BREAKING

Friday 10 December 2021

RAIS UHURU AFANYA ZIARA NCHINI TANZANIA






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, na mgeni wake Mhe. Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya wakiwa katika picha yenye waasisi wa Mataifa mawili Tanzania na Kenya Hayati Mwalim Julius Nyerere wa Tanzania na Hayati Jomo Kenyatta wa Kenya wakati Rais Kenyatta alipowasili Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Desemba, 2021. Mhe. Rais Kenyatta yupo nchini kwa Ziara ya Kiserikali ya siku moja.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na mgeni wake Mhe. Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alipowasili Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Desemba, 202. Mhe. Rais Uhuru Kenyatta yupo nchini kwa Ziara ya Kiserikali ya siku moja.

 

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AWATUNUKU NISHANI ASKARI 893 ZA MIAKA 60 YA UHURU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitunuku Nishani ya Utumishi mrefu na Tabia Njema Mkaguzi wa Polisi Stahmili Herman Lusatila kati ya watunukiwa 893 ikiwa ni sehemu ya Sherehe ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara, katika hafla iliyofanyika leo tarehe 09 Desemba 2021, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitunuku Nishani ya miaka 60 ya Uhuru kwa Mkuu wa Jeshi la Uhamiaji nchini Kamishna Jenerali Dkt. Anna Peter Makakala kati ya watunukiwa 893 ikiwa ni sehemu ya Sherehe ya Maadhimisho ya kutimiza miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara, hafla ya utoaji wa Nishani hizo imefanyika leo tarehe 09 Desemba 2021, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitunuku Nishani ya miaka 60 ya Uhuru kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Simon Nyakoro Sirro kati ya watunukiwa 893 ikiwa ni sehemu ya Sherehe ya Maadhimisho ya kutimiza miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara, hafla ya utoaji wa Nishani hizo imefanyika leo tarehe 09 Desemba 2021, Ikulu Jijini Da es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitunuku Nishani ya miaka 60 ya Uhuru kwa Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee kati ya watunukiwa 893 ikiwa ni sehemu ya Sherehe ya Maadhimisho ya kutimiza miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara, hafla ya utoaji wa Nishani hizo imefanyika leo tarehe 09 Desemba 2021, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

TANZANIA ILIVYOANDIKA HISTORIA KUBWA DUNIANI,SIKU YA UHURU WA MIAKA 60 MAONYESHO YASISIMUA






















Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na kuwapongeza Watanzania kwa kutimiza  miaka 60 ya  Uhuru wa Tanzania Bara, katika Maadhimisho  yaliyofanyika leo tarehe 09 Desemba 2021 katika Uwanja wa Uhuru  Jijini Dar es Salaam.

DC MOYO: AMEPIGA MARUFUKU KUZIBA VICHOCHORO MANISPAA YA IRINGA



Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiona na baadhi ya wananchi wa manispaa ya Iringa wakati wa ziara ya kusikiliza kero za wananchi wa wilaya hiyo
Baadhi ya vichochoro ambavyo vimezibwa kwa kuta na kuhatari maisha ya wananchi wengine endapo itatokea majanga yoyte yale hasa moto
Baadhi ya vichochoro ambavyo vimezibwa kwa kuta na kuhatari maisha ya wananchi wengine endapo itatokea majanga yoyte yale hasa moto
Baadhi ya vichochoro ambavyo vimezibwa kwa kuta na mageti na kuhatari maisha ya wananchi wengine endapo itatokea majanga yoyte yale hasa moto

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ametoa amri ya kuvunjwa kwa kuta zote zilizojengwa kuziba vichochoro katika maeneo ya makazi ya watu Manispaa ya Iringa wavunje mara moja kabla sheria haijachukua mkondo wake kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria za nchi.

 

Moyo alitoa amri hiyo baada ya kufanya ziara katika baadhi ya mitaa ya kati kati ya mji wa Iringa na kubaini kuzibwa kwa vichochoro jambo ambalo amelitaja kuwa ni kinyume na sheria za mipango miji.

 

Wakati wa ziara hiyo iliyofuatiwa na mkutano wa hadhara katika kata ya Mivinjeni Moyo amesema kuzibwa kwa vichochoro kunakwamisha jitihada za uokoaji nyakati yanapotokea majanga ya moto hali inayohatarisha usalama.

 

Alisema kuwa kumeibuka tatizo la wananchi kuziba vichochoro vilivyopo mtaani bila kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika.

 

Moyo alisema kuwa wananchi wote walioziba vichochoro watachukuliwa hatua kali za kisheria kwa kuwa wanafanya makosa hayo makusudi hivyo wanapaswa kuvunja mara moja ili kuweka mitaa yote katika hali ya usalama.

 

Alisema wananchi wote wanaofanya shughuli za ujenzi  wanatakiwa kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika la sivyo watakukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa wanakuwa wamevunja sheria kwa makusudi.

 

 

Moyo alisema kuwa vichochoro vyote vilivyopo manispaa ya Iringa vinatakuwa kuwa wazi na marufuku wa idara ya mipango miji kutoa kibali cha kuziba vichochoro kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi wa manispaa ya Iringa na nje ya Iringa.

 

Alisema kuwa ukitokea moto inakuwa vigumu kuuzima kutokana na kuziba kwa vichochoro na kuleta madhara kwa wananchi ambao wanakuwa wamepata majanga hayo kwa kujitakia.

 

Moyo aliwataka wafanyakazi wote wa manispaa ya Iringa kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa kuwa serikali haijawahi kwenda likizo hivyo wafanyakazi wanatakiwa kuwa kazini muda wote.

 

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo anatoa agizo hilo ikiwa ni siku ya pili mara baada ya kuanza ziara katika manispaa ya Iringa na kubaini kuwepo kwa changamoto ya kuzibwa kwa vichochoro vinavyopaswa kuwapo kati ya jengo moja na jingnine

 

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya Makusudi ya amri hii aliyoitoa ni kuyafanya makazi ya watu katika manispaa ya Iringa kuwa maeneo salama na hasa akieleza kuachwa wazi kwa maeneo hayo kutarahisisha shughuli za uokoaji pindi majanga ya moto yanapotokea

 

Hata hivyo anawageukia maafisa wa Idara ya Mipango miji Manispaa ya Iringa akiwaonya kuwa endapo wamehusika kuruhusu kuzibwa kwa vichochcoro hiyo hatua kali zitachukuliwa huku akiwahusisha na Rushwa

 

Mkuu huyo wa Wilaya anasema ni jambo la kushangangaza kuona wataalam wa Idara ya Mipango miji pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa na kata kwa kushindwa kuchukua hatua licha ya kushughudia kila kukicha vichochcoro vikiendelea kuzibwa huku akiwataka kuasha kufanya kazi kwa mazo

Friday 29 October 2021

HATIMAYE VIBALI VYA NEMC (EIA CERTIFICATE) NDANI YA SIKU 14 BADALA YA SIKU 105



Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Andrea Kundo (Kushoto) akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande wakati wa kikao kazi cha kujadili kuhusu ufumbuzi wa kero ya ucheleweshwaji wa vibali (Eia Certificate) vinavyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa NHIF Jijini Dodoma tarehe 28 Octoba 2021



Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Andrea Kundo (Kushoto) akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili kuhusu ufumbuzi wa kero ya ucheleweshwaji wa vibali (Eia Certificate) vinavyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa NHIF Jijini Dodoma tarehe 28 Octoba 2021.


Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili kuhusu ufumbuzi wa kero ya ucheleweshwaji wa vibali (Eia Certificate) vinavyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa NHIF Jijini Dodoma tarehe 28 Octoba 2021.


Sehemu ya wajumbe wakifuatilia kikao kazi kilichoongozwa na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Andrea Kundo (Kushoto) akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande kujadili kuhusu ufumbuzi wa kero ya ucheleweshwaji wa vibali (Eia Certificate) vinavyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa NHIF Jijini Dodoma tarehe 28 Octoba 2021.


Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC Dkt Samuel Gwamaka akisisitiza jambo mbele ya Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Andrea Kundo (Kushoto) akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande wakati wa kikao kazi cha kujadili kuhusu ufumbuzi wa kero ya ucheleweshwaji wa vibali (Eia Certificate) vinavyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa NHIF Jijini Dodoma tarehe 28 Octoba 2021.


Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Andrea Kundo na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande kwa pamoja wamekutana na kujadili kuhusu ufumbuzi wa kero ya ucheleweshwaji wa vibali (Eia Certificate) vinavyotolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC.

 

Katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Jijini Dodoma, imebainishwa kuwa kuchelewa kwa upatikanaji wa vibali hivyo kwa kiasi kikubwa imekuwa kikwazo katika miradi ya mawasiliano iliyokuwa ikihitaji Vibali kutoka NEMC.

 

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Andrea Kundo na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande katika nyakati tofauti wamewaagiza wataalamu wa Wizara hizo mbili kukaa pamoja na kuunganisha mifumo yao ili iweze kusomana na kuondoa kabisa visingizio vya kutopatikana Vibali kwa wakati.

 

Mhe Kundo amesema kuwa utatuzi huo wa changamoto hiyo iliyopelekea kuchelewa kukamilika kwa miradi ya serikali kwa Zaidi ya miezi saba jambo ambalo lilikuwa likirudisha nyuma utendaji na ufanisi wa kazi za serikali kwa wakati.

 

Amesema kuwa sasa vibali vitaanza kutoka ndani ya siku 14 mpaka 30 kutoka siku 105 za awali ambazo zilikuwa kikwazo kwa wakandarasi waliokuwa wanajenga minara mbalimbali ya mawasiliano.

“Ndugu zangu nimehangika na minara mingi ambayo imebaki viporo ikiwa na visingizio vya kutopatikana Vibali, sasa najua nani ambaye anakwamisha miradi yetu na tutachukua hatua kulingana na uhalisia” Amesisitiza Mhe Kundo

 

Katika kikao kazi hicho, Mhadisi Kundo amemshukuru Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Suleiman Jaffo pamoja na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande kwa kufanikisha kikao hiki ambacho kimezaa matunda.


Naibu Waziri Kundo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha Bajeti kwa ajili ya miundombinu ya Mawasiliano ambayo ni moja ya njia kuu za uchumi wa nchi.

 

Naye Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe Hamad Hassan Chande amesema kuwa kikao kazi hicho baina ya Wizara hizo mbili kimezaa matunda ambayo ni manufaa kwa Taifa na vizazi vijavyo kwani kimekuwa na maridhiano makubwa na muhimu.

 

Amesema kuwa pamoja na kuwa na makubaliano hayo yatakayopelekea maendeleo ya uwekezaji lakini ni lazima wananchi kuzingatia umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa sababu ni wazi kuwa bila mazingira hakuna maisha.

 

“Itakuja kuwa ni lawama kubwa sana kwa wajukuu zetu au watoto wetu kama tumewekeza kwenye maendeleo bila kujali mazingira hivyo tumekubaliana kuwa tunaenda kwenye maendeleo lakini maingira lazima tuyatazame kwa jicho la tatu” Amesisitiza Mhe Chande

 

Naibu Waziri Chande amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ambaye ameamua kuleta na kuwakaribisha wawekezaji na kuzifanya sera kuwa rahisi zinazowafanya wawekezaji kutokuwa na kigugumizi katika kuwekezaji nchini Tanzania.

“Ushirikiano huo unapaswa kuwa sababu ya mahusiano ya karibu ya ujenzi wa Taifa kwa pamoja kwani kufanya hivyo Taifa litafaidika na matunda ambayo yatakuwa ni endelevu wakati wote” Amekaririwa Mhe Chande

 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira-NEMC Dkt Samuel Gwamaka ameahidi kufanya kazi na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote nchini UCSAF ili kuweka mazingira mazuri ya kufanya kazi hizo.

 

Asema kuwa atatekeleza maelekezo yaliyotolewa na Naibu Mawaziri hao ikiwemo kutoa vibali kwa wakati kama ilivyotakiwa kutolewa ndani ya siku 14 mpaka 30.

 

Naye Mkuu wa Uendeshaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote nchini Mhandisi Albert Richard amesema kuwa kikao kazi hicho kimekuwa na tija kwa kiasi kikubwa kwani serikali inadhamiria kufikisha huduma mawasiliano kwa wananchi wa mijini na vijijini ambapo hakuna mvuto wa kibiashara.

 

Mhandisi Richard amesema kuwa ili kufanikisha miradi hiyo ni lazima kupata vibali mbalimbali kwa wakati ikiwemo cha Mazingira ili kurahisisha na kutatua tatizo la kuchelewa kwa vibali hivyo.


Wednesday 1 September 2021

KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU,SAYANSI NA TEKNOLOJIA AFUNGUA KIKAO CHA SIKU MBILI CHA WADAU MAENDELEO YA ELIMU


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akifungua kikao cha wadau wa maendeleo ya sekta ya elimu wakati wakijadili taarifa ya uchambuzi wa hali halisi ya sekta ya elimu kwa mustakabali wa  uimarishaji wa Sekta.





Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo ametoa wito kwa wadau wa elimu kuendelea kutoa maoni katika hatua mbalimbali za maandalizi ya Mpango wa tatu wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu ili kuongeza wigo na ubora wa elimu inayotolewa kwa Watanzania.

 

Akizungumza  Jijini Dar es Salaam wakati akifungua kikao cha wadau wa maendeleo  sekta ya elimu wakati wakijadili taarifa ya uchambuzi wa hali halisi ya sekta ya elimu kwa mustakabali wa  uimarishaji wa Sekta amesema Wizara ipo katika uandaaji wa Mpango Tatu wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (2021/22 - 2025/26), hivyo ni ni jambo zuri kufanya uchambuzi wa hali halisi ya sekta katika kipindi cha utekelezaji wa mpango uliomalizika ili kujua yale yaliyopangwa yamefanikiwa kwa kiasi gani.


“Wengi wenu mtakuwa mnatambua kuwa Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu Awamu ya pili (2016/17 - 2020/21) umemalizika, Hivyo uandaaji wa Mpango wa Tatu wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu (2021/22- 2025/26) umeanza na hatua ya kwanza ni kufanya tathmini ya hali halisi ya sekta katika kipindi cha utekelezaji wa mpango uliomalizika muda wake. Kazi hiyo ya kufanya uchambuzi ndio iliyotukusanya hapa siku hii leo hivyo nawaomba mtoe mchango wenu katika taarifa hii na mapendekezo ya namna ya kuboresha sekta ya elimu nchini,” amesema Katibu Mkuu Akwilapo

 

Amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa wadau katika kuwahudumia watanzania wote kwa kutoa elimu bora katika ngazi zote, kuanzia elimu ya awali hadi Chuo kikuu na kwamba Wizara itaendelea kushirikiana nao kwa karibu na kuweka mazingira rafiki na wezeshi ili kuharakisha azma ya Serikali ya kuleta maendeleo kwa wananchi

 

Katibu Mkuu Akwilapo ametumia fursa hiyo kuwashukuru wadau ambao wamegharimia zoezi la uchambuzi wa hali ya sekta ya elimu hapa nchini, ambao ni Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza Benki ya Dunia na UNICEF ambao wamekuwa wasimizi Wakuu wa zoezi zima la tathmini ya sekta. Pia amewapongeza Washauri Elekezi, kitaifa na kimataifa waliotekeleza zoezi la uchambuzi kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Fedha na Mipango.

 

Kwa upande wake Naibu Katibu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Gerald Mweli amesema kila baada ya miaka mitano Serikali imekuwa ikiandaa Mpango unaotoa mwelekeo wa namna ya kuboresha utoaji wa elimu nchini ili kujua mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mpango ulioisha.


 Aidha amebainisha TAMISEMI imepewa jukumu la kusimamia utoaji wa elimu msingi na sekondari nchini na kwamba kwa mwaka huu wa fedha wamefanikiwa kuajiri walimu wanaofundisha elimu ya msingi na sekondari elfu 14,949 ikiwa ni sambamba ujenzi wa miundombinu ili kuhakikisha ufundishaji unaendelea na katika mazingira yaliyoimarishwa.


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania Lydia Wilbard ameonesha furaha yake kwa Serikali kufanya kikao hicho na kuwashirikisha wadau amesema ni utaratibu mzuri ndani ya serikali katika kuhakikisha kwamba Sekta ya elimu inapojadiliwa inahusisha wadau wa elimu kwani utekelezaji wa mipango ni  jumuishi


“Kushirikishwa kwetu sisi wadau tunapata fursa ya kuona kwa undani sekta yetu elimu imekwendaje na kutusaidia kupanga mikakati maalum ambayo italeta matokeo chanya katika kupanga mkakati unaokuja,”amesema Lydia Makamu Mwenyekiti Bodi ya TENMET.


Tuesday 24 August 2021

WAZIRI MKENDA ALIVYOONGOZA MAMIA YA WANANCHI MAZISHI YA BASIL MRAMBA//ANENA MAZITO


Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda akitoa salamu za Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan wakati akiaga mwili wa marehemu Mhe Basil Mramba katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro.
Mwili wa marehemu Mhe Basil Mramba katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya ibada ya mazishi.

Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda (Kulia) pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Stephen Kagaigai (Wa pili kulia) wakiwa katika ibada maalumu ya kuaga  mwili wa marehemu Mhe Basil Mramba katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro.


Sehemu ya familia ya Marehe Mhe Basil Mramba wakiwa katika ibada maalumu ya kuaga  mwili wa marehemu Mramba katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro.


Sehemu ya viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika ibada maalumu ya kuaga  mwili wa marehemu Mramba katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro.


Mwakilishi wa Askofu wa jimbo katoliki la moshi Padre Deogratius Matiika akiendesha misa katika viwanja vya Sabasaba katika Halmashauri ya Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro wakati wa ibada ya mazishi ya Mhe Basil Pesambili Mramba.


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Stephen Kagaigai akitoa salamu za wananchi wa mkoa huo wakiwa katika ibada maalumu ya kuaga  mwili wa marehemu Mhe Basil Mramba katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro.


Geofrey Mramba ambaye ni mtoto wa kwanza wa marehemu Mhe Basil Mramba, akisoma wosia wa marehemu baba yake katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika Wilaya ya rombo Mkoani Kilimanjaro wakati wa ibada ya mazishi.


Mamia ya wananchi wa Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro na kwingineko nchini wamejitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Rombo na kushika wadhifa mkubwa akihudumu wakati huo kama waziri wa fedha, Mhe Basil Pesambili Mramba.


Katika shughuli hiyo ya kuaga mwili huo iliyofanyika katika viwanja vya sabasaba vilivyopo katika Halamshauri ya wilaya ya Rombo kwa niaba ya serikali, iliongozwa na Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda aliyemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan.


Mhe Mramba ambaye alifariki Agosti 17, mwaka huu katika hospitali ya Regency iliyopo mkoani Dar es salam ameagwa katika uwanja wa sabasaba na kisha kuzikwa kijijini kwake Shimbi wilayani Rombo.


Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Rais Samia,  Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda ambaye amesema Taifa litamkumba Basil Mramba kwa uzalendo na juhudi zake alizozifanya wakati akiwa katika nyadhifa mbalimbali za uwaziri serikali na kusema ameacha alama kubwa kwa Taifa inayopaswa kutambuliwa ipasavyo.


Waziri Mkenda amesema kuwa, Mramba ameacha alama ambazo hazitafutika kamwe katika wilaya ya Rombo hasa katika suala la barabara na kilimo cha ndizi na maparachichi ambacho ndio uchumi mkubwa na tegemezi kwa wananchi wa wilaya hiyo.


"Wananchi wa Rombo kamwe hatutamsahau Mramba kwa mambo makubwa aliyoyafanya wakati wa ubunge wake,wakati anaingia kwenye ubunge kwa mara ya kwanza Rombo ilikuwa na shule nne pekee za Sekondari na mpaka anaondoka kwenye nafasi hii ya ubunge alicha shule zaidi ya 40 kutokana upambanaji wake," Amekaririwa Profesa Mkenda


Waziri huyo wa Kilimo Mhe Profesa Mkenda amewaahidi wananchi wa Jimbo hilo kuwa ataendeleza yale yote ambayo Mramba alitamani kuyakamilisha lakini hayakukamilika wakati alipouwa madarakani.


Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kilimanjaro, Ndg Patrick Boisafi amesema kifo cha Mramba ni pigo kubwa kwa wanachi na wakazi wa Rombo na Taifa kwa ujumla kwani alikuwa ni mtu aliyetumikia Taifa kwa upendo na kulipenda jimbo lake.


"Mramba ameacha alama hapa Rombo na Taifa kwa ujumla, maisha yake yanajieleza na alifanya kazi kubwa kwenye nchi hii na sisi sote ni mashahidi, aliipenda Rombo na Kilimanjaro kwa ujumla tuna cha kujifunza  kupitia kwake, alitumia nafasi aliyopewa na serikali kuwatumikia wananchi wake," Amesema Boisafi


Akizungumza wakati wa ibada ya mazishi, Mwakilishi wa Askofu wa jimbo katoliki la moshi, Padre Deogratius Matiika amesema Mramba ameandika historia katika jimbo hilo na kwa kanisa katoliki na kwamba atakumbukwa kwa mengi kwani alikuwa ni kimbilio la wengi.


"Tutaendelea kumuenzi ndugu yetu Mramba amekuwa ni mti mzuri uliozaa matunda kwani alimpenda Mungu na alimtumikia ipasavyo, alishiriki nasi katika maeneo mbalimbali pale ambapo kulikuwa na msaada kanisani alitusaidia, ameandika historia ambayo haitafutika Kilimanjaro, hakuna anayeweza kupinga hili kwamba aliweka historia wilaya ya Rombo," Amesisitiza Padre Matiika


Mramba alihudumu katika nyadhifa mbalimbali za uwaziri ikiwemo Waziri wa Fedha, Waziri wa Viwanda na Biashara ambaye pia alikuwa mwanzilishi wa viwanda vidogo vidogo nchini (SIDO)


 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube