BREAKING

Friday 29 March 2019

WASHINDI 15 WAPATIKANA KATIKA PROMOSHENI YA TIA KITU PATA VITUZ NA DSTV

 Mkuu wa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania Johnson Mshana (Kushoto) Akizungumza wakati wa droo ya tano ya Promosheni ya Tia Kitu pata vituz, Kulia ni Afisa wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Jehud Ngolo.   Promosheni hiyo ni ya muda wa wiki 8 ambapo jumla ya washindi 120 watapatikana.


    
Photos: Mkuu wa Uhusiano MultiChoice Tanzania Johnson Mshana (Wa pili kushoto) akiongoza droo ya kupata washindi wa wiki ya 5  katika promosheni  ya Tia kitu pata vituz ya DStv . Kulia  Afisa Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Jehud Ngolo , kushoto ni Afisa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania akifuatiwa na Benson Urio wa kitengo cha Teknohama cha DStv. Promosheni hiyo ni kwa wateja wanaolipia kwa wakati kabla vifurushi vyao havijakatika hivyo kupata fursa ya kushinda kifurushi cha miezi miwili. Promosheni hiyo ni ya muda wa wiki 8 ambapo jumla ya washindi 120 watapatikana.

 Kampuni ya inayoongoza kwa huduma bora za vinga’muzi nchini, DStv  imetangaza washindi 15 wa  droo ya 5 ya  Promosheni hiyo ya wiki nane inayoendelea  nchi nzima maarufu kama “ Tia Kitu pata vituz”.
Promosheni hiyo ni ya wazi kwa wateja wote wa DStv ambao watalipia vifurushi vyao kabla havijakatika. “Mteja yeyote wa DStv atakayelipia kifurushi chake kabla hakijakatika moja kwa moja anaingia katika droo na fursa ya kujishindia kifurushi chake kwa muda wa miezi miwili.” Alieleza Mkuu wa Uhusiano MultiChoice Tanzania Johnson Mshana wakati akiendesha  droo ya wiki ya nne ya promosheni hiyo.
Akizungumza  baada ya kufahamishwa juu ya ushindi wake huo Bw. Yohana Francis ambaye ni mteja wa DStv aliyepo mkoani Mbeya alisema kuwa amefurahi sana kuibuka mshindi na kuongeza kuwa anaishukuru sana DStv na kuwaasa kuwa waendelea kuwajali wateja wake hivyo hivyo.

Friday 22 March 2019

RAYVAN AMKAMATA WAZIRI MWAKYEMBE KUELEKEA MECHI YA STARS NA UGANDA KUFUZU AFCON SIKU YA JUMAPILI

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe jana alibaki na mshangao baada ya kumuona msanii wa bongo fleva Raymond Shaban akirekodi wimbo video ya wimbo wake maalumu kwa ajili ya hamasa kwa timu ya Taifa ya Tanzania.

Mwakyembe ambaye alitia timu Uwanjani hapo kwa ajili ya kuwapa hamasa wachezaji alikuwa hajajua kama Rayvany, anayesumbua na wimbo wake wa 'tetema' kama angetunga wimbo maalumu wa hamasa na kurekodi video yake kwenye Uwanja wa Taifa.



Mwakyembe alifurahishwa na kitendo hicho na amesema kuwa kutokana na sapoti ambayo Starz wanaipata kutoka kwa kila mtanzania wanapaswa wapambane kwa vitendo Uwanjani ili kutimiza ndoto za wengi wapenda mpira.

"Ni zamu yetu sasa Tanzania, kuweza kufikia malengo na ndoto za wengi hivyo tuungane na kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa kuipa sapoti timu yetu na jambo jema linalofanywa na wasanii kuimba nyimbo maalumu kwa ajili ya kuisapoti timu yetu, hivyo hata Rayvany naye anatakiwa awepo Uwanjani Jumapili," amesema Mwakyembe.

Stars imeweka kambi bongo safari hii huku wapinzani wao Uganda wajiongozwa na nyota Emanuel Okwi wakijichimbia Misri kwa ajili ya mchezo huu utakaopigwa Uwanja wa Mkapa Jumapili.


DSTV YATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA PROMOSHEN YA TIA KITU PATA VITUZ!

 Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo akichezesha droo ya kupata washindi wa huku Afisa Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Humudi Semvua  (kulia) akifuatilia kwa makini. Kushoto ni Benson Urio wa kitengo cha Teknohama cha DStv. Promosheni hiyo ni kwa wateja wanaolipia kwa wakati kabla vifurushi vyao havijakatika hivyo kupata fursa ya kushinda kifurushi cha miezi miwili. Promosheni hiyo itaendelea kwa wiki 8 ambapo jumla ya washindi 120 watapatikana.

z!


Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo (Katikati) Akizungumza kwa ismu na moja ya washindi wa promosheni hiyo.  Kulia ni Afisa wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Humudi Semvua  na kushoto ni Afisa Uhusiano Grace  Mgaya  Promosheni hiyo ni kwa wateja wanaolipia kwa wakati kabla vifurushi vyao havijakatika hivyo kupata fursa ya kushinda kifurushi cha miezi miwili. Promosheni hiyo itaendelea kwa wiki 8 ambapo jumla ya washindi 120 watapatikana.
 Kampuni ya inayoongoza kwa huduma bora za vinga’muzi nchini, DStv  imetangaza washindi 15 wa  droo ya 4 ya  Promosheni hiyo ya wiki nane inayoendelea  nchi nzima maarufu kama “ Tia Kitu pata vituz”.

Promosheni hiyo ni ya wazi kwa wateja wote wa DStv ambao watalipia vifurushi vyao kabla havijakatika. “Mteja yeyote wa DStv atakayelipia kifurushi chake kabla hakijakatika moja kwa moja anaingia katika droo na fursa ya kujishindia kifurushi chake kwa muda wa miezi miwili.” Alisema Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Shelukindo wakati wa kufanya droo ya wiki ya nne ya promosheni hiyo.

Akizungumza  baada ya kufahamishwa juu ya ushindi wake huo Bw. Issa Mohammed ambaye ni mteja wa DStv aliyepo mkoani Dar es Salaam alisema kuwa amefurahi sana kuibuka mshindi na kuongeza kuwa anaishukuru sana DStv na kuwaasa kuwa waendelea kuwajali wateja wake hivyo hivyo.


Thursday 14 March 2019

ZANA COULIBALY BEKI WA SIMBA ASIYEISHA VITUKO....


SIMBA HAITANII!! YAAPA JUMAMOSI ITAKUWA VITA YA KISASI....


Timu ya Simba itakuwa uwanjani kuvaana na AS Vita kwenye mchezo mgumu wa kufuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika siku ya Jumamosi katika Dimba la kisasa la Taifa. 

Kama Simba watashinda mechi hii basi ni asilimia 100 watakuwa wamefuzu kwa lakini pia ni heshima kubwa kwa Tanzania na ukanda huu wa Afrika Mashariki kwa kuwa ndiyo timu pekee iliyobaki.

Kutokana na hali hiyo ni vyema sasa tukabadilika kidogo na kuziunga mkono timu zetu zinazoshiriki
hatua hiyo na hii itakuwa heshima ya pekee kwenye soka la nchi hii. 

Kufuzu kwa Simba ni faida pia kwa Yanga kwa kuwa timu hizo ndiyo kubwa ambazo zinashiriki michuano ya kimataifa mara kwa mara michuano ya kimataifa.

Mashabiki wa Yanga Jumamosi wanatakiwa kuingia uwanjani kwa ajili ya kuiunga mkono Simba ili kuliletea taifa sifa kubwa. 

Kwenda na kuishangilia Vita haliwezi kuwa jambo zuri kwa
kuwa wote ni Watanzania na tunatakiwa kuhakikisha tunaweka uzalendo mbele zaidi ya mambo mengine yote kama ambavyo yamekuwa yakifanya mataifa mengine ambayo yameendelea kisoka.

UWANJA WA SOKA WA KISASA ULIVYOINUA DODOMA ....


Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na timu ya wataalamu wa Tanzania na Misri wanaoshughulikia ujenzi wa uwanja wa michezo katika Jiji la Dodoma, unaotarajiwa kujengwa kwa msaada wa Mfalme wa Morocco, Mtukufu Mohammed VI.

Balozi wa Morocco hapa nchini aliyeongoza ujumbe wa wataalamu kutoka Morocco Abdelilah Benryane amesema pamoja na kuzungumzia uhusiano mzuri wa Tanzania na Morocoo wamejadiliana kuhusu utekelezaji wa miradi iliyokubaliwa wakati wa ziara ya Mfalme wa Morocco hapa nchini mwaka 2016 ikiwemo ujenzi wa Msikiti wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) unaojengwa Jijini DSM na kuanza kwa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Patrick Mfugale amesema uwanja huo utajengwa eneo la Nanenane kando ya barabara ya Dodoma – Morogoro, utajengwa kwa mfano wa mlima Kilimanjaro na utakuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji kati ya 85,000 na 100,005.

Wednesday 6 March 2019

TANZANIA YAIBUKA KIDEDEA TUZO ZA KIMATAIFATA


Mkuu wa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania Johnson Mshana (Kulia) na Afisa Uhusiano wa kampuni hiyo Grace Mgaya (kushoto) wakikabidhi seti ya DStv kwa mkuu wa shule ya sekondari St Mary Goretti Sr. Lucrecia Njau na mshindi wa tuzo za kimataifa za DStv Eutelsat Star Awards Pricilla Marealle wakati wa mahafali ya kidato cha sita katika shule ya St Mary Goretti hivi karibuni. Pricilla aliibuka mshindi wa kwanza katika tuzo hizo na kuwashinda wanafunzi kutoka nchi zaidi ya 10 kote barani Afrika. Mbali na kutunukiwa cheti maalum, Pricilla atapata fursa ya kutembelea kituo cha Anga cha Afrika Kusini na makao makuu ya MultiChoice jijini Johannesburg wakati shule yake imepata cheti na zawadi ya kufungiwa huduma ya DStv.




Mkuu wa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania Johnson Mshana akimkabidhi mshindi wa tuzo za kimataifa za DStv Eutelsat Star Awards Pricilla Marealle cheti cha ushindi wakati wa mahafali ya kidato cha sita katika shule ya St Mary Goretti hivi karibuni. Kulia ni Afisa Uhusiano  wa MultiChoice Tanzania. Grace Mgaya. Pricilla aliibuka mshindi wa kwanza katika tuzo hizo na kuwashinda wanafunzi kutoka nchi zaidi ya 10 kote barani Afrika. Mbali na kutunukiwa cheti maalum, Pricilla atapata fursa ya kutembelea kituo cha Anga cha Afrika Kusini na makao makuu ya MultiChoice jijini Johannesburg. 
 Mkuu wa shule ya  St Mary Goretti Sr. Lucrecia Njau akifurahi baada ya kupokea cheti kutoka kwa Mkuu wa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania Johnson Mshana mara baada ya shule hiyo kufanikiwa kutoa mshindi wa jumla wa wa tuzo za kimataifa za DStv Eutelsat Star Awards Pricilla Marealle. Pricilla aliibuka mshindi wa kwanza katika tuzo hizo na kuwashinda wanafunzi kutoka nchi zaidi ya 10 kote barani Afrika. Mbali na kutunukiwa cheti maalum, Pricilla atapata fursa ya kutembelea kituo cha Anga cha Afrika Kusini na makao makuu ya MultiChoice jijini Johannesburg
 
 Mshindi wa Jumla wa tuzo za kimataifa za DStv Eutelsat Star Awards Pricilla Marealle akikabidhiwa kikombe cha ushindi na Mkuu wa shule ya St Mary Goretti Sr. Lucrecia Njau baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa jumla wa wa tuzo za kimataifa za DStv Eutelsat Star Awards. Kulia ni Mkuu wa Uhusiano wa MultiChoice Tanzania Johnson Mshana. Pricilla aliibuka mshindi wa kwanza katika tuzo hizo na kuwashinda wanafunzi kutoka nchi zaidi ya 10 kote barani Afrika. Mbali na kutunukiwa cheti maalum, Pricilla atapata fursa ya kutembelea kituo cha Anga cha Afrika Kusini na makao makuu ya MultiChoice jijini Johannesburg.
 

Mshindi wa Jumla wa tuzo za kimataifa za DStv Eutelsat Star Awards Pricilla Marealle akifurahi na wazazi wake Calvin Marealle  na Jamila Marealle mara baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi. Pricilla aliibuka mshindi wa kwanza katika tuzo hizo na kuwashinda wanafunzi kutoka nchi zaidi ya 10 kote barani Afrika. Mbali na kutunukiwa cheti maalum, Pricilla atapata fursa ya kutembelea kituo cha Anga cha Afrika Kusini na makao makuu ya MultiChoice jijini Johannesburg.



Kwa mara nyingine tena Tanzania imeibuka kinara  katika tuzo za kimataifa za wanafunzi zijulikanazo kama DStv Eutelsat Star Awards ambapo mwanafunzi Priscilla Marealle kutoka shule ya sekondari ya St. Mary Goreti mkoani Kilimanjaro ameweza kuipeperusha bendera ya Tanzania kwa kunyakua nafasi ya kwanza katika kipengele cha uchoraji bango  ikiwa ni baada ya mchuano mkali baina ya mamia ya wanafunzi kutoka nchi zaidi ya 10 kote barani Afrika. 
Kwa upande wa uandishi wa insha kijana Tanaka Chonyera kutoka  nchini Botswana aliweza kujinyakulia ushindi wa kwanza.

Tuzo hizi ambazo huhusisha uandishi wa insha maalum au kuandaa bango yenye ujumbe kuhusiana na elimu ya anga hususan Setelait ni za wazi kwa wanafunzi wote wa shule za sekondari wenye umri kati ya miaka 14 – 19 kote barani Afrika ambapo kampuni ya MultiChoice inaendesha shughuli zake.

Katika msimu huu wa nane, washindani walitakiwa kuandika insha au kubuni bango litakaloelezea licha ya Satelait kutumika katika shughuli mbalimbali, ni namna gani zitaweza kutumika zaidi ili kuleta maendeleo chanya ulimwenguni.

Priscilla ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha sita wa mchepuo wa Sayansi katika shule ya Mtakatifu Maria Goreti alitangazwa rasmi kuwa mshindi mjini Accra nchini Ghana ambapo ndipo jopo la watahini liliongozwa na Paolo Nespoli, mwanaanga nguli kutoka European Space Agency (ESA) lilikaa kupitia kazi kutoka kwa wanafunzi walioshinda katika nchi mbalimbali. 

Akiongea baada ya kukabidhiwa cheti cha uthibitisho wa ushindi wakati wa mahafali ya kidato cha sita ya shule ya Mtakatifu Mary Goreti iliyopo Moshi Kilimanjaro, Priscilla amesema amefurahi sana kwa ushindi huo mkubwa ambao umemletea yeye, shule yake na taifa zima kwa ujumla sifa kubwa. “Nimefurahi sana kupokea taarifa hizi nzuri. Naamini ushindi wangu utakuwa ni chachu kubwa kwa wanafunzi wenzangu kote nchini kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika tuzo kama hizi na mashindano mengine ya kitaaluma ya ndani na nje ya nchi, na kusisitiza  kuwa Ndoto huanza kufanya kazi pale unapojiamini” alisema Priscilla.

Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo ya Mtakatifu Maria Goreti Sister Lucresia Njau alisema kuwa anaishukuru sana kampuni ya MultiChoice Tanzania kwa kuwapatia nafasi ya kushiriki katika Mashindano hayo na hatimaye kuweza kunyakua tuzo hiyo kupitia mwanafunzi wao Priscilla.

“Huyu kijana ana jitahidi sana katika chochote kile anachokifanya, iwe ni darasani au hata katika majukumu mengine nje ya darasani. Ni msikivu mtiifu lakini zaidi ya yote ni mbunifu sana. Naamini haya ndiyo yaliyomfanya aweze kushinda tuzo hizi” alisema Sr. Lucrecia Njau.

Naye, Mkuu wa Uhusiano MultiChoice Tanzania Johnson Mshana alisema,” Huu ni msimu wa tatu mfululizo kwa Tanzania kuendelea kung’ara katika tuzo hizi za DStv Star Awards. Tulianza kupeperusha bendera yetu na kijana Davids Bwana msimu wa sita baada ya kushika nafasi ya pili Afrika katika kipengele cha uandishi wa insha, kisha tukaibuka kidedea baada ya kupokea taarifa za ushindi wa kwanza wa kijana Taheer Rashid katika msimu wa saba mwaka jana na leo hii tunayofuraha kubwa kuona kuwa tumeendeleza wimbi la ushindi.”

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya Pricilla kutangazwa kuwa mshindi, walimu na wazazi wa mwanafunzi huyo wa kidato cha sita mwenye umri wa miaka 19, wamesema kuwa wanamfahamu vyoma Pricilla kuwa ni kijana mwenye kupenda kujibidisha sana katika masuala ya kitaaluma na kijamii hivyo ushindi wake ni kitu kilichotarajiwa na kwamba wanaamini kuwa anastahili ushindi huo.
Pamoja na kupata cheti maalum cha ushindi, Pricilla atapata fursa (Yeye na Mzazi au mlezi) ya kutembelea kitua cha Anga cha Afrika Kusini na pia kutembelea makao makuu ya MultiChoice jijini Johannesburg kama mgeni maalum wa DStv  huku shule aliyotoka ikipata zawadi ya cheti pamoja na kufungiwa huduma ya DStv.
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube