BREAKING

Friday, 10 January 2025

NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO



 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt Doto Biteko amekerwa na utendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akitoa maagizo uongozi wa kituo cha miito ya simu (call centre) ufumuliwe.


Maagizo ya Dk Biteko kwa Tenesco ni kufuatia kutotekelezwa kwa maagizo yake ya aliyoyatoa mwaka jana ya kuwepo kwa namba ya mawasiliano ya wateja isiyolipiwa ambapo itamwezesha mteja kupiga simu bila kukatwa salio  agizo ambalo halijatekelezwa.

Dkt Biteko ameyatoa maagizo hayo  baada ya kutembelea kituo cha miito ya simu Tanesco ambapo amesema watendaji wa shirika hilo wamezoea kazi.



No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube