BREAKING

Friday 22 May 2020

LAMPARD HANA NENO NA KANTE,KUJITENGA KUTAZAMA AFYA YAKE






Kocha Mkuu wa Chelsea, Frank Lampard amesema kuwa uamuzi wa kiungo wake N'Golo Kante kujitenga na wenzake ni mzuri kwa manufaa yake na afya za wengine pia.

Kante aliripoti mazoezini siku ya Jumanne katika kituo cha Cobham HQ ila alishindwa kurejea siku ya Jumatano kutokana na kutojihisi vizuri.

Kwa sasa timu nyingi zinazoshiriki Ligi Kuu England zimeanza maandalizi ya kufanya mazoezi ya pamoja kwa ajili ya kumalizia mechi zilizobaki baada ya ligi kusimamishwa kutokana na janga la Virusi vya Corona .

Habari zinaeleza kuwa sababu kubwa ya Kante kushindwa kuendelea kuripoti mazoezini ni hofu ya kupata maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo bado vinasambaa kwa kasi.

RAIS MAGUFULI ARUHUSU MICHEZO NA VYUO JUNI MOSI....


Rais wa Tanzania, John Magufuli ametangaza kuwa vyuo vikuu nchini humo vitafungufuliwa Juni Mosi, na kuruhusu pia shughuli zote za michezo nazo ziendelee kama kawaida.
Rais Magufuli amesema vyuo vikuu vyote sasa vitarejea katika hali yake ya kawaida kuendelea na masomo kuanzia Juni Mosi baada ya kijiridhisha kutokana na maendeleo ya hali ya maambukizi ya virusi vya corona.
Amesema maambukizi nchini humu yameshuka kwa kiwango cha kuridhisha hatua ambayo imemfanya aanze kufungua baadhi ya shughuli zilizokuwa zimesimama kutokana na janga hilo la virusi vya corona lilipopiga hodi kwa mara ya kwanza nchini Machi 16.
"Ikiwa mwelekeo nnaouona utandelea katika wiki zijazo, napanga kufungua vyuo vikuu ili wanfunzi waendelee na masomo yao, alisema Magufuli wakati akizungumza kwenye ibada ya misa kaskazini-magharibi mwa nchi wiki iliyopita.
Hatua nyingine ambazo Rais Magufuli amezitangata wakati alipokuwa akiwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni ni kuwaruhusu wanafunzi wa kidato cha sita wanaojiandaa na mitihani ya kuhitimu masomo yao kurejea shuleni.
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube