BREAKING

Tuesday 29 December 2015

MAKONTENA MENGINE 11,884 YAGUNDULIKA KUPOTEA,Proffessa MAKAME MBARAWA,AAGIZA KUSAKWA KWA WEZI NANE WALIOKIMBIA







Wafanyakazi wanane wa mamlaka ya bandari kitengo cha makasha ya bidhaa,yaani CONTAINER'S,wamekimbia ajira zao kufuatia serikali kuwakamata wenzao 7 wanaotuhumiwa kuwa vinara wa kuikosesha serikali mapato kwa kuyapitisha kinyemela makasha hayo bila ya kulipiwa ushuru wa forodha.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari leo asubuhi bandarini hapo,waziri wa uchukuzi,ujenzi na mawasiliano,Proffessa MAKAME MBARAWA,alisema kuwa wafanyakazi hao walikimbia baada ya tume maalum iliyoundwa ili kufuatilia upotevu wa makasha hapo bandari na kugundua makasha 300 hayaonekani kama yamepitia njia sahihi za kutolewa katika bandari kavu,kugundua kuwa kuna mengine 11,884 yalipotea kwa mtindo uleule wa yale ya awali.

Amesema inaonekana kuwa wafanyakazi hao walikuwa na ushirikiano na mawakala wa makasha wasiokuwa waaminifu kwa kushirikiana kuidanganya mamlaka ya mapato nchini,TRA,ikishirikiana na wafanyakazi wasio waaminifu wa TRA,pamoja na mamlaka ya Bandari kuhusu ulipaji wa WHARFAGE(TOZO YA BANDARI) huku wakijua kuwa ni kosa.


Aidha amesema kuwa mawakala wa forodha 243 wamepewa siku 7 kukamilisha malipo ya makasha na magari yaliyotolewa bandarini hapo bila ya kulipiwa tozo ya bandari kufanya hivyo katika muda huo vinginevyo serikali italazimika kuwakamata na kuwafikisha polisi ili walipe na kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufungiwa kufanya biashara na mamlaka ya bandari.

Kwa upande wake naibu waziri wa wizara hiyo,Injinia EDWIN NGONYANI,amesema kuwa kuna malalamiko kuwa wapo mawakala wa forodha ambao wanadai wamelipia fedha za tozo lakini bado wanahesabiwa kuwa hawajalipa,amewataka kuwasilisha nyaraka stahiki zitakazoonesha kuwa wamelipia tozo hizo kihalali ili hatua stahiki zichukuliwe.

Akihitimisha kuwasomea taarifa hiyo waandishi wa habari,waziri Professa Mbarawa amesema serikali haitamvumilia mfanyakazi yeyote wa mamlaka ya usimamizi wa bandari nchini awe mkubwa au mdogo ambae ataendelea na kujihusisha na upotevu wa mapato ya mamlaka ya bandari hiyo pia inahusisha mawakala wote wa forodha ambao wataendelea kujihusisha na wafanyakazi wa mamlaka ya bandari kutoa mizigo bila ya kulipa tozo watafutiwa leseni zao.



Monday 28 December 2015

YANGA YAVUNJA MKATABA NA NIYONZIMA,YAMUAMURU KULIPA KITITA CHA FEDHA DOLA ZA KIMAREKANI ZAIDI YA 71 ELFU





Uongozi wa Klabu ya Soka ya Yanga umetangaza kuachana na kiungo wa Yanga ambaye pia ni Nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda Haruna Niyonzima baada ya nyota huyo kuelezwa kuwa amekuwa na utovu wa nidhamu kwa muda mrefu.

Uongozi huo umeachana na Nyota huyo, huku wakimdai kuwalipa Yanga kiasi cha Dola za kimarekani zaidi ya  elfu 71.

Kuvunjwa kwa mkataba huo na Yanga kumekuja baada ya Nionzima kushindwa kufika kwa wakati katika kambi ya timu hiyo mara baada ya kwenda kwao kuitumikia timu ya Taifa , kwani hata mara baada ya kurejea nyota huyo hakufika kambini kwa wakati.



Monday 14 December 2015

News:MAPIGANO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI WAZIRI NCHEMBA ASIKITIKA ACHUKUA HATUA MVOMERO ASHANGWAZWA NA UKATILI KWA WANANCHI WA MJI HUO





 
Mgogoro wa wakulima na Wafugaji:Hii leo nimefika Mvomero kijiji cha DIhinda kata ya Kanga kufuatilia na kuchukua hatua dhidi ya tukio baya la mauaji,Kujeruhi BInadamu na Wanyama lililotokea Desemba 12/2015.
"Natoa rai kwa Wananchi hususani wa jamii ya Wafugaji na Wakulima,Hakuna ardhi au Mnyama mwenye thamani sawa na Maisha ya Mwanadamu yeyote yule,njia bora na salama ya kutatua migogoro hii inayohusisha wakuliama na wafugaji ni kufuata taratibu za kuonana na Uongozi wa serikali wa eneo husika hatua kwa hatua,Nawaomba wananchi waache kujichukulia sheria mikononi.Tunakwenda kuunda kamati za usuruhishi wa migogoro hii kwa kila kijiji zitakazohusisha pande zote mbili ili kubaini wavamizi wa maeneo na kuwachukulia hatua za kisheria."
Nimeagiza kupitia kwa Mkuu wa wilaya na kamati yake ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Mvomero(kwa husika maeno yote ya Nchi yetu) kuhakikisha wanaimarisha ulinzi maeneo yote yenye migogoro,pili wahakikishe waliosababisha maafa wanakamatwa mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sharia.
Kwa walio jeruhiwa,nimeagiza wapatiwe matibabu kwanza bila kuchelewa na hatua za kisheria kwa wenye hatia zifuate.


WASOMI KUMJADILI RAIS DK. MAGUFULI UDSM JUMAPILI

Waandaaji wa Mdajala kuhusu Hotuba ya Rais Dk. John Magufuli, aliyoitoa wakati wa kufungua Bunge mjini Dodoma, wakizungumza na waandishi wa habari leo, katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dar es Salaam.



Wednesday 9 December 2015

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI ASHIRIKI USAFI KATIKA SHEREHE ZA KUADHIMISHA SIKUKUU YA MIAKA 54 YA UHURU TANZANIA

Rais John Pombe Magufuli, akikusanya rundo la takataka, siku ya kuadhimisha miaka 54

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AONGOZA SHEREHE ZA UHURU KWA KUSHIRIKI, KUFANYA USAFI,,MAKAMU WA RAIS BI SAMIA SULUHU HASSAN NAYE ASHIRIKI, JK NA MAMA SALAMA, WASHIRIKIANA NA WANANCHI




Monday 7 December 2015

CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI (MoCU) CHAFANYA MAHAFALI YA KWANZA.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi  (MoCU) Pius Msekwa akitunuku Shahada ,Stashahada na Astashahada kwa wahitimu wa Chuo hicho wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho.
Wahitimu wa kozi mbalimbali waliohitimu katika Chuo Kikuu cha Ushirika mjini Moshi,(MoCU)
Miongoni mwa wageni waalikwa alikuwepo pia Mbunge wa jimbo la Moshi mjini ,Jafary Michael.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Profesa Faustine Bee akizungumza wakati wa sherehe za mahafali ya kwanza ya Chuo hicho yaliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Chuo hicho.
Miongoni mwa wahitimu walikuwepo pia Mbunge wa viti maalum,Sharry Raymond pamoja na Mkuu wa wilaya ya Mwanga ,Shaibu Ndemanga.
Baadhi ya wakufunzi katika chuo hicho.
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro ,Severine Kahitwa (Kulia) akiteta jambo na Meneja wa benki ya NMB ,tawi la Mandela mjini Moshi ,Emanuel Kashusho wakatiwa mahafali ya kwanza katika chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Kaimu Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo (Utawala na Fedha) Ndayizera Manta (Kushoto) akiwa na Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) Profesa Gerald Monera wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Muongozaji wa sherehe ya mahafali hayo Cyril Komba akitoa muongozo wa shughuli hiyo iliyofanyika viwanja ya Chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Pius Msekwa akitoka katika viwanja vya Ushirika mara baada ya kumalizika kwa sherehe ya mahafali ya kwanza ya chuo hicho.
Baadhi ya wakufunzi wa Chuo hicho,Profesa Wakuru Magigi (kulia ) wakiwa na Mkuu wa Shule ya Polisi zamani Chuo cha Polisi Moshi,Matanga Mbushi .
Mkuu wa wilaya ya Ilala,Raymond Mushi (kushoto) akiwa na mmmoja wa wakufunzi katika chuo hicho Dkt Kaleshu ,wakipozi katika picha ya pamoja na Mbunge wa Viti maalum CCM ,Sharry Raymond.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini (0755659929).

MKUU WA MAJESHI MSTAAFU,JENERALI GEORGE WAITARA AONGOZA TIMU YA MAAFISA 24 WA JESHI KUPANDA MLIMA KILIMANJARO.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Fulgence Mponji akizungumza katia hafla fupi ya kuanzisha safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa maofisa 24 wa jeshi la wananchi Tanzania .kulia ni Mkuu wa Majeshi Mstaafu,Jenerali George Waitara na kushoto ni Mnadhimu mkuu wa Jeshi la wananchi ,Luteni Jenerali ,Samweli Ndomba.
Baadhi ya washiriki wa zoezi la kupanda Mlima Kilimanjaro.
Mkuu wa majeshi Mstaafu,Jenerali George Waitara akizungumza katika hafla hiyo.
Baadhi ya wapandaji.
Mhifadhi Mkuu ,Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro,( KINAPA) akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Washiriki.
Afisa Masoko wa KINAPA,Antypas Mgungusi akieleza jambo wakati wa hafala hiyo.
Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Utalii,Balozi Charles Sanga ni mingoni mwa washiriki wa zoezi hilo la kupanda mlima Kilimanjaro.
Mhifadhi mkuu KINAPA,Erastus Lufunguro akiongozana na mgeni rasmi kwa ajili ya kukabidhi bendera kwa wapandaji mlima hao.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo ,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi,Fulgence Mponji akikabidhi bendera kwa Mkuu wa majeshi mstaafu ,Jenerali George Waitara ambaye ndiye kiongozi wa msafara huo.
Washiriki wakijiandaa kuanza safari.
Safari ya kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro ikaanza kwa maafisa 24 wa JWTZ .
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube