BREAKING

Wednesday 11 May 2022

TANESCO KUNUNUA NGUZO ZA UMEME NCHINI,WAZIRI ATANGAZA MASHARTI YAKE.


Waziri wa nishati January Makamba akiongea na wadau wa nguzo za umeme mkoani Iringa akiwaondolea sitofaumu iliyokuwepo ya kutonunua nguzo zao
Waziri wa nishati January Makamba akiwasikiliza wadau wa nguzo za umeme mkoani Iringa akiwaondolea sitofaumu iliyokuwepo ya kutonunua nguzo zaoWaziri wa nishati January Makambaakiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Queen Sendiga wakati wa majadiliano ya kuondoa sitofaumu iliyokuwepo ya kutonunua nguzo zao

 

Na Fredy Mgunda,Iringa.

WAZIRI wa nishati January Makamba ameliagiza shirika la umeme Tanzania (TANESCO) kuingia zabuni za ununuzi wa nguzo za kusambaza umeme kwa wakandarasi wanaokidhi vigezo,ikiwemo kuthibitisha baadhi ya nguzo zimetoka kwa wazalishaji wadogo wa ndani.

Waziri Makamba alisema kuwa TANESCO inatakiwa kushirikiana na taasisi zinazosimamia ubora wa bidhaa,ikiwepo shirika la viwango nchini (TBS) ili kuhakikisha nguzo zinazonunuliwa zinakidhi viwango vinavyotakiwa na shirika hilo.

Makamba alisema kuwa ili kuondoa changamoto kwa wadau wa nguzo na serikali ataunda kamati y wadau wa nguzo watakaokuwa wanafuatilia namna ya utengenezaji wa nguzo bora za umeme ambao utasaidia kuuza nje ya nchi ambavyo wadau wanguzo nchi nyingine wanafanya kwa ubora unaotakiwa.

“Sasa ipo mifano ya mfumo huu wa uwekezaji wa viwanda vya nguzo,nchi kama Afrika Kusini inamfumo mzuri sana na serikali yenu ipo tayari kuwachukua watu kadhaa kwenye kila wadau na kuwapeleka na kuwalipia mkajifunze kuhusu mfumo wa kudhibiti na kuhusu ubora” alisema makamba

Aidha aliwatoa hofu wadau wa nguzo za Miti za Umeme nchini kwa kuwahakikishia soko la kuuza nguzo zenye ubora kwa Shirika la Umeme nchini( TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini ( REA), hapa nchini.

Makamba alisema kuwa mkutano ulilenga kuondoa sintofahamu pamoja na minong’ono inayoendelea kwa baadhi ya watu wanaopotosha kuwa Serikali haitanunua nguzo za Umeme za ndani na badala yake zitaagizwa kutoka nje ya Nchi.

Katika mazungumzo yake na Wadau hao, Makamba alisema kuwa, Serikali itaendelea kununua nguzo za miti za Umeme kutoka kwa wazalishaji wa ndani ili kulinda viwanda vya ndani kwa kuzingatia ubora wa nguzo uliowekwa.

“Tutakapo toa zabuni ili ufanikiwe kupata zabuni hiyo lazima angalau asilimia Fulani ya nguzo hizo utakazouza ziwe zimetoka ka watu wadogo wadogo na katika nyaraka yako ya kuomba zabuni iwepo ili ufanikiwa angalau asilimia 20 au 10 ya nguzo iwe inatoka kwa wadau wadogo na wawe wamepewa mikataba inayoeleweka” alisema Makamba

Makamba amewataka Wadau hao kuunda chama Cha wazalishaji wa nguzo ili kiweze kudhibiti ubora unaotakiwa na hata kutoa adhabu kali kwa atakayebainika kuzalisha chini ya Kiwango pamoja na kuandaa sheria zitakazoongoza chama hicho.



“Lengo la Serikali ni kukuza uchumi wa wananchi wake kwa kuboresha bidhaa zao kwa kuwasimamia katika kuzalisha kwa vigezo na ubora uliowekwa, ili wananchi hao waweze kunufaika na kukuza uchumi wao na pato la Taifa kwa ujumla” Alisema Makamba.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Maharagwe Change, aliwataka Wadau hao kuwa waaminifu pale nguzo zao zinapotakiwa kupelekwa katika maeneo ya miradi kwa kuweka nguzo halisi zilizokaguliwa na siyo kufanya udanganyifu wa kuweka zisizokuwa na ubora.

Amesema kumekuwa na changamoto ya nguzo kuharibika baada ya muda mfupi kutumika kutokana na kuwa chini ya kiwango na ubora unaotakiwa, huku nguzo hizo zikiwa tayari zimekaguliwa na kuonekana zina ubora unaotakiwa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Said, amewahakikishia Wadau hao kuwa soko la nguzo lipo la kutosha kwani bado miradi mingi ya usambazaji wa Umeme vijijini inaendelea na nguzo nyingi zinahitajika.

Akitoa mfano Mkoa wa Iringa kuwa kuna Mradi wa Ujazilizi ambao unatarajia kuanza hivi karibuni katika Mkoa huo na mikoa mingine.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Queen Sendiga amewapongeza wabunge wa Mkoa wa Iringa Kwa kuwa wamoja Katika kutetea ajenda za kimaendeleo zinazohusu Mkoa wa Iringa. 

Alisema kuwa umoja ambao wameonesha kwenye kupigania suala la nguzo za Umeme kuendelea  kununuliwa hapa hapa Nchini wamefanya Jambo la kizalendo sana kwani linaenda kuongeza mapato kwa serikali na Wananchi kwa ujumla. Vivyo hivyo amewataka kuendelea  kufanya hivyo kwenye ajenda nyingine za ki mkoa .

Sendiga Alisema kuwa  Mkoa wa Iringa na Njombe ndio ambao wameuza nguzo zaidi ya asilimia 90 zilizotumika kusambaza Umeme nchini na walishangazwa kusikia hoja ya kuwa nguzo za ndani sio bora wakati tayari nguzo nyingi zimesimikwa Vijijini na zipo imara

"Tukushukuru Mheshimiwa Waziri wa Nishati kwa kufanya maamuzi haya ambayo yana Afya kubwa Kwa uchumi wa mikoa hii miwili na Taifa"

Amewataka Wadau hao kutoa ushirikiano kwa mamlaka husika na kuwa wasikivu kwa kile watakachokuwa wakielezwa kwa lengo la kupata bidhaa Bora kwa manufaa yao na taifa kwa jumla.

Sendiga alisema kuwa baada ya suala la nguzo kumalizika wabunge hao wana wajibu wa kuendelea kusukuma ajenda ya Mkoa wa Iringa ya ujenzi wa barabara ya kiwango cha Lami toka Iringa hadi Ruaha Kwa ajili ya kuchochea kasi ya utalii ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha




 

RC SENDIGA ATOA SIKU SABA KWA MKANDARASI PRIPAM KURUDIA UPYA UJENZI WA BARABARA YA ZIZILANG’OMBE NGEREWALA


Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga akiwa kwenye ukaguzi wa barabara zaTARURA manispaa ya Iringa
Barabara ambazo mkuu wa mkoa wa Iringa alikuwa analalamikia kuwa zimejengwa chini ya kiwango
Barabara ambazo mkuu wa mkoa wa Iringa alikuwa analalamikia kuwa zimejengwa chini ya kiwango

Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga akiwa kwenye ukaguzi wa barabara zaTARURA manispaa ya Iringa

 Na Fredy Mgunda, Iringa.

 

Mkuu wa mkoa wa Iringa ametoa siku saba kwa mkandarasi Pripam kurudia upya ujenzi wa barabara ya Zizilang’ombe Ngelewala kwa kujenga chini ya kiwango na kusababisha barabara hiyo kuweka nyufa mwezi mmoja tu toka kukamilika kwake.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa barabara za TARURA Manispaa ya Iringa,mkuu wa mkoa Queen Sendiga alisema kuwa hawezi kufarahishwa hata kidogo akikuta barabara imejengwa chini ya kiwango tofauti na thamani ya fedha iliyotolewa kwa mkandarasi.

Sendiga alisema kuwa haiwezekani barabara nyingi za manispaa ya Iringa zimejengwa kwa kiwango kizuri ispokuwa baarabara ya Zizilang’ombe Kitasengwa kwa kuwa imeanza kupasuka mapema jambo ambalo linaashiria kuwa barabara hiyo imejengwa chini ya kiwango.

Aliwataka wataalam Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini wilaya ya Iringa kuhakikisha wanawasimamia vilivyo wakandarasi ambao wanakuwa wamepewa tenda za ujenzi wa barabara wanajenga kwa ubora unaotakiwa kulingana na thamani ya fedha ambayo imetolewa kutoka serikalini.

Sendiga alisema kuwa baada ya siku saba atafanya ziara kukagua barabara hiyo kama imejengwa kwa kiwango kinachotakiwa kulingana na f thamani ya fedha ambayo imetolewa na serikali la sivyo mkandarasi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Sijaridhishwa na ujenzi wa barabara inayotoka Zizi la Ng'ombe kuelekea Ngelewala Manispaa ya Iringa.Nimetoa siku saba kwa mkandarasi kuijenga upya kwa gharama zake na katika ubora unaotakiwa.” Alisema Sendiga

Aliwaambia wataalam wa TARURA wilaya ya Iringa kufanya kazi kwa weredi unaotakiwa ili kuiondolea serikali sitofahamu inayokuwa inaendelea kwenye mitandao ya kijamii juu ya ubovu wa barabara zinazojengwa katika wilaya ya Iringa.

Sendiga alimalizia kwa kuwapongeza viongozi wa TARURA Iringa kwa kazi wanayoifanya isipokuwa mradi mmoja wa barabara ya Zizilang’ombe Ngelewala ambao umeweka doa la mkoa kwa video za nyufa za barabara hiyo kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

 

Kwa upande wake meneja wa TARURA mkoa wa Iringa Makori George Kisare alisema kuwa wameyapokea mawazo na maagizo yote ya mkuu wa mkoa na watayafanyia kazi haraka ipasavyo kama alivyo agiza.

Akizungumzia swala la kupasuka kwa barabara ya Zizilang’ombe Ngelewala alisema kuwa mkandarasi anawajibu wa kurudia kwa gharama zake kwa kuwa yeye ndio aliyefanya kosa hilo la kiufundi.

 

Alisema kuwa watahakikisha wanamsimamia ndani ya siku hizo saba anafanya marekebisho yanayotakiwa kwenye barabara hiyo.

 


 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube