenye mchezo mgumu wa kufuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika siku ya Jumamosi katika Dimba la kisasa la Taifa. 

Kama Simba watashinda mechi hii basi ni asilimia 100 watakuwa wamefuzu kwa lakini pia ni heshima kubwa kwa Tanzania na ukanda huu wa Afrika Mashariki kwa kuwa ndiyo timu pekee iliyobaki.

Kutokana na hali hiyo ni vyema sasa tukabadilika kidogo na kuziunga mkono timu zetu zinazoshiriki
hatua hiyo na hii itakuwa heshima ya pekee kwenye soka la nchi hii. 

Kufuzu kwa Simba ni faida pia kwa Yanga kwa kuwa timu hizo ndiyo kubwa ambazo zinashiriki michuano ya kimataifa mara kwa mara michuano ya kimataifa.

Mashabiki wa Yanga Jumamosi wanatakiwa kuingia uwanjani kwa ajili ya kuiunga mkono Simba ili kuliletea taifa sifa kubwa. 

Kwenda na kuishangilia Vita haliwezi kuwa jambo zuri kwa
kuwa wote ni Watanzania na tunatakiwa kuhakikisha tunaweka uzalendo mbele zaidi ya mambo mengine yote kama ambavyo yamekuwa yakifanya mataifa mengine ambayo yameendelea kisoka.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube