BREAKING

Thursday 28 July 2016

SIMBA USO KWA USO NA TIMU YA KOCHA WAO WA ZAMANI LOGA...KUTOKA ANGOLA SIMBA DAY


Viongozi na wanachama mbalimbali wa Simba watachangia damu katika hospitali mbalimbali nchini kauli iliyotolewa na Rais wa Simba, Evans Aveva ambapo amesema watafanya hivyo ikiwe ni sehemu ya kuadhimisha wiki ya Simba kwenda kusherekea miaka 80 ya klabu hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Aveva amesema Siku kamili ya sherehe itakuwa ni Agosti 8 ikiwa ni kawaida ya klabu hiyo kufanya tamasha la Simba Day ambalo hufanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijiji Dar es Salaamm

Simba wamekuwa wakifanya Tamasha hilo likiwa ni sehemu pia ya kuwatambulisha wachezaji wao wapya waliowasajili kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania bara, utamaduni ambao wamekuwa wakiufanya kila mwaka.

Aveva ameeleza pia katika wiki nzima ambayo watakuwa wakifanya kazi za kijamanii watatumia muda huo kuzngumza na wanachama wao juu ya mstakabali wa timu yao na kuhakikisha inafanya vyema katika msimu mpya unaoaanza mapema mwezi Agosti.


Simba pia itamenyana na timu ya aliyekuwa kocha wao wa zamani anayekinoa kikosi cha Girabola Zdravko Logarusic

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube