BREAKING

Monday 25 November 2019

KLOPP PRESHA YASHUKA KWA MO SALAH NI KUELEKEA MCHEZO WA LIGI YA MABINGWA JUMATANO



Kocha mkuu wa Liverpool Klopp,  amethibitisha kuwa mshambuliaji wake Mohamed Salah atarejea uwanjani Jumatano kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Napol.

Salah raia wa Misri alikosa mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Crystal Palace ambao Liverpool ilishinda mabao 2-1 na kuifanya izidi kujikita kileleni ikiwa na pointi 37 kwenye msimamo  kutokana na kusumbuliwa na majeruhi.
.
Klopp amesema kuwa Salah alikuwa fiti kuivaa Crysytal Palace kutokana na hali yake kuimarika ila aliamua kumpumzisha kwa ajili ya kazi nzito ya jumatano dhidi ya Napol.

“Salah yupo vizuri na ilibidi aanze kwenye mchezo dhidi ya Crystal Palace niliamua nimpe mapumziko ila mwisho wa siku mchezo wetu tulishinda kwani hakuwa na timu kwa muda wa siku nane alikuwa nchini Misri na mabao yalifungwa na Robert Firmino na Sadio Mane.
“Tulipaswa kufanya changuo la kumuanzisha ama kumuacha apumzike tukakubaliana tumpumzishe atarejea uwanjani Jumatano kukabiliana na Napol,” amesema Klopp.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube