BREAKING

Monday, 25 January 2021

BALOZI WA UINGEREZA APONGEZA UBORA WA MAJI YA MKWAWA MKOANI IRINGA


Balozi wa uingereza nchini Tanzania David Concar akinywa maji yanayozalishwa na kiwanda cha Mkwawa kilichopo mkoani Iringa akiwa sambamba na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard kasesela akiwa na wadau mbalimbali  wanaokuwanywa maji hapoBalozi wa uingereza nchini Tanzania David Concar amekipongeza kiwanda cha Mkwawa cha uzalishaji wa bidhaa ya maji yenye ubora kwa matumizi ya binadam yeyeto yule

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akitoa maelezo kwa Balozi wa uingereza nchini Tanzania David Concar juu ya ubora wa kiwanda cha Mkwawa cha uzalishaji wa bidhaa ya maji yenye ubora kwa matumizi ya binadam yeyeto yule.

Na Fredy Mgunda,Iringa.

Balozi wa uingereza nchini Tanzania David Concar amekipongeza kiwanda cha Mkwawa cha uzalishaji wa bidhaa ya maji yenye ubora kwa matumizi ya binadam yeyeto yule wa ndani na nje ya nchi ya Tanzania.

Akizungumza wakati alipotembelea banda la maji ya kunywa la kiwanda cha Mkwawa wakati wa maonyesho ya kibiashara ya mkoani Iringa yaliyofanyika katika chuo cha Mkwawa balozi David Concar alisema kuwa amepongeza uzalishaji bora wa maji hayo ambayo yamekidhi vigezo vyote vinavyohitajika kwa afya ya binadamu.

Balozi Concar alisema kuwa amekunywa maji hayo na kugundua kuwa yanaradha ya maji hayo ambayo anaamini kuwa kila mtu atayeonja maji hayo lazima avutiwe kwa namna yalivyokuwa bora.

Alisema kuwa amevutiwa na bidhaa hiyo ya maji ya kunywa ya kampuni ya Mkwawa na kuahidi kuitangaza kokote Kule atakapokuwa ametembea kutoka na kuvutiwa na jinsi ya uzalishwaji wake ulivyokuwa na bora wa kimataifa.

Balozi Concar aliwataka wamiliki wa kiwanda hicho cha uzalishaji wa maji kuhakikisha wanatanua na kijitangaza zaidi kitaifa na kimataifa kwa sababu ametembea kwenye super market nyingi hajaona maji ya kampuni hiyo ambayo yeye anaamni kuwa in maji bora hapa nchini.

Akiwa ameambatana na balozi wa uingereza nchini Tanzania, mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alisema kuwa amekuwa balozi wa kujitegemea kuyatangaza maji hayo kila kona ya Tanzania kutokana na ubora wake.

Alisema kuwa anamuomba balozi huyo Nate awe balozi wa kutangaza maji yanayozalishwa na kiwanda cha Mkwawa kutokana na ubora wake ambao maji hayo yanayo.

Kasesela aliwataka viongozi wa kiwanda hicho kuhakikisha wanatanua wigo wa masoko ya bidhaa hiyo ya maji ya kampuni ya uzalishaji wa maji ya Mkwawa inayopatikana mkoani Iringa wilaya ya Iringa.

Alisisitiza wananchi wa mkoa wa Iringa na nje ya mkoa wa Iringa kuendelea kunywa maji safi na salama yanayozalishwa na kiwanda cha Mkwawa kilichopo mkoani Iringa kutokana na ubora wake.

Kwa upande wao baadhi ya wanachi mkoani Iringa waliohudhulia katika maonyesho hayo yaliyofanyikia katika chuo cha Mkwawa waliyapongeza maji hayo safi na salama kwa kunywa kutokana na ubora wake.

Walisisistiza kuwa wataendelea kunywa maji hayo yaliyokuwa na ubora wa hali ya juu lakini wanatakiwa kuhakikisha wanaulinda na kuuboresha ubora wake ambao upo hadi hivi sasa.

Wednesday, 20 January 2021

ZLATAN APIGA ZOTE AC MILAN YASHINDA 2-0 NA KUPAA KILELENI



Zlatan Ibrahimovic jana amefunga mabao yote mawili dakika ya saba kwa penalti na 52, AC Milan ikiichapa Cagliari 2-0 katika mchezo wa Serie A Uwanja wa Sardegna Arena, Cagliari.
Sasa AC Milan inafikisha pointi 43 na kuendelea kuongoza Serie A  kwa pointi tatu zaidi ya mahasimu wao wa Jiji, Inter Milan (43-40) baada ya wote kuchezsa mechi 18


AC Milan beat Cagliari in their Serie A clash on Monday evening to reopen a three-point gap
Striker Zlatan Ibrahimovic scored twice on his first Serie A start since returning from injury
Milan are on 43 points, three ahead of city rivals Inter Milan, and 10 clear of Juventus in fifth




OZIL ANA KWA ANA NA MTANZANIANIA MBWANA SAMATTA - UTURUKI

Mesut Ozil amesaini kujiunga na klabu ya soka ya  Fenerbahce, akiondoka ndani ya washika mitutu wa London Arsenal baada ya kudumu ndani ya Arsenal kwa mika saba na nusu. 

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu tangu kuwasili kwa kocha wa Arsenal Mikel Arteta ambaye alionekana kutokwenda sawa na kocha huyo ambaye pia aliwahi kucheza naye kabla ya kustaafu kandanda.

Mesut Ozil poses with a Fenerbahce scarf after touching down in Istanbul on Sunday night

Ozil

Ozil earlier shared a snap of him and his family on a plane with Fenerbahce flags behind him

Mesut Ozil aliposafiri na familia yake kujiunga na klabu yake mpya ya  Fenerbahce Istanbul -Uturuki The playmaker is greeted by airport staff as he arrives to complete his Fenerbahce move

Kiungo Mahiri Ozil akiwasili Uwasili Uturuki

Mesut Ozil has brought his time at Arsenal to an end and joined Turkish club Fenerbahce


The German playmaker was the club's record signing when he moved from Real Madrid in 2013

Picha mojawapo aliyopiga na kocha wa zamani wa Arsenal Arsene Wenger baada ya kusaini kuichezea timu hiyo mwaka 2013 akitokea Real Madrid 

Tuesday, 19 January 2021

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI-DODOMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Seikali ya Mapinduzi Zanzibar  Mhe. Tabia Maulid Mwita na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Abdalla Ulega baada ya Kufungua Maadhimisho ya Siku ya kiswahili katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma Leo Januari 19,2021.  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi, Wajumbe, Wadhamini na Wafanyakazi wa  Taasisi za Kiswahili baada ya Kufungua Maadhimisho ya Siku ya kiswahili katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma Leo Januari 19,2021.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Vitabu vya Mkakati na Muongozo wa kufundishia Lugha ya Kiswahili kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili yaliyoadhimishwa leo Januari 19,2021 katika Ukumbi wa Hazina Jijini DodomaMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma leo Januari 19,2021.

 

Monday, 18 January 2021

RAIS MAGUFULI AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MULEBA -MKOANI KAGERA


    

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Muleba wakati akiwa njiani kuelekea Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 17 Januari 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli  akizungumza na Wananchi wa Kemondo wakati akieleka Bukoba mjini mkoani Kagera leo tarehe 17 Januari 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli  akizungumza na Wananchi wa Kemondo wakati akieleka Bukoba mjini mkoani Kagera leo tarehe 17 Januari 2021

RAIS MAGUFULI KUZINDUA SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA YA IHUNGO...

Huu ndio muonekano wa Shule ya Sekondari ya wavulana Ihungo iliyoko Bukoba Mkoani Kagera inayotarajiwa kuzinduliwa na Mhe.Rais Dkt.John Pombe Magufuli Januari 18 mwaka huu wa 2020. kufuatiwa ukarabati kukamilika ambao umegharimu shilingi Bilioni 10.9 

   


Saturday, 16 January 2021

MLETE MWANAO KWA BABA MZAZI LAWENA NSONDA HOLYLA APATE MAARIFA ,MAZINGIRA BORA AFYA BORA...






 

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube