BREAKING

Wednesday 19 October 2016

MBUNGE VENNANCE MWAMOTO AGAWA VIFAA VYA MICHEZO KATIKA JIMBO LA KILOLO

 Mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto akikabidhi vifaa vya mchezo wa mpira wa miguu kwa wanamichezo wa kijiji cha Bomalang'ombe wakati wa mkutano wa hadhara ulifanyika katika kijiji hicho na kulia ni wachezaji wa timu ya kijiji cha Bomalang'ombe wakipokea jezi na mpira walizopewa na mbunge wa jimbo la kilolo
 Mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto akikabidhi vifaa vya mchezo wa mpira wa miguu kwa wanamichezo wa kijiji cha Bomalang'ombe wakati wa mkutano wa hadhara ulifanyika katika kijiji hicho na kulia ni wachezaji wa timu ya kijiji cha Bomalang'ombe wakipokea jezi na mpira walizopewa na mbunge wa jimbo la kilolo
 Mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto akikabidhi vifaa vya mchezo wa mpira wa miguu kwa wanamichezo wa kijiji cha Bomalang'ombe wakati wa mkutano wa hadhara ulifanyika katika kijiji hicho na kulia ni wachezaji wa timu ya wanawake wa  kijiji cha Bomalang'ombe wakipokea jezi na mpira walizopewa na mbunge wa jimbo la kilolo
 Mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto akikabidhi vifaa vya mchezo wa mpira wa miguu kwa wanamichezo wa kijiji cha Bomalang'ombe wakati wa mkutano wa hadhara ulifanyika katika kijiji hicho na kulia ni wachezaji wa timu ya kijiji cha Bomalang'ombe wakipokea jezi na mpira walizopewa na mbunge wa jimbo la kilolo


Mbunge wa Jimbo la Kilolo Vennance Mwamoto amegawa vifaa mbalimbali vya michezo kama alivyowahidi kwa Vijana na timu  za Jimbo hilo kwa lengo la kukuza vipaji vya wanamichezo na kuwandeleza ili wawe wachezaji bora hapo baadae.

Mwamoto ametekeleza ahadi hiyo katika Vijiji mbalimbali vinanvyounganisha Jimbo hilo la Kilolo katika ziara yake inayoendelea ya kuwashukuru wananchi wake kwa kuweza kumchagua kwa kura nyingi na kwenda kuwaakilisha Bungeni.

Akielezea wakati wa kutoa vifaa hivyo vya Michezo, Mwamoto amebainisha kuwa, vifaa hivyo anavitoa ni  kutokana na ahadi yake  yeye kama Mbunge aliiahidi kwa Vijana hao kuwapatia vifaa hivyo huku  baadhi yao pamoja na timu zilimuomba vifaa hivyo ambapo sasa anafanya kutekeleza.

“Niliahidi kuleta vifaa vya Michezo kwa kila Kata.Lakini pia mimi mwenyewe niliwaahdi kuwaletea vifaa nan leo hii natimiza ahadi yangu kwenu.” Alieleza Mwamoto.
Mwamoto ameongeza kwa kusema ameamua kutoa vifaa hivyo Kwa lengo la kusaidia Serikali katika juhudi za kuinua michezo lakini pia nisehemu ya Kazi zake kama Mbunge.
“Mimi nimecheza mpira kwa mafanikio ndio maana hadi saizi,kwa hilo mimi najua kuwa michezo ni ajira rasmi hivyo mtu kama unakipaji kitumie kipaji chako vizuri”. Mwamoto
Amesema kuwa michezo licha ya kujenga utimamu wa mwili lakini pia ni ajira huku akitoa mfano Kwa Mbwana Samatta anavyofanikiwa na leo anakipiga Ulaya.
Vifaa hivyo vya michezo ikiwemo seti nzima za Jezi  na mipira ya kuchezea ni hatua ya kuinua na kuendeleza vipaji kwa Vijana wa Jimbo hilo ambao wamekuwa na shahuku kubwa ya kuibua vipaji vyao vya mpira wa miguu.
“Leo nimetoa mipira na jezi hizi kwa timu za Bomalang’ombe na vijiji vya jirani kwa timu zote za wanaume na wanawake kwa lengo la kuendeleza vipaji vyenu”alisema Mwamoto
Aidha, amewataka Vijana hao kuwa na tabia ya kufanya mazoezi ya mara kwa mara kwani yatawasaidia kufanya vizuri katika mpira wa miguu na pia mazoezi ni afya huku kipaji cha mpira wa miguu kikiwa ni ajira kwao pia endapo michezo itaendelezwa zaidi hasa kwa vijana walio pembezoni.

Friday 14 October 2016

KAMANDA CHOUGHULE: VIJANA TUMUENZI BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE KWA KUFANYAKAZI ZA KUJIAJIRI

KAMANDA CHOUGHULE: VIJANA TUMUENZI BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE KWA KUFANYAKAZI ZA KUJIAJIRI

Friday, October 14, 2016
Sharik Chughule
Na Mwandishi Wetu
Mwenyekiti wa CCM, Shina la Pamba Road, Dar es Saaam, Sharik Choughule, amewaasa vijana kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa kufanya kazi za kujiajiri.

Amesema, kufanya hivyo kutawawezesha vjana wengi kuwa na ajira za uhakika, badala ya kusubiri ajira za serikali au taasisi mbalimbali kwa kuwa nafasi za ajira katika sekta hizo ni chache huku mahitaji yakiwa ni makubwa.

Choughule ambaye pia ni Kamanda wa Vijana Kata ya Kivukoni, Dar es Salaam, amesema hayo leo wakati akizungumzia kumbukumbu ya miaka 17 ya Kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambayo Maadhimisho yake yanafayika leo Kitaifa mkoani Simiyu kwa shughuli ya kuzima Mwenge.

Amesema, ili kuweza kufanya kazi za kujiajiri, vijana ni lazima kwanza kuondoa woga, ili kujiamini kuwa wanaweza kwa kuwa ajira binafsi zipo nyingi hasa ikizingatiwa kwamba wengi siku hizi wana elimu za kutosha hadi za viwango vya Chuo Kikuu.

"Vijana lazima tujiamini kwa kuwa sisi ndiyo tegemeo la taifa, hivyo siyo busara vijana kuanza kulalamika kuwa hatuna ajira kwa lengo la kutarajia kuwa Taifa ndilo tulitegemee kutupatia ajira, hayo si mawazo mwafaka kwa afya ya nchi yetu", alisema Shoughule.

Alisema, hatua ya vijana kuanza kuweka kisingizio cha ukosefu wa ajira za kuajiriwa, kinawadumaza vijana na kukosa maamuzi ya kubuni au kukosa ubunifu wa kubuni miradi aina tofauti tofauti kwa manufaa yao.

Choughule alisema, hivi sasa umefikia wakati wa vijana kuachana na mawazo mgando, kwa wasababu baadhi ya vijana ambao wameonyesha uthubutu, wameweza kujiajiri katika sekta za mitandao ya mawasiliano ambayo ni sekta imeenea duniani kote.

Alisema, mfano mzuri wa kuigwa ni vijana walipo Jeshi la Kujenga Taifa, JKT, ambao wamekuwa wakionyesha kufanya kazi nyingi ambazo siyo za kuajiriwa ikiwemo kuanzisha shughuli za kilimo cha kisasa, ufugaji na ufundi wa aina mbalimbali ikiwemo kutengeneza samani na ujenzi wa nyumba.

Choghule amesema, hatua ya vijana kufanyakazi za kujiajiri siyo tu watakuwa wamemuenzi Baba wa taaifa Mwalimu Nyerere, lakini pia watakuwa wamemuunga mkono Rais Dk John Magufuli katika azma yake ya kukuza uchumi wa taifa kwa kaulimbiu yake ya 'Hapa kazi tu'.

Saturday 8 October 2016

MD KAYOMBO ABAINI UBADHILIFU WA MAPATO KATIKA DUKA LA DAWA HOSPITALI YA SINZA

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo alipotembelea wodi ya wanawake
Watumishi, wauguzi na madaktari wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo alipozuri katika hospitali ya Manispaa ya Ubungo kwa ziara ya kikazi
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akiwasili Ofisi za Manispaa ya Ubungo

NEWS ALERT,,,OFISI YA MAKAO MAKUU YA HIFADHI YA SERENGETI YATEKETEA KWA MOTO LEO JUMAMOS


 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube