BREAKING

Wednesday 17 June 2020

BABA WA SAMATTA ANENA JAMBO....WAKATI SAMATTA AKIWA UWANJANI LEO EPL

MSHAMBULIAJI wa timu ya Aston Villa inayoshiriki Premier League, Mtanzania, Mbwana Samatta amemhakikishia baba yake mzazi, mzee Ally Samatta kuwa atapambana kuhakikisha anainusuru timu yake isishuke daraja msimu huu.

Samatta ambaye amejiunga na timu hiyo katika usajili wa dirisha dogo msimu huu kwa mkataba wa miaka minne na nusu, ana kazi kubwa ya kuibakisha timu hiyo kutokana na kuwa kwenye nafasi mbaya ya 19 ikiwa na pointi 25 ikifuatiwa na Norwich City ambayo inaburuza mkia ikiwa na pointi 21.

Mzee Samatta alisema kuwa, kutokana na ligi kutarajiwa kurejea tena leo Juni 17, 2020, mtoto wake amemwambia atapambana kuinusuru timu hiyo kushuka daraja.

“Suala la ligi kurejea lipo wazi na kila mmoja amekuwa akilijua vizuri isipokuwa kijana amenieleza nia yake ni kutaka kuinusuru timu isishuke hivyo amepanga kucheza kwa kujituma zaidi ili kufikia malengo.

“Unajua wapo ambao walitaka ligi ifutwe kama zilizofanya nchi nyingine lakini England wao wameona ni bora kumalizia hivyo kila mmoja anatakiwa apambane na yeye ndiye amenieleza kwamba hatamani kuona wakishuka hivyo lazima ajitoe ili kuinusuru timu na msimu ujao waanze pamoja,” alisema mzee Samatta.

WADAU WATAKIWA KUENDELEA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KUINUA MICHEZO







WADAU WAMETAKIWA KUENDELEA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KUINUA MICHEZO  KUWEKA UDHAMINI KWENYE TIMU ZA MTAANI ILI KUIBUA VIPAJI AMBAVYO VITAKUA NA MANUFAA KWA TAIFA 
Kuali hiyo imetolewa katika Mchezo wa Kusisimua uliozikutanisha  timu mbili kati ya Soccer City ya Mabwepande ya Mtaa wa Mji Mpya  dhidi ya timu ya New Kibamba FC Mchezo ambao umedhaminiwa na kampuni ya Msukuma One inayodhalisha na kusambaza Nafaka huku lengo ikiwa kuunga Mkono Serikali ya awamu ya tank kuunga mkono juhudi za kuinua sekta ya Michezo.

Mkurugenzi Mkuu wa Msukuma One Aman Manengero amesema kuwa wataendelea kusaidia jitihada hizo ili kuleta meandeleo zaidi.
Ktika mchezo huo mkali ilishuhudiwa timu ya kibamba FC kukubali kipigo baada ya kuzidiwa kwa mikwaju ya penati dhidi ya timu ya soka city baada ya timu hizo kutoka sare ya 

goli mbili kwa mbili ndani ya dakika tisini huku timu ya soka city ikiibuka na zawadi ya jezi iliyotolewa na mdau huyo.






Tuesday 2 June 2020

NDEGE YA MIZIGO KUIMARISHA USAFIRISHAJI SAMAKI NJE NCHI HIYOOO KUTUA


 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema mipango ya Serikali kununua ndege ya mizigo utaimarisha usafirishaji wa minofu ya samaki moja kwa moja kwenda nje ya nchi kutokea uwanja wa ndege wa Mwanza.

Waziri Kamwelwe ameyasema hayo Jumatatu Juni Mosi 2020 jijini Mwanza wakati akifungua mkutano wa kupokea mikakati ya pamoja kuondoa vikwazo na kufanikisha biashara ya usafirishaji minofu ya samaki kwenda nje ya nchi hususani mataifa ya Ulaya ambako kumekuwa na soko la uhakika.

Kikao hicho kimewajumuisha pia Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara za Mifugo na Uvuvi, Viwanda na Biashara pamoja na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa.

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (katika) akizungumza kwenye kikao hicho. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa na kulia ni Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.


 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube