BREAKING

Monday 7 October 2019

MULTICHOICE TANZANIA YAANZA MAADHIMISHO YA WIKI KWA WATEJA

 Mkuu wa Huduma kwa Wateja wa MultiChoice Tanzania Ngwitika Mwakihesya  akimuelekeza mmoja wa wateja waliofika katika tawi la MultiChoice Mlimani City Aziz Makupa jinsi ya kupata huduma mbalimbali za DStv ikiwa ni sehemu ya maaadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja. Kushoto ni afisa wa huduma kwa wateja wa tawi hilo Vedastina Ishengoma. Katika maadhimisho hayo, MultiChoice itatoa zawadi mbalimbali kwa wafanyakazi na wateja wake ikiwemo pia kuwatembelea wateja na kukusanya maoni yao ili kuweza kuboresha zaidi huduma zake.



Mkuu wa Huduma kwa wateja wa MultiChoice Tanzania Ngwitika Mwakihesya (kushoto) na Afisa Uhusiano Diana Ayo wakiwa na baadhi ya watoto waliofika na wazazi wao katika tawi la DStv Mlimani City mwishoni mwa wiki kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali. MultiChoice inaadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambapo pamoja na mambo mengine, itatoa zawadi mbalimbali kwa wafanyakazi na wateja wake ikiwemo pia kuwatembelea wateja na kukusanya maoni yao ili kuweza kuboresha zaidi huduma zake.

Kampuni ya MultiChoice Tanzania imeanza maadhimisho ya wiki ya wateja ambapo itaendesha shughuli mbalimbali ikiwemo kutoa zawadi kwa wafanyakazi na wateja kwa muda wa mwezi mzima.

Mkuu wa huduma kwa wateja Ngwitika Mwakihesya amesema kuwa katika kipindi hicho, MultiChoice Tanzania itakuwa na matukio mbalimbali yenye lengo la kuiwezesha kuwasogelea wateja karibu zaidi na kufahamu kwa kina uzoefu wao wa kupata huduma za DStv.

‘MultiChoice inaamini kuwa wafanyakazi na wateja wetu ndiyo nguzo ya ustawi wetu hivyo katika kipindi hiki tutahakikisha tunawafikia na kuwasikiliza maoni yao na hili tunalifanya ili tuweze kuboresha zaidi huduma zetu na kumfanya mteja ajisikie kuwa yeye kweli ni mfalme” alisema Ngwitika na kuongeza kuwa zoezi hilo litahusisha kuwazawadia wafanyakazi mbalimbali pamoja na wateja na pia kuwatembelea wateja wao maeneo mbalimblai ili kuwasikiliza na kupata maoni yao.

Amesisitiza kuwa kutokana na uzito huo, zoezi la kutembelea wateja litafanywa kwa kushirikiana na uogozi wa kampuni hiyo “Zoezi hili la kuwatembelea wateja litafanywa kwa kushirikiana na viongozi hivyo hata mkurugenzi mwenyewe na timu yake ya Menejimenti wataenda kuwatembelea wateja” alisisitiza Ngwitika.

Tuesday 1 October 2019

WASANII WA TANZANIA 'WAJIUZA' KISANAA TAMASHA LA JAMAFEST...


Wasanii wa muziki wa Kizazi kipya wa kundi la TMK Wanaume Family wakiongozwa na Mhe. Temba akiogoza jahazi kutoa burudani ndani ya katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Country Boy akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Country Boy akitoa burudani.
Msanii Barnaba akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.


Msanii Nahreel wa kundi la Navy Kenzo akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Aika wa Navy Kenzo akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Nahreel na Aika wa kundi la Navy Kenzo wakitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Joh Makin akitoa burudani katika katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Dj D- Ommy kwenye mashine akiendelea kuwapagawisha wanajumuiya ya Afrika Mashariki waliofika katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.

Msanii Jux akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Wasanii Jux (kushoto) na Joh Makin (kulia) wakitoa burudani. 
Aika, Nahreel na Jux wakitoa burudani kwa pamoja katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.

Msanii Jux akimtambulisha mpenzi wake.



TANZANIA YAMIMINIWA SIFA KEDE KEDE TAMASHA LA JAMAFEST....

Wachezaji ngoma wa Kinyarwanda wamesimamisha kwa muda shughuli nyingine zilizokuwa zikiendelea kwenye maonyesho ya Tamasha la Utamaduni la Afrika Mashariki (JAMAFEST) jijini Dar es Salaam nchini Tanzania baada ya kupanda jukwaani. Watazamaji mbalimbali kwenye maonyesho wameacha shughuli zao kwa muda na kusogea kushuhudia ngoma hiyo iliyoshirikisha wanaume na wanawake. Wadada wa Kinyarwanda walikuwa kivutio zaidi huku baadhi ya watazamaji wakiwashangilia na wengine wakionyesha kuwakubali kwa kuchukua video kwa simu na wengine wakijadiliana kuhusu urembo wa wanawake wa Kinyarwanda. “Huwa nashangaa hawa kina dada kutoka nchini Rwanda ni warembo jamani “Halafu hawatumii mavitu vitu lakini kama wananyumbulika.” “Nikiwaona kwenye picha huwa nahisi wamejiumba wenyewe jinsi wanavyovutia kama wamezaliwa na mama mmoja..” walisikia vijana wawili waliokuwa wakizungumza uwanja hapo wakati ngoma hiyo ikiendelea kutumbuiza Walisikika baadhi ya watu uwanjani hapo kila mmoja akisema lake kuhusu urembo wa wanawake hao ambao umekuwa gumzo.
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube