BREAKING

Friday 26 July 2019

KATIKA MAKOCHA 100 WANAOOMBA KUINOA TAIFA STARS HAKUNA KOCHA HATA MMOJA MZAWA, JE NI UOGA AMA MASILAHI KIDUCHU?



Wilfredy Kidao, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) amesema kuwa mpaka sasa tayari wamepokea maombi ya makocha 100 wanaotaka nafasi ya kuinoa timu ya Taifa.

Katika orodha hiyo hakuna hata jina moja la mzawa ambaye ameomba kuinoa timu ya Taifa ya Tanzania baada ya 
Kocha Mkuu Emmanuel Ammunike  kusitishiwa mkataba wake baada ya kuboronga kwenye michuano ya Afcon 2019 nchini Misri.

 "Tumepokea maombi ya makocha zaidi ya 100 wakitaka kazi ya kuifundisha timu ya Taifa, maombi ni mengi na tunayafanyia kazi.

 "Kwa sasa nguvu zeru tunazielekeza kwenye michuano ya Chan na kwenye maombi hayo 100 hakuna mzawa hata mmoja," amesema.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube