BREAKING
ROSE MHANDO :MSAMA NI BABA KWANGU ACHENI KUNIGOMBISHA NAYE.   UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA    UTEKAJI WA WATOTO MKUU WA MKOA WA MBEYA JUMA HOMERA AWATAKA WANAFUNZI WA HOLY LAND PRE- & PRIMARY SCHOOL KUKATAA LIFTI   MSAMA ANG'AKA WAIMBAJI WA IN JILI KUPOTOKA MAADILI   DCEA YAFANIKIWA OPERESHENI DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA JAHAZI DAWA ZA KULEVYA   NAIBU WAZIRI MKUU AKARIPIA UZEMBE TANESCO   MHE. RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA MAZUNGUMZA NA RAIS WA CHINA MHE. XI JINPING    MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI CHINA..   RAIS SAMIA NCHINI KENYA-ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI   RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA-KENYA    Blogger Tips and Tricks & Blogger Templates

Monday, April 07, 2025

Friday, 21 February 2025

UPANDIKIZAJI WA MENO BANDIA KWA NJIA YA KISASA MUHIMBILI MLOGANZILA 45 KUNUFAIKA NA HUDUMA








Katika kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita  za kuboresha huduma za afya nchini  Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imenza kambi maalum ya upasuaji wa upandikizaji wa meno bandia kwa njia ya kisasa kwa wagonjwa ambao wamepoteza meno yao kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kambi hiyo Daktari Bingwa wa Afya ya Kinywa na Meno MNH.Mloganzila Dkt. Peter Shempemba  amesema wagonjwa watakao hudumiwa katika kambi hiyo ni pamoja na wale ambao walifanyiwa upasuaji mwishoni mwa mwaka jana na wale ambao wanakuja  kwa mara ya kwanza.

Ameongeza kuwa kundi la kwanza ni wale  ambao walishawapandikiza mizizi ya meno katika awamu ya kwanza na kipindi hiki watapandikizwa meno na kundi lingine  ni wale ambao wanapandikizwa mizizi kwa mara ya kwanza.

“Upandikizaji huu ni wa ubora wa hali ya juu, meno tunayoyapandikiza hayana tofauti na meno ya asili kwakuwa yanapandikizwa moja kwa moja kwenye mfupa wa taya na yanadumu kwa   muda mrefu, hayawezi kutoka kirahisi, mtu ataweza kutafuna vizuri kama kawaida ” amesema Dkt. Shempemba.

Kambi hiyo inafanyika kwa kushirikiana wataalam wa ndani na Daktari Bingwa aliyebobea katika Upasuaji wa Taya kutoka Hospitali za Wochhardt Dkt. Chirag Desai ambapo itafanyika kwa kipindiki hiki cha siku saba kuanzia tarehe 20 hadi 26 Februari, 2025 ambapo takribani wagonjwa 45 watafanyiwa upandikizaji.

No comments:

Post a Comment

 
Copyright © 2016 Shamakala
Designed by Switch International | SHAMAKALA 360
    Twitter Facebook Google Plus Vimeo Videosmall Flickr YouTube