Balozi wa uingereza nchini Tanzania David Concar amekipongeza kiwanda cha Mkwawa cha uzalishaji wa bidhaa ya maji yenye ubora kwa matumizi ya binadam yeyeto yule wa ndani na nje ya nchi ya Tanzania.
Monday, 25 January 2021
BALOZI WA UINGEREZA APONGEZA UBORA WA MAJI YA MKWAWA MKOANI IRINGA
Wednesday, 20 January 2021
ZLATAN APIGA ZOTE AC MILAN YASHINDA 2-0 NA KUPAA KILELENI
Zlatan Ibrahimovic jana amefunga mabao yote mawili dakika ya saba kwa penalti na 52, AC Milan ikiichapa Cagliari 2-0 katika mchezo wa Serie A Uwanja wa Sardegna Arena, Cagliari.
Sasa AC Milan inafikisha pointi 43 na kuendelea kuongoza Serie A kwa pointi tatu zaidi ya mahasimu wao wa Jiji, Inter Milan (43-40) baada ya wote kuchezsa mechi 18



OZIL ANA KWA ANA NA MTANZANIANIA MBWANA SAMATTA - UTURUKI
Mesut Ozil amesaini kujiunga na klabu ya soka ya Fenerbahce, akiondoka ndani ya washika mitutu wa London Arsenal baada ya kudumu ndani ya Arsenal kwa mika saba na nusu.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu tangu kuwasili kwa kocha wa Arsenal Mikel Arteta ambaye alionekana kutokwenda sawa na kocha huyo ambaye pia aliwahi kucheza naye kabla ya kustaafu kandanda.

Ozil

Mesut Ozil aliposafiri na familia yake kujiunga na klabu yake mpya ya Fenerbahce Istanbul -Uturuki 
Kiungo Mahiri Ozil akiwasili Uwasili Uturuki


Picha mojawapo aliyopiga na kocha wa zamani wa Arsenal Arsene Wenger baada ya kusaini kuichezea timu hiyo mwaka 2013 akitokea Real Madrid
Tuesday, 19 January 2021
MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI-DODOMA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Seikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Abdalla Ulega baada ya Kufungua Maadhimisho ya Siku ya kiswahili katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma Leo Januari 19,2021.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi, Wajumbe, Wadhamini na Wafanyakazi wa Taasisi za Kiswahili baada ya Kufungua Maadhimisho ya Siku ya kiswahili katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma Leo Januari 19,2021.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Vitabu vya Mkakati na Muongozo wa kufundishia Lugha ya Kiswahili kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili yaliyoadhimishwa leo Januari 19,2021 katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma leo Januari 19,2021.
Monday, 18 January 2021
RAIS MAGUFULI AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MULEBA -MKOANI KAGERA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Muleba wakati akiwa njiani kuelekea Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 17 Januari 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Kemondo wakati akieleka Bukoba mjini mkoani Kagera leo tarehe 17 Januari 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Kemondo wakati akieleka Bukoba mjini mkoani Kagera leo tarehe 17 Januari 2021
RAIS MAGUFULI KUZINDUA SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA YA IHUNGO...
Huu ndio muonekano wa Shule ya Sekondari ya wavulana Ihungo iliyoko Bukoba Mkoani Kagera inayotarajiwa kuzinduliwa na Mhe.Rais Dkt.John Pombe Magufuli Januari 18 mwaka huu wa 2020. kufuatiwa ukarabati kukamilika ambao umegharimu shilingi Bilioni 10.9















