BREAKING

Sunday 11 July 2021

ARGENTINA MABINGWA WA COPA AMERICA....MESSI AZOA TUZO....



TIMU ya taifa ya Argentina imetwaa taji la Copa America baada ya ushindi wa bao 1-0 mbele ya Brazil katika mchezo wa fainali uliochezwa usiku wa kuamkia leo. 

Ni Angel Di Maria alipachika bao la ushindi dk 22 ambalo lilidumu mpaka dakika ya 90. Argentina pia ilipiga jumla ya mashuti 6 huku mawili yakilenga lango na Brazil wao walipiga 13 na mawili yalilenga lango.

Licha ya uwepo wa staa wa Brazil Neymar Jr ndani ya kikosi hicho bado alishindwa kuipa ushindi timu hiyo ambayo ilikuwa inapambana na staa wa Argentina,  Lionel Messi.

Ilikuwa ni fainali ya kibabe Uwanja wa Maracana ambayo ilishuhudia jumla ya kadi 9 za njano zikitolewa ambapo Argentina wao walionyeshwa 5 na Brazil 4

RAIS SAMIA AKUTANA NA NAIBU MKURUGENZI WA UNEP


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) Bibi Joyce Msuya, Ikulu Jijini Dodoma leo Julai 09,2021.(picha na Ikulu)



 

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube