BREAKING

Friday 12 April 2019

DSTV YAWASHA MOTO KUELEKEA AFCON U17 2019

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Omar Singo (aliyevaa koti) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa zamani wa timu ya Taifa (Taifa Stars) na maafisa waandamizi wa MultiChoice Tanzania wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni maalum ya DStv Inogile ambayo pia inalenga kuhamasisha umma kwa ajili ya mashindano ya AFCON U17 yanayoanza mwisho wa wiki hii. kutoka kushoto (waliasimama) ni Dua Said, Lubigisa Madata, Edibily Lunyamila, Amri Kiemba, Mohammed Hussein na Fikiri Magoso. Kwa waliokaa  ni Sekilojo Chambua, Ronald  Shelukindo na Salum Salum.


Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Omar Singo (aliyevaa koti) akimkabidhi mchezaji wa zamani wa Taifa Stars Amri Kiemba mpira wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni maalum ya DStv Inogile ambayo pia inalenga kuhamasisha umma kwa ajili ya mashindano ya AFCON U17 yanayoanza mwisho wa wiki hii. Wengine wachezaji wa zamani wa Taifa Stars na maafisa waandamizi wa MultiChoice Tanzania. Miongoni mwao ni  Dua Said, Lubigisa Madata, Edibily Lunyamila, Amri Kiemba, Mohammed Hussein na Fikiri Magoso na Sekilojo Chambua.

Katika kuhakikisha kuwa Tanzania inaendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya kimataifa na Watanzania kushuhudia mubashara timu yao DStv imetangaza rasmi kuwa itarusha mubashara michuano ya kombe la AFCON U17 2019 na hivyo kutangaza kampeni maalum ya kuhamasisha ushindi kwa timu yetu ya Serengeti Boys!

Akizungumza katika hafla ya kuzindua kampeni hiyo ya DStv ijulikanayo kama ‘DStv Inogile’, Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania Ronald Baraka Shelukindo amesema kuwa katika kuunga mkono kampeni ya kuifanya nchi yetu ifanye vizuri katika michezo mbalimbali, DStv imehakikisha kuwa michuano mbalimbali ya kimataifa inarushwa mubashara tena katika kifurushi cha chini kabisa cha DStv Bomba cha Sh. 19,000 tu - hivyo kuwawezesha mamilioni ya watanzania kuziona timu zetu na hivyo kuongeza ari ya kuziunga mkono kwa hali na mali.

Kwa upande wa michuano ya AFCON ya vijana inayoana mwishoni mwa wiki hii, Shelukindo amesema DStv itakuwa ikifanya kampeni kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa njia ya mitandao na matangazo mbalimbali kuhamasisha na kuitia nguvu timu ya taifa ili iweze kufanya vizuri

“Hili ni swala la kitaifa, hivyo tunataka watanzania popote walipo waweze kushuhudia timu yetu ikipambana kwa ajili ya sifa ya nchi yetu” alisema Shelukindo na kuongeza kuwa DStv inaonekana kote barani Afrika hivyo kitendo cha kuonyesha michuano hiyo ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini kitaufanya ulimwengu kuyashuhudia mashindano hayo na pia kuitangaza nchi yetu. “Kwa michuano hii kuonekana DStv, ina maana kubwa sana kwa nchi yetu, hii ni njia moja wapo pia ya kuitangaza nchi yetu na Afrika na dunia nzima itambue kuwa na sisi tuna uwezo siyo tu wa kuandaa mashindano haya bali pia wa kuyaonyesha”

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Dr. Omar Singo amesema kuwa kitendo cha DStv kuonyesha mubashara michuano hiyo ni cha kupongezwa kwani ni sifa kubwa kwa nchi yetu. Pia amesema mchango mkubwa unaotolewa na MultiChoice Tanzania katika sekta ya michezo umechangia sana katika kukuza michezo na kuliletea taifa sifa kubwa.
“Serikali inathamini sana michango ya aina mbalimbali inayotolewa na wadau kama DStv katika kukuza michezo hapa nchini. Tunaamini kuwa kwa ushirikiano huu mafanikia haya ambayo tumeanza kuyapata yataendelea na tutafikia azma yetu ya kuwa taifa kubwa kimichezo duniani” alisema Dr. Singo

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake waliowahi kuichezea timu ya Taifa – Taifa Stars ambao walishiriki katika hafla hiyo, mchezaji machachari Amri Kiemba moja kati ya wachezaji nguli waliowahi kuichezea timu ya Taifa ya Tanzania kwa miaka ya nyuma aieleza kuwa , “Kwa mara ya kwanza Tanzania imepewa heshima kubwa kuyaandaa mashindano haya makubwa hivyo ni wajibu wetu sisi watanzania kuonyesha uzalendo na kuwatia moyo vijana wetu ili kuhakikisha wanashinda katika michuano hii na kupata tiketi ya kwenda kwenye mashindano ya dunia nchini  Brazil”. Wanasoka wengine nguli walioshiriki katika hafla hiyo ni Fikiri Magoso, Dua Said, Lubigisa Madata, Amri Kiemba, Edibily Lunyamila na Sekilojo Chambua

Mbali ya michuano ya kombe hili la vijana wa chini ya miaka 17 itakayoanza hivi karibuni, wateja wa DStv pia wataendelea kufurahia maudhui mbalimbali zikiwemo sinema na tamthilia mbalimbali kutoka nje na hapa nyumbani kama vile msimu mpya wa vichekesho vya Kitimtim, tamthilia ya HUBA, Rebeca kipindi maarufu cha Shilawadu Xtra na bila kusahau kipindi kipya cha Maisha Yangu kinachoelezea maisha na mapito ya watu mashuhuri kutoka hapa nyumbani Tanzania vyote vikiwa vinapatikana kupitia chaneli ya Maisha Magic Bongo iliyopo katika kifurushi cha Bomba.

Wednesday 3 April 2019

DC KASESELA: MARUFUKU AKINA MAMA KUJIFUNGULIA NYUMBANI


Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka viongozi wa sekta ya afya katika halmauri ya Iringa vijijini kuendelea kutundika bendera nyekundu kwa wananchi ambao hawana vyoo bora ili kutumisha usafi na afya kwa wananchi wote.Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akimpongeza mwenyekiti wa halmshuri ya wilaya ya Iringa Vijijini Stephen Mhapa kumpa tuzo ya ngao kwa kufanya vizuri katika utunzaji wa mazingira pamoja na kuwa na vyoo safi na bora.
 Baadhi ya washiriki waliofika katika kikao hicho cha utoaji tuzo kwa utunzaji bora wa mazingira na kuwa na vyoo bora
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa sambamba na mkurugeni wa halmashauri ya Iringa vijijini Robert Masunya wakinywa maziwa ya asas

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka viongozi wa sekta ya afya katika halmauri ya Iringa vijijini kuendelea kutundika bendera nyekundu kwa wananchi ambao hawana vyoo bora ili kutumisha usafi na afya kwa wananchi wote.

Akizungumza wakati wa utoaji tuzo kwa wananchi,viongozi,taasisi na jumuiya mbalimbali kwa kutekeleza vizuri kampeni ya kuwa na vyoo bora ambavyo vimeipa ushindi halmasahuri ya Iringa Vijijini kwa kupata tuzo ya usafi hapa nchini.

Kasesela alisema kuwa ofisi ya afya katika halmasahuri ya Iringa Vijijini wamekuwa wakisimamia vizuri swala la afya na kuwa na vyoo bora ambapo wanataraji kuwa halmashauri ya kwanza kwa kuwa na vyoo bora kuliko halmashuri zote za mkoa wa Iringa hadi taifa.

“Nampengeza bibi afya wa hapa amekuwa mkali kuhakikisha hakuna mtu anayeweza kukwamisha zoezi lolote la kuboresha sekta ya afya na kuhakikisha afya za wananchi wa wilaya hii wanakuwa na afya njema” alisema Kasesela

Aidha Kasesela amepiga marufuku wa wazazi kujifungulia majumbani kwa kuwa sio sehemu salama kwa uzazi wa mtoto wakati serikali imefanikiwa kuboresha sekta ya afya ambayo ndio kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano.

“Jukumu la kwanza kwa baba ni kuhakikisha amempeleka mama kliniki kupata huduma ili kuwa na malezi mazuri ya mtoto,hivyo tutaondoa ile njia ya akinamama kujifungulia majumbani kwa kuwa tayari baba atakuwa anajua wajibu wake” alisema Kasesela

Kasesela amewataka watendaji wa kata,vijiji na maafisa tarafa kuhakikisha hakuna mama anajifungulia nyumbani na nitamshughulikia mtendaji yeyeto Yule ambaye hata wachukulia hatua akibaba watakao fanikisha mama kujifungulia numbani.

Awali akitoa hutuba kwa mgeni rasmi mkurugenzi wa halmasahuri ya Iringa Vijijini Robert Masunya aliwataka  watendaji wa halmashauri hiyo kuhakikisha wameendeleza juhudi hiyo ya kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na vyoo bora ili kupunguza na kumaliza tatizo la milipuko ya magonjwa.

“Niwaombeni tena tuendelee kushirikiana vyema katika kuhakikisha halmasahuri ya Iringa Vijijini inaongoza kwa kuwa na mazingira bora na safi kuliko halmashuri zote hapa nchini kwa kuwa tuna mikakati ambayo ni bora sana” alisema Masunya

MKAZI WA MTWARA ALAMBA MAPESA YA VODACOM TUZO POINTS

 Meneja wa Vodacom Tanzania (PLC), mkoani Mtwara, Charles Minungu (kushoto) akiwa na meneja wa vodashop Mtwara, Frank Daud wakimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi 500,000/-mmoja wa washiriki wa kampeni ya Vodacom M-Pesa Tuzo Points, Eladius Lutha mkazi wa Naliendele katika hafla iliyofanyika Mtwara. Kupitia kampeni hii wateja 140 wa Vodacom walizawadiwa shilingi 25,000/-kila mmoja na baada ya kampeni kumalizika wateja 10 wa Vodacom nchi nzima watazawadiwa shilingi 500,000/-kila mmoja
 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube